Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, September 20, 2014

Mambo Matano Ambayo Watu Waliofanikiwa Hufanya Mwisho Wa Wiki.

Kwa taratibu nyingi za kazi kwa walioajiriwa na hata aliojiajiri mwisho wa wiki huwa ni siku za mapumziko. Kwa walioajiriwa wanaweza kuwa na siku mbili za mapumziko na waliojiajiri wanaweza kuwa na muda mfupi zaidi ya hapo.

Jinsi unavyoweza kutumia siku hizo za mwisho wa wiki inaweza kukufanya ufikie mafanikio au ushindwe kufikia mafanikio.

Hapa utaona mambo matano ambayo watu wenye mafanikio makubwa hufanya mwisho wa wiki.

1. Hupumzika.

Japokuwa siku hizi ni za mapumziko bado sio watu wote wanapumzika. Wengine hutumia muda huu kufanya kazi nyingine zaidi. Watu wenye mafanikio hupata muda wa kupumzika mwisho wa wiki.

2. Hufanya tathmini wa wiki inayoisha.

Watu wenye mafanikio hutenga muda mwisho wa wiki na kufanya tathmini ya wiki inayoisha. Huangalia ni kipi walishofanikiwa na ni wapi waliposhindwa.

3. Hupanga wiki inayoanza.

Watu wenye mafanikio hutumia mwisho wa wiki kuweka malengo na mipango ya wiki inayofuatia. Mipango hii huwawezesha kuwa na wiki yenye mafanikio makubwa.

4. Hujumuika na ndugu na jamaa.

Watu wengi wenye mafanikio huwa na kazi nyingi sana katikati ya wiki na hivyo kukosa nafasi ya kuonana na ndugu jamaa na marafiki. Hutumia mwisho wa wiki kujumuika na watu ambao hawajakuwa nao kwa muda mrefu.

5. Hukata mawasiliano.

Watu wenye mafanikio hutenga masaa machache mwisho wa wiki kukata mawasiliano yote. Hutumia muda huu kukaa na kutafakari maisha yao zaidi. Katika kukata mawasiliano huondoka kwenye mtandao, huzima simu na vifaa vingine vyote vya mawasiliano.

Na wewe unaweza kufanya mambo haya kila mwisho wa wiki na ukaboresha maisha yako zaidi.

Nakutakia kila la kheri, TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment