Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, September 17, 2014

Mambo Matano(5) Ya Kufanya Wakati Unaelekea Kukata Tamaa.

Maisha yana changamoto nyingi sana. Kuna wakati mambo yanaweza kuwa magumu sana kwako na kuona kama vile huo ndio mwisho wa dunia. Huu ndio wakati ambao unakata tamaa na kuona haiwezekani tena. Kabla ya kufikia hali hii ya kukata tamaa kuna mambo matano ya kufanya ambayo yatabadili kabisa hali yako.

1. Pitia tena malengo yako. Ni kipi hasa kinakusukuma ufanye hicho unachofanya? Ni nini hasa kinakufanya utake kufikia malengo hayo. Ukijua sababu hii itakusukuma zaidi hata mambo yanapokuwa magumu.

2. Kumbuka mafanikio yako. Kabla hujakata tamaa hebu kumbuka ni mambo mangapi umeshafanikiwa mpaka sasa. Kama unafikiri hujafanikiwa kwa lolote, fikiri tena kwa kina.

3. Kumbuka kwamba vikwazo ni sehemu ya maisha. Hakuna safari ya maisha iliyonyooka, kila mtu aliyefikia mafanikio makubwa alikutana na vikwazo vikubwa sana.

4. Fanya kile unachoweza kufanya kwa ubora. Wakati mambo yanapokuwa magumu badala ya kutumia muda mwingi kufikiria kwa nini mambo yanakwenda hivyo, tumia muda wako kufanya kile unachoweza kufanya kwa ubora wa hali ya juu. Utaongeza thamani na kuweza kuondoka kwenye magumu.

5. Kumbuka kwamba hauko peke yako. Kuna watu wengi sana ambao wako tayari kukusaidia katika hali unayopitia. Moja ya njia rahisi za kupata msaada wa watu hawa ni kusoma vitabu vya kukuhamasisha. Kuna vitabu vingi sana vinavyoweza kukuhamasisha na kubadili kabisa mtazamo wako. Soma nusu saa kila siku na utaona mabadiliko makubwa. Kama huna kitabu cha kusoma bonyeza hapa na uweke email yako utatumiwa vitabu.

Fanya mambo haya machache unapokuwa unapitia hali ngumu yenye kukatisha tamaa. Kumbuka ya kwamba kama utakata tamaa ndio unakuwa umeaga mashindano. Ila kama ukiendelea kuvumilia utaibuka mshindi.

Nakutakia kila la kheri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment