Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, September 19, 2014

NILICHOJIFUNZA LEO; Sababu Za Kihistoria Kwa Nini Scotland Ilitaka Kujitenga Na Uingereza.

Jana tarehe 18/09/2014 wananchi wa Scotland walipiga kura ya kuamua kama Scotland ijitenge na kuwa na mamlaka yake kamili au iendelee kuwa sehemu ya Uingereza(United Kingdoms). Matokeo ya kura hiyo yaliyotangazwa leo asubuhi yanaonesha kwamba asilimia 55.3 wamekataa kujitenga na asilimia 44.7 walipiga kura ya kutaka kujitenga. Kwa matokeo hayo Scotland inaendelea kuwa sehemu ya Uingereza.

 

Nilitaka kujifunza zaidi juu ya muungano huu wa Scotland na England.

Mwaka 1602 malkia Elizabert I wa England alifariki dunia bila ya kuacha uongozi kwa watu wa familia yake. Mfalme James I wa Scotland alikuwa msimamizi wa ncho zote mbili lakini kila nchi ilikuwa na uhuru wake.

Mwaka 1707 viongozi wa Scotland walikubali kuungana moja kwa moja na England kutengeneza United Kingdoms. Baadhi ya wananchi wa Scotland hawakufurahishwa na maamuzi haya ni hivyo yalitokea maandamano mengi kupinga muungano huo. Kwa miaka mingi baadhi ya wananchi wa Scotland wamekuwa wanajaribu kujitoa ila wanashindwa.

Mwaka 1999 Scotland waliweza kuwa na bunge lao. Uingereza waliruhusu Scotland kuweza kufanya maamuzi yao juu ya mambo kama afya, nyumba na elimu, lakini bajeti walipangiwa na Uingereza.

Bado wananchi wengi wa Scotland hawakufurahishwa na hili na hivyo manunguniko ya chini chini yalikuwa yakiendelea. Chama cha upinzani kiliposhika nafasi ya kuongoza bunge la Scotland viongozi wake walipendekeza ipingwe kura ya kuamua kuendelea kuwepo chini ya Uingereza au kujitegemea wenyewe.

Haya yote ndiyo yaliyopelekea kwenye kura iliyofanyika jana. Na kama tulivyoona kwenye matokeo asilimia 44 ya wanaotaka kujitenga sio ndogo na hivyo huenda chokochoko zikaendelea.

Tunaweza kujifunza nini hapa kwenye muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar? Karibu kwa maoni.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment