Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, September 18, 2014

Fanya Mambo Haya Matano Kila Siku Asubuhi Na Utakuwa Na Siku Yenye Mafanikio.

Kila siku inayoanza ni siku mpya kwako kuleta mabadiliko kwenye maisha yako na dunia kwa ujumla. Hijalishi siku ya jana ilikuwaje kwako, ila leo unayo kwenye mikono yako na ni uamuzi wako kama unataka kuifanya siku yenye mafanikio au unataka kuipoteza.

Fanya mambo haya matano kila siku asubuhi na utakuwa na siku yenye mafanikio makubwa.

1. Amka asubuhi na mapema. Unapoamka asubuhi na mapema unakuwa na faida ya kuwa macho kabla ya watu wengine. Muda huu ni muda wenye utulivu na unaweza kufanya mambo yako vizuri.

2. Soma nusu saa kila siku. Baada ya kuamka mapema, tumia nusu saa ya kwanza akujisomea kitabu kizuri kitakachokufundisha na kukuhamasisha. Kama huna kitabu bonyeza hapa na uweke email yako utatumiwa vitabu.

3. Pangilia siku yako. Andika ni mambo gani matatu ambayo ukiyakamilisha siku ya leo yatakuletea mafanikio makubwa. Pangilia jinsi utakavyofanya mambo hayo.

4. Fanya mazoezi. Unapofanya mazoezi asubuhi unauweka mwili wako katika hali ya uchangamfu na ukakamavu, hata akili yako inaweza kufanya kazi vizuri.

SOMA; Faida 5 za kukimbia dakika 5 kila siku.

5. Pata kifungua kinywa. Ni muhimu sana kupata kifungua kinywa asubuhi. Hii ni kwa sababu unapolala ni kama unakuwa umefunga na hivyo unapoamka mwili unakuwa hauna chakula cha kutosha.

Haya ni mambo ambayo unaweza kuanza kuyafanya mara moja na ukaona mabadiliko kwenye maisha yako. Hebu anza kuyafanya sasa na upate mafanikio kwneye maisha yako.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment