Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, September 17, 2014

Faida 5 Za Kukimbia Dakika 5 Kila Siku.

Kila mtu anafahamu kwamba mazoezi ni kitu muhimu sana kwa afya njema na maisha kwa ujumla. Lakini inapokuja kwenye kufanya mazoezi, watu wengi hufikiri ni lazima kwenda kwenye eneo maalumu la mazoezi au kununua vifaa maalumu. Kwa hiyo ukosefu wa vifaa hivyo na ukosefu wa muda pia hufanya watu wengi kushindwa kufanya mazoezi.

Leo utajifunza faida tano za kukimbia dakika tano kila siku. Nani ambaye hana dakika tano kwenye siku yake? Nani ambaye hana eneo la kukimbia dakika tano? Jibu ni hakuna.

Hizi ndio faida 5 za kukimbia dakika 5 kila siku.

1. Inapunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo. Magonjwa ya moyo sasa hivi yamekuwa tishio sana kutokana na watu kutofanya mazoezi.

2. Utaishi muda mrefu. Kwa kufanya mazoezi utakuwa na afya imara na hivyo utaweza kuishi muda mrefu zaidi.

3. Inakusaidia kuwa katika hali nzuri. Kwa kufanya mazoezi unakuwa katika hali nzuri inayokuwezesha kufanya majukumu yako kwa ufanisi zaidi.

4. Unapata usingizi mzuri. Kwa kufanya mazoezi, mwili unapata nafasi nzuri ya kupumzika unapolala, na hivyo kuwa na usingizi mzuri.

5. Kuongeza ufanisi wa akili. Mazoezi hasa yanapofanywa asubuhi huifanya akili kuwa katika ufanisi wa hali ya juu.

Hizi ndio faida tano unazoweza kuzipata kwa kukimbia dakika tano kila siku. Anza leo jioni au kesho asubuhi ili kuepuka magonjwa na pia kuongeza ufanisi wa akili yako.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment