Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, September 22, 2014

Mambo 5 Muhimu Ya Kufanya Kabla Hujalala Leo.

Siku ya leo ndio inaelekea kuisha na kwa siku nzima ya leo umepitia mambo mengi sana. Kuna mengi umefanikiwa kufanya leo na pia kuna ambayo umepata changamoto kubwa.

Hata kama siku yako ilikuwa mbaya kiasi gani, kuna mambo mazuri uliyojifunza kwa siku hii.

Hapa kuna mambo matano muhimu unayotakiwa kufanya kabla ya kulala.

1. Fanya tathmini ya leo.

Fanya tathmini ujue umeitumiaje siku ya leo. Ni mambo gani umefanikiwa kufanya na ni yapi umeshindwa. Chukua kalamu na karatasi uandike mambo matatu uliyofanikiwa kufanya leo ambayo yamekusogeza kwenye mafanikio. Pia andika mambo matatu ambayo inabidi uyarekebishe.

2. Pangilia kesho yako.

Kabla ya kulala pangilia siku yako ya kesho. Andika mambo makubwa matatu unayohitaji kukamilisha kesho na uanze kuyafanyia kazi mapema kesho.

3. Pata muda wa kujisomea.

Tenga muda mchache wa kusoma kitabu, ndio kusoma kitabu cha kawaida.

4. Lala mapema.

Kwa kawaida watu wengi huchelewa kulala kwa sababu ambazo sio za msingi. Inaweza kuwa kuangalia tv au movie, kuperuzi mitandao mbalimbali na kadhalika. Ukilala mapema unaweza kuamka mapema ukiwa na nguvu.

5. Kaa mbali na mwanga wa vifaa.

Sasa hivi tunatumia vifaa vingi vinavyotoa mwanga mkali. Simu, kompyuta, tv hivi vinatoa mwanga mkali sana. Mwanga huu unakufanya uchelewe kupata usingizi. Hivyo ni vyema usitumie simu au kompyuta kitandani.

Anza kufanya mambo hayo matano leo na utaona mabadiliko kwenye maisha yako.

Tuko pamoja.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment