Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, September 17, 2014

Mbinu 5 Zitakazokufanya Uwe Mbunifu Zaidi.

Iwe umeajiriwa au umejiajiri unalipwa kulingana na ubunifu wako. Kama unataka kulipwa zaidi, yaani kupata wateja wengi zaidi au kupata kipato kikubwa zaidi ni muhimu kila siku kuongeza ubunifu wako kwenye kile unachofanya.

Hizi hapa ni mbinu tano zitakazokufanya uwe mbunifu zaidi;

1. Pata muda wa kupumzika. Tafiti zinaonesha kwamba mtu anapokuwa amechoka, uwezo wake wa kufikiri unakuwa chini sana.

2. Fikiria kama mtoto. Watoto wana ubunifu mkubwa sana kwa sababu hufikiri bila ya kujiwekea mipanga. Anza kuondoa mipaka kwenye fikra zako na ufikiri kwa uhuru zaidi.

3. Fanya mazoezi. Mazoezi ni muhimu sana ili kuweka akili yako katika ufanisi wa hali ya juu.

4. Jipe muda wa mwisho wa kukamilisha kitu. Kama kuna jukumu unafanya jipe muda ambao ni lazima uwe umemaliza. Jinsi muda unavyokaribia kuisha utajikuta unapata mawazo mazuri ya kufanya.

5. Usikatae mawazo mabaya haraka. Wakati unafikiri unaweza kuja na mawazo mengi sana. Usianze kujiwekea mipaka kwamba hili ni zuri na hili ni baya, yaangalie yote vizuri na ujue ni kipi cha kufanya.

Tumia mbinu hizi kila siku na utaona ubunifu wako ukiongezeka.

Muhimu; Kila siku fanya unachofanya kwa ubunifu zaidi.

TUKO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment