Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Tuesday, June 30, 2015

UKURASA WA 181; Kitu Cha Kufanya Pale Watu Wanapokuwa Hawakuamini Kama Unaweza.

Kama unataka kufanya jambo jipya, kama unataka kufanya jambo tofauti na wengine walivyozoea kufanya, naweza nikakuhakikishia jambo moja, WATU HAWATAKUAMINI.
Watu hawatakuamini kwamba unaweza kufanya jambo hilo. Watu hawatakuamini kwamba kuna uwezekano wa jambo hilo kufanyika kwa tofauti. Na hapa ndipo watu wengi hukata tamaa na kuamua kuacha. Na hivyo watu wale walioshindwa kuwaamini mwanzo wanakuwa sahihi na wanazidi kupata nguvu ya kuwaambia wengine kwamba hawawezi au haiwezekani.
Leo nataka nikuulize, je unajua unatakiwa kufanya nini pale ambapo watu hawakuamini kwamba unaweza? Au umekuwa mtu wa kukatishwa tamaa mara nyingi na wewe kukubali?
Sasa kuna kitu kimoja muhimu sana unachotakiwa kufanya pale ambapo watu hawakuamini kama unaweza. JIAMINI WEWE MWENYEWE. Wewe ndio umekuja na mawazo hayo uliyonayo, wewe ndiye ambaye umekuwa unafikiria usiku na mchana jinsi unavyoweza kubadili hali ya mambo. Wewe ndiye uliyefikiria na kuona kuna njia mbadala na ambayo inawezekana. Sasa kwa nini ukubali kumsikiliza mtu ambaye amefikiria kwa upande mmoja tu wa kwamba vitu haviwezekani?
SOMA; Hukuja Na Maelekezo Kwa Mtumiaji Na Kwa Nini Ufurahie Hili.
Kama utawasikiliza watu hawa utakuwa hujajitendea haki kabisa, kwa sababu hata watu hawa sio kwamba wana uhakika haiwezekani, ni vile tu hawajawahi kuona mtu mwingine akifanya hicho unachotarajia kufanya.
Kama watu hawaamini kwamba unaweza, huo ndio wakati wa kujiamini na hata kufurahia sana kwenye maisha yako. Unajua ni kwa nini? Kwa sababu unapoanza kufanya kitu ambacho wengi wanaona hakiwezekani, jua unafanya kitu ambacho sio cha kawaida, unafanya kitu kikubwa. Na mafanikio yanakuja kwa kufanya vitu ambavyo sio vya kawaida.
TAMKO LA LEO;
Najua ya kwamba pale ninapopanga kufanya jambo kubwa, watu wengi watashindwa kuniamini. Huu ni wakati muhimu sana wa mimi mwenyewe kujiamini na kuendelea kuweka juhudi. Hakuna mafanikio yanayokuja kwa kufanya vitu ambavyo ni vya kawaida. Hivyo ninapoona watu hawaniamini kwa kitu kikubwa ninachotaka kufanya, najua hapo ndio penye mafanikio.
Tukutane kwenye ukurasa wa 182 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Monday, June 29, 2015

UKURASA WA 180; Pamoja Na Ushauri Mzuri Utakaopewa, Bado Kitu Hiki Utafanya Wewe Mwenyewe.


Unapokuwa unahitaji kufanya maamuzi ambayo huenda ni magumu kwenye kazi yako, biashara yako au hata maisha yako kwa ujumla, huwa unahitaji kupata ushauri. Unaweza kupewa ushauri mzuri sana kutoka kwa watu mbalimbali ambao unaweza kuwa unawaamini sana.
Pamoja na ushauri huu muhimu bado wewe mwenyewe ndio utahitaji kufanya maamuzi ya mwisho. Wewe ndio utakayekaa chini na kufanya maamuzi ambayo utakuwa tayari kuishi nayo.
Hivyo ni muhimu sana wewe uwe na uwezo wa kufanya maamuzi. Huwezi kutegemea tu watu watakavyokushauri, kwa sababu watu mbalimbali watakuwa na ushauri tofauti. Kama hutakuwa na uwezo mzuri wa kufanya maamuzi ambayo utakuwa tayari kuishi nayo, utaishia kufanya maamuzi ambayo yatakupoteza.
SOMA; Mambo Kumi(10) Unayotakiwa Kubadili Leo Ili Kufikia Mafanikio Makubwa.
Nakumbuka siku sio nyingi rafiki yangu mmoja aliniomba ushauri kuhusiana na maamuzi ya kibiashara aliyokuwa anataka kufanya. Nilimpa ushauri wangu na mambo muhimu anayohitaji kuzingatia. Baadae alinipigia kuniambia kwamba ameamua kufanya tofauti na nilivyomshauri. Nilistuka kidogo kwa sababu alichokuwa anakwenda kufanya ni kosa kubwa sana ambalo mimi binafsi nimewahi kufanya na likanigharimu na nimekuwa naona wengi wakifanya kosa hilo na linawagharimu sana. Nilijaribu kumwelewesha, labda kama hakuwa amenielewa vizuri, lakini alisisitiza kuendelea na kile alichopanga kufanya.
Nilijikumbusha kwamba yeye pekee ndio mwinye kufanya maamuzi ya mwisho na hivyo nilimwambia kila la kheri kama ndio maamuzi ambayo yuko tayari kuishi nayo. Siku chache baadae alinipigia na kuniambia hataendelea tena na mpango ule, hapa nilichanganyikiwa zaidi na sikutaka hata kujua zaidi.
Katika maisha yako jiandae kuweza kufanya mamauzi ambayo ni sahihi kwako na sio ya kusukumwa na mtu au kitu chochote.
TAMKO LA LEO;
Najua ya kwamba nitapata ushauri kutoka kwa watu wengi. Najua ushauri huu utakuwa mzuri sana, lakini mwisho wa siku ni mimi pekee nitakayehitaji kufanya maamuzi ambayo ni sahihi kwangu na nitakuwa tayari kuishi nayo. Kila siku nitajijenga ili niweze kufanya maamuzi ambayo yatakuwa bora kwangu.
Tukutane kwenye ukurasa wa 181 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Sunday, June 28, 2015

UKURASA WA 179; Unataka Kuwazidi Wengine? Umeshapotea.

Kwanza kabisa nikiri kwamba mimi huwa napinga sana dhana ya kushindana. Ndio kuna wakati ushindani unaonekana ni mzuri, lakini tatizo linakuja kwamba ukishakuwa na akili ya kushindana ndio unadumaa.
Kama unakuwa na akili ya kushindana maana yake lengo lako kubwa ni kuwazidi wengine. Kuwa wa kwanza, kuwa bora zaidi ya wengine.
Sasa tuseme labda unafanya biashara eneo ambalo watu wanafanya biashara kwa mitindo ya kizamani. Mtu akipata faida kidogo siku moja kesho yake analala, anaona amewini maisha. Na wewe ukawa unashindana nao, unafikiri utafika wapi?
Au tuseme unafanya kazi kwenye eneo ambalo kila mtu anakazana kununua gari na wewe ukawa na akili ya kushindana, unafikiri mafanikio yako makubwa kwenye maisha yatakuwa nini. Ukishanunua gari bora zaidi ya wengine tayari umekwisha. Utaonekana wewe ndio wewe na kile kiroho chako cha kushindana kitafurahi, kitakufanya uone maisha umeyamaliza.
SOMA; Sheria Tatu Muhimu Za Kufanikiwa Kwenye Maisha.
Lengo lako sio kuwa zaidi ya wengine, kama unataka kufikia mafanikio makubwa. Bali lengo lako ni wewe kuwa bora zaidi yako wewe mwenyewe. Wewe kuwa bora kuliko wewe mwenyewe. Wewe kuwa mbele yako mwenyewe. Hii ina maana kwamba leo uwe bora zaidi ya ulivyokuwa jana, leo ufanye kazi yako au biashara yako kwa ubora zaidi kuliko ulivyokuwa unafanya siku zilizopita. Leo upate kipato kikubwa zaidi ya ulichopata siku zilizopita. Leo upate mteja mpya tofauti na uliokuwa nao zamani.
Hiki ndio unatakiwa kupigania, hiki ndio unatakiwa kufanya kila siku. Na sio kuingia kwenye mbio za kundi na kujiingiza kwenye mashindano ambayo hujui hata yanakupeleka wapi.
TAMKO LA LEO;
Najua kukazana kuwa bora zaidi ya wengine ni kupoteza muda wangu na kujizuia kufikia mafanikio makubwa. Kuanzia sasa nitakazana kuwa bora zaidi yangu mwenyewe, nitakazana kuwa mbele yangu mwenyewe, kwa sababu najua kuna uwezo mkubwa uliopo ndani yangu ambao bado sijautumia. Nitahakikisha nautumia sasa ili niweze kufika mbali zaidi ya hapa nilipo sasa.
Tukutane kwenye ukurasa wa 180 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Saturday, June 27, 2015

UKURASA WA 178; Lakini Nitapitwa.... (Sababu Ya Kijinga Inayokufanya Upoteze Muda)

Kama umejitoa ili kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako, unahitaji kujifunza jinsi ya kutumia muda wako vizuri. Na kwa kuwa siku ina masaa 24 tu na hakuna anayeweza kuyazidisha, hakuna njia ya kuongeza muda ambao tunao.
Kwa kuwa tunahitaji muda mwingi zaidi wa kufanya kile tunachofanya kwa ubora, basi tunahitaji kupunguza mambo mengi tunayofanya ili tuokoe muda mwingi.
Ili kupata muda mwingi nimekuwa nawashauri watu kufanya yafuatayo, ambayo hata mimi nafanya; usifuatilie habari, punguza sana muda unaotumia kwenye mitandao ya kijamii, tenga muda wa kuwa mbali na simu yako pale ambapo unafanya kazi inayohitaji umakini wako.
Watu wamekuwa wakipinga sana baadhi ya mambo haya, hasa kutokufuatilia habari au kukaa mbali na simu. Watu wamekuwa wakisema lakini nitapitwa.....
Najua na wewe unaona usipoangalia au kusoma habari siku moja unaona unapitwa. Yaani unapitwa na habari ya mtu aliyejinyonga huko mpanda, ukishaisikia inakusaidia nini? Utaniambia kuna habari muhimu kuhusu mambo yanayoendelea. Kama habari ni muhimu kweli zitakufikia tu. Kwa mfano kama nchi inaingia vitani, utajua hata kama huangalii habari. Lakini mambo ya mgombea gani kapata wadhamini wangapi sio habari za mtu makini kushabikia, ni kupoteza muda wako.
SOMA; Unacho Kila Unachohitaji Ili Kufanikiwa.
Asilimia kubwa ya watu wanaotumia simu ni kama wamefunga ndoa na simu hizo. Kila dakika mtu upo na simu na hazipiti dakika tano unaangalia kama kuna mtu katuma ujumbe au kapiga hukusikia. Na hata unapokwenda kulala, unaiweka pembeni ya kichwa chako, ili usipitwe. Unapoteza muda mwingi sana, ni vigumu kufanya kazi yenye maana huku unajibu ujumbe wa simu au kupokea simu kila mara. Ni afadhali uweke simu hiyo kimya kabisa na ufanye kazi yako, bila ya kuiangalia. Utasema lakini watu watanipigia na kunikosa, nitakosa dili nzuri. Ukweli ni kwamba, na hapa nakuambia kwa uzoefu, kama mtu ana shida ya kuwasiliana na wewe kweli, atakutafuta hata mara kumi. Ila anayepiga mara moja na kuacha, hata ukija kumpigia baadae hakuna jambo kubwa na la haraka sana alilokuwa anakuambia. Mwingine atasema labda mtoto wangu ataumwa ghafla inabidi nipate taarifa, sawa umeshazipata unafanya nini? Maana hata kama wewe ni daktari huwezi kumtibu mtoto wako, itabidi apelekwe tu hospitali. Sisemi usikae na simu siku nzima, bali masaa machache hivyo taarifa hizi utazipata baadae na utafanya maamuzi sahihi, huku umeshakamilisha kazi uliyopanga kufanya.
TAMKO LA LEO;
Nimekuwa najidanganya kwamba nitapitwa na hivyo kuwa karibu na habari, kuwa karibu na mitandao na kuwa karibu na simu yangu kila mara. Hali hii imekuwa inanipotezea muda wangu mwingi kwa kufuatilia vitu visivyo na maana na kukosa muda w akufuatilia yale ambayo yataniletea mafanikio. Kuanzia sasa natenga muda wangu wa kufanya mambo muhimu na muda huu hautaingiliwa na kitu kingine chochote.
Tukutane kwenye ukurasa wa 179 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Friday, June 26, 2015

UKURASA WA 177; Ndio, Kwa Hiyo...

Ni vigumu sana kuweza kufanikiwa kwenye biashara, ndio kwa hiyo unahitaji kujipanga vizuri na kutokukata tamaa ili uweze kufikia mafanikio unayotarajia.
Umri wangu ni mdogo/mkubwa sana kuweza kuanza kufanya jambo hili sasa. Ndio kwa hiyo unahitaji kuwa wa tofauti, licha ya umri wako kuwa usiotegemewa bado unaweza kuweka juhudi na ukafikia kile ambacho unataka.
Nimejaribu mara nyingi sana lakini nimeshindwa. Ndio kwa hiyo unahitaji kubadili mbinu zako, kuendelea kufanya kitu kile kile na kutegemea majibu tofauti ni ujinga wa kupindukia.
Napenda sana kuanza biashara ila sina mtaji. Ndio kwa hiyo unahitaji kufikiria njia ya kuweza kuanza biashara kidogo au kutafuta kitu kingine cha kukuingizia kipato kwa sasa ili ujiandae na kuingia kwenye biashara unaotazamia.
SOMA; Vitu Ambavyo Ni Rahisi Kufanya.... Na Madhara Yake.
Ukweli ni kwamba mtu yeyote anaweza kuja na sababu zaidi ya elfu moja kwa nini hawezi kufanya kitu fulani. Ila sababu hizi haziwezi kusaidia chochote.
Watu waliofanikiwa wanakuja na sababu lakini huzipatia sababu zao suluhisho ambalo hulifanyia kazi na hatimaye kufanikiwa.
Usiwe mtu wa kutafuta au kutoa sababu tu. Hebu anza kuzipa sababu zako suluhisho na utaona fursa nyingi sana za kukufikisha kwenye kile unachotaka.
Wakati wowote unapokuja na sababu tafadhali sana mbele yake ongeza NDIO KWA HIYO....
TAMKO LA LEO;
Najua sababu yoyote ninayojipa haiwezi kunifikisha kule ninakotaka kwenda. Ila ninapoifanyia kazi sababu ninayoipata ndio natoa nafasi kubwa kwangu kuweza kupata kile ninachotaka. Najua mjinga yeyote anaweza kuja na sababu kwa nini hafanikiwi na hii ndio inazidi kumfanya asifanikiwe. Lakini mimi sio mmoja wa wajinga hawa, kila sababu ninayopata lazima niipatie ufumbuzi.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Thursday, June 25, 2015

UKURASA WA 176; Hiki Ni Kipimo Kibovu Sana Cha Kupima Mafanikio Yako.

Kuna watu walikaa chini wakaamua kwamba kuwe na mtihani mmoja na wanafunzi wote waufanye, atakayepata maksi nyingi ndio amefaulu, atakayepata chache amefeli.
Kuna watu pia wamekaa wakakubaliana kwamba ukiwa na magari ya kifahari, ukawa na nyumba ya kifahari na fedha isipokuwa tatizo kwako basi wewe umefanikiwa.
Vyote hivi vinaweza kuwa vipimo kwa sababu vitakusukuma na wewe uweze kufika mbali zaidi ila sio vipimo sahihi kwa mafanikio yako. Hivi ni vipimo vibovu sana kwako kujipima kama umefikia mafanikio au la.
Hakuna kipimo kimoja kinachoweza kupima mafanikio ya watu wote kwa kigezo kimoja, ndio maana mara zote nimekuwa nakusisitizia sana usijilinganishe na wengine. Ni vizuri kujua wengine wanafanya nini, ila usijione umeshinda au umeshindwa kwa sababu ya kile unachofanya unavyokilinganisha na wengine wanavyofanya.
Kwa kifupi ni kwamba usipime mafanikio yako kwa vigezo ambavyo vimewekwa na watu wengine. Utakuwa hujitendei haki na kinaweza kuwa kikwazo kikubwa sana kwako kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako.
Sasa ujipime na nini?
1. Jipimie kwa malengo makubwa uliyojiwekea? Je umeyafikia? Na kama hujayafikia ni kwa nini na umejifunza nini? Hakikisha malengo hayo ni makubwa; soma hapa kujua umuhimu wa malengo makubwa; Ni Bora Kuweka Malengo Makubwa Na Kushindwa Kuliko Kuweka Malengo Madogo Na Kushinda.
2. Jipime kwa juhudi unazoweka, je ni juhudi za kutosha? Je zinaleta matunda unayotarajia?
3. Jipime kwa ulivyokuwa jana na utakavyokuwa leo. je leo uko bora zaidi ya ulivyokuwa jana? Je kadiri siku zinavyokwenda unazidi kuwa bora au unazidi kuwa hovyo?
4. Jipime kwa maisha ya wengine uliyogusa. Je ni kwa kiasi gani watu wengine wamenufaika kwa kile ambacho unafanya? Je wataendelea kunufaika na kile unachofanya? Je watakukumbuka hata usipokuwepo?
Hivi ni baadhi ya vigezo sahihi kwako kujipima kama kweli umefikia mafanikio au la. Vigezo vinavyotengenezwa na wengine ni sumu kwako, usijaribu kuvitumia.
TAMKO LA LEO;
Nimekuwa napima mafanikio yangu kwa vigezo ambavyo vimewekwa na watu wengine. Njia hii imekuwa inaniumiza na kunirudisha nyuma. Kuanzia sasa nitapima mafanikio yangu kwa vigezo vyangu mwenyewe na nitahakikisha navifikia na kuweka vikubwa zaidi ili kila siku niwe bora zaidi ya siku iliyopita.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, June 24, 2015

UKURASA WA 175; Ni Bora Kuweka Malengo Makubwa Na Kushindwa Kuliko Kuweka Malengo Madogo Na Kushinda.


Kwa jinsi tulivyolelewa na kukuzwa, kushindwa ni kitu cha aibu sana, ni kitu kinachostahili adhabu kubwa na kama utashindwa basi wewe ni mtu ambaye hufai. Si ndio tulivyofundishwa shuleni? Na ndio maana tulipewa adhabu kali pale ambapo tulishindwa kwenye kazi au mtihani.
Kinyume na ilivyo kwenye elimu na hata kwenye malezi uliyopewa, kwenye maisha ya kawaida kushindwa ni kitu kizuri sana. Kushindwa ni muhimu kwa sababu unajifunza mambo mengi kuliko unavyoshinda. Japo wengi hawaamini hili na hawataki hata kusikia.
Kwa woga wetu wa kushindwa, wengi wetu wamekuwa wakiogopa hata kuweka malengo makubwa kwa kuogopa kushindwa. Mtu anaona kama aliweka malengo makubwa na akashindwa kuyafikia basi ni sawa na kujidhalilisha. Kwa sababu hiyo anaweka malengo madogo ambayo yapo ndani ya uwezo wake na anayafikia vizuri.
SOMA; Hii ndio faida ya kushindwa.
Sasa kuweka malengo ambayo yako ndani ya uwezo wako na ukayafikia vizuri, unafikiri ni kitu gani kikubwa umejifuza? Hakuna, yaani umeendelea kuwa vile ulivyokuwa na huwezi kufikia mafanikio makubwa.
Lakini unapoweka malengo makubwa, malengo ambayo hata wewe mwenyewe yanakuogopesha, haya ndio malengo ambayo yatakusukuma ufanye zaidi na hata kama hutayafikia, utamaliza ukiwa mbali kuliko ungeweka malengo madogo.
Hivyo kuanzia leo na kwa muda wote uliobakia, malengo yote uliyoweka mwanzo yazidishe mara kumi na anza kuangalia ni njia gani zitakufikisha pale. Ndio weka mara kumi halafu umiza kichwa chako na weka juhudi mpaka tone la mwisho. Huenda hutafikia mara 10 lakini utafikia mara 5 au hata mara 3 ambayo ni bora zaidi ya kama ungeendelea na lengo lako la mwanzo.
TAMKO LA LEO;
Najua naogopa sana kushindwa, najua naona kushindwa ni kama aibu kwangu. Lakini nimeshajua kwamba kushindwa ni sehemu muhimu sana kwenye maisha ya kila siku. Kuanzia sasa nitaweka malengo makubwa na ambayo yatanisukuma kila siku ili kufanya zaidi ya ninavyofanya sasa. Kwa kuweka malengo makubwa hata kama sitayafikia nitajifunza na kuwa mbali zaidi kuliko nikiweka malengo madogo na ambayo naweza kuyafikia.
Tukutane kwenye ukurasa wa 176 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tuesday, June 23, 2015

UKURASA WA 174; Je Unafanya Kile Unachopenda Au Unachotegemewa Kufanya?(Na Mbinu Za Kuweza Kufanya Kile Unachopenda Kufanya)

Ni jambo la kushangaza kwenye maisha kwamba baadhi yetu tunaishi maisha ambao hata hatuyajui. Tunatumia muda wetu mwingi kuishi maisha ambayo hata hatukupanga kuyaishi. Tunajikuta tunaishi maisha tofauti kabisa kwa sababu tunalazimika kuishi maisha ambao kila mtu anaishi.
Tumeshazungumza sana kuhusu kuishi maisha ya wengine, leo ngoja tuzungumze kufanya kazi za wengine.
Kama imetokea kazi unayoifanya ikawa ndio kitu unachopenda kufanya upo kwenye nafasi nzuri sana. Na mafanikio yapo mbele yako. Ila ni nadra sana kuwa kwenye kundi hili ambalo lina watu wachache, asilimia 3 tu ya watu kwenye jamii.
Kama upo kwenye asilimia 97 iliyobaki, maana yake unafanya kazi unayofanya kwa sababu tu ndio unayotegemewa kufanya. Unafanya kwa sababu unafikiri ndio njia pekee ya kukupatia wewe kipato. Na kila mtu ameshakuaminisha hivyo na huwezi kuona nafasi ya kuondoka kwenye hilo.
SOMA; Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu Kinaitwa SELF-IMPROVEMENT 101.
Kama unafanya kile ambacho kila mtu anakutegemea ufanye, leo nataka nikupe mbinu ya kuanza kufanya kile ambacho unapenda kufanya.
Kwanza kabisa jua ni kitu gani unapenda, licha ya kazi ambayo sasa unaifanya. Amua ni kipi unapenda kukifanya na kila ukikifanya unajisikia vizuri sana. Iwe ni sanaa, iwe ni kitu cha kuwasaidia wengine, iwe ni mchezo na kadhalika. Chochote kile kinachokufanya ujisikie vizuri ni kitu muhimu sana kwako.
Baada ya kujua kitu hiki panga ni vipi unaanza kukifanya. Jua kwa sasa upo wapi na utaanzia wapi ili kufika wapi.
Kisha tenga muda kila siku wa kufanya kitu hiki. Kama kinahusiana na biashara, tenga muda kila siku wa kufanya biashara hiyo. Huna haja ya kuanzia mbali, anza kidogo na anza kwa kutafuta mteja mmoja, mpatie bidhaa au huduma nzuri na hakikisha unabadili maisha yake kupitia kile unachofanya. Tafuta tena mteja mwingine na fanya kama ulivyofanya kwa mteja wa kwanza na endelea kuboresha. Wakati huu bado unaendelea na kazi yako hivyo hujali sana kuhusu kipato, bali kutoa kitu bora ambacho kitawafanya wengine wakuzungumzie.
Ukiendelea hivi kwa muda, miaka kadhaa utafikia kuwa na wateja wengi kiasi kwamba kipato unachopata kwenye ajira yako ni kidogo ukilinganisha na hiki cha pembeni. Na hapo unakosa muda wa kuwahudumia wateja wako wote. Hapa ndio unaacha kazi na kufanyia kazi kitu hiko moja kwa moja.
Uko makini na umejitoa kutengeneza kitu kama hiki na unahitaji muongozo zaidi? Tuwasiliane, niandikie email kwenye makirita@kisimachamaarifa.co.tz na niambie ni nini unataka kufanya na tutajadili jinsi ya kuweza kupata muongozo mzuri. Ukiwa mwenyewe ni rahisi kukata tamaa, ukiwa na mwongozo utapata hamasa ya kwenda zaidi.
TAMKO LA LEO;
Najua ninachofanya sasa sio kile ambacho napenda kufanya bali ambacho kila mtu anategemea nifanye, ili nipate kipato cha kuendesha maisha. Sasa nimeamua kutenga muda kila siku na kuanza kufanyia kazi kile ambacho ninapenda kufanya. Nitaweka juhudi kubwa kwenye kitu hiki na najua kwa muda wa mbeleni kitakuwa chanzo changu kikubwa cha mapato.
Tukutane kwenye ukurasa wa 175 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Monday, June 22, 2015

UKURASA WA 173; Maamuzi Uliyofanya Awali Na Maamuzi Mapya.

Mambo unayofanya sasa yanatokana na maamuzi uliyofanya awali. Na maamuzi haya uliyofanya awali yalitokana na uelewa uliokuwa nao kwa kipindi hiko unafanya maamuzi hayo.
Sasa swali linakuja kwako je sasa hivi bado una uelewa kama uliokuwa nao kipindi unafanya maamuzi? Kama jibu ni ndio basi endelea na kile unachofanya.
Kama jibu ni hapana, maana yake uelewa wako ni tofauti na ulivyokuwa zamani wakati unafanya maamuzi. Je kwa kuwa na uelewa wa tofauti sasa upo tayari kubadilika na kufanya maamuzi mapya ambayo yatakuwa bora zaidi?
Hili ni swali la msingi sana nakuuliza kwa sababu watu wengi wakishafanya maamuzi na kuona mambo yanakwenda vizuri wanajisahau, wanaendelea kufanya kile walichozoea kufanya mpaka wanapojikuta kwenye wakati ambao wanachofanya hakifai tena.
Mtu anaingia kwenye kazi lakini anaendelea kufanya kazi yake kwa mbinui zile zile alizokuwa anatumia awali. Wanakuja vijana wenye mawazo mapya na wanaweka mbinu mpya na mtu huyu anaanza kuchukia na kuona nafasi yake ipo hatarini.
Mtu anaingia kwenye biashara lakini miaka nenda miaka rudi anafanya kwa mbinu zile zile, wakija watu wapya na mbinu mpya wanamwondoa kwenye biashara ile anabaki kulia kwamba kafanyiwa mchezo mchafu.
Kadiri uelewa wako unavyoongezeka, boresha maamuzi yako na fanya mabadiliko yanayostahili. Dunia inabadilika, ni lazima na wewe ubadilike. Nafikiri umeona hapo nimekuambia NI LAZIMA ubadilike, sio unaombwa, ndivyo dunia inavyokutaka, la sivyo unaachwa nyuma, unapotezwa.
Kama mpaka sasa hujasoma kitabu, JINSI YA KUNUFAIKA NA MABADILIKO YANAYOTOKEA KWENYE MAISHA unasubiri nini? Bonyeza hayo maandishi kujipatia kitabu hiki kitakachokuandaa vizuri na mabadiliko.
TAMKO LA LEO;
Najua ya kwamba maamuzi niliyofanya awali yalitokana na uelewa wangu kwa kipindi kile. Najua kwamba mpaka sasa uelewa wangu umebadilika na hata dunia imebadilika pia. Nahitaji kufanya maamuzi mapya kulingana na mabadiliko ya sasa na uelewa nilio nao. Na kuanzia sasa mabadiliko kwangu yatakuwa ni mara kwa mara, sitafanya kitu chochote kwa mazoea.
Tukutane kwenye ukurasa wa 174 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Sunday, June 21, 2015

UKURASA WA 172; Tatizo La Kuweka Kinyongo...

Ni kwamba unakosa nafasi ya kufuatilia mambo mengine muhimu kwako.
Unaweza kujiaminisha kwamba kinyongo ulichomwekea mtu unastahili kabisa.
Alininyanyasa sana nilipokuwa mdogo...
Alinitesa sana katika mapenzi/ndoa....
Alinisababishia hasara kubwa kwenye biashara yangu...
Alisababisha kifo cha mtu muhimu sana kwangu....
Na sababu nyingine nyingi unazojipa kwamba kuweka kinyongo kwa mtu ni haki yako kabisa.
Lakini hebu niambie, kwa kuwa na kinyongo hiko kumekusaidia nini mpaka sasa? Je alichokufanyia mtu huyo kipindi hiko kimebadilika?
SOMA; SAMEHE…
Kukaa na kinyongo ni kuendelea kujitesa, kujinyima nafasi ya kufanya mambo ya msingi kwako na yatakayokupeleka kwenye mafanikio.
Na kinyongo hiko hakikusaidii wewe wala yule ambaye umemwekea.
TAMKO LA LEO;
Kuanzia leo nafuta vinyongo vyote ambavyo nimewawekea watu. Nimegundua vinyongo hivi haviniongezei chochote zaidi ya kunirudisha nyuma. Yeyote aliyenifanyia jambo baya sina muda wa kuendelea kumfikiria, nina maisha mengine mazuri ya kuishi na kufurahia. Sina nafasi ya vinyongo.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.