Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, May 29, 2015

#NENO_BUSARA; Tatizo La Vitu Ambavyo Ni Rahisi Kufanya.

Tatizo la vitu ambavyo ni rahisi kufanya ni kwamba ndio vitu ambavyo ni rahisi kutokufanya.
Ni rahisi sana kuwa na afya bora, kwa kula vyakula bora, mboga mboga na matunda. Lakini pia ni rahisi sana kutokula vyakula hivyo, kutokana na wingi wa vyakula visivyo vya afya.
Ni rahisi sana kufikia uhuru wa kifedha. Nunua kile unachohitaji kutumia tu, punguza matumizi yasiyo ya lazima na wekeza angalau sehemu ya 10 ya kipato chako. Lakini pia ni rahisi kutokufanya hivi, kwa sababu kuna vitu vizuri na vya kuvutia, ambavyo vinatamanisha kununua, japo sio muhimu kwako. Na hata kama huwezi kulipia unaweza kukopeshwa na hivyo kujikuta kwenye shimo refu la madeni na matatizo ya kifedha.
Ni rahisi sana kufanikiwa, chagua kile unapenda kufanya na weka moyo wako wote kwenye kukifanya. Lakini pia ni rahisi sana kutokufanikiwa, kwa sababu kuna vitu vingi vizuri vya kufanya na pia huna muda wa kutosha kuweka moyo wako wote kwenye kile unafanya. Na hapo bado watu hawajakukatisha tamaa kwa kukuambia huwezi au haiwezekani.
Vitu ambavyo ni rahisi kufanya ndio vitu ambavyo ni rahisi kutokufanya. Jua hili na uchukue hatua.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment