Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, May 2, 2015

Hii Ni Nafasi Ya Mwisho Kabisa, Usiikose Tena.

Kwanza niwashukuru sana wale wote ambao wameshajiunga na semina ya MAFANIKIO KATIKA BIASHARA  mwaka 2015. Umefanya maamuzi sahihi sana kujiunga na semina hii na utajifunza mambo mazuri ambayo kama utayatumia utaboresha zaidi biashara yako na kufikia mafanikio makubwa.

Nimepokea ujumbe kutoka kwa watu wengi jana kusumbuliwa na mtandao hivyo kushindwa kutuma malipo ya ada ya semina. Na jana hiyo ndio ilikuwa mwisho w akujiunga na semina hii ya kipekee ambayo mtu hawezi kuipata mahali pengine. Kutokana na changamoto hii ya kukamilisha ambayo wengi imewazuia kukamilisha malipo, nimeona ni busara kuongeza siku ya leo kufanya malipo.

Kama ulikwama kufanya malipo au kama ulikuwa bado hujaamua kujiunga unaweza kutumia siku ya leo jumamosi tarehe 02/05/2015 kukamilisha malipo yako na kujiunga. Nyongeza hii ya siku za kuijunga ni kwa leo tu hivyo itumie vizuri kama hutaki kupitwa na semina hii.

Kama ndio unapata ujumbe huu kw amara ya kwanza habari iko hivi; AMKA CONSULTANTS wamekuandalia semina ya biashara inayokwenda kwa jina MAFANIKIO KATIKA BIASHARA na semina hii inaendeshwa kwa njia ya email kwa kipindi cha mwezi mmoja. Katika mwezi huu ni kama unapata nafasi ya kuwasiliana na mimi moja kwa moja kila siku, kujifunza, kuuliza maswali na kupata majibu. Ada ya kujiunga na semina hii ni tsh elfu 30, na ili kujiunga tuma ada hiyo kwa namba 0717396253/0755953887 na kisha tuma ujumbe wenye jina lako na email kwenye moja ya namba hizi na utaunganishwa.

Hii ni semina ambayo hupaswi kuikosa labda kama umeamua kubaki pale ambapo upo kwa sasa.

Tumia siku hii ya leo kukamilisha malipo yako ili uweze kuingia kwenye semina hii. Uzoefu ambao nimekuwa nao kwenye maandalizi ya semina hizi ni kwamba watu wengi hutaka kujiunga pale ambapo semina inakuwa imeshaanza. Inakuwa ni changamoto sana kwa muundo tunaotumia kutoa mafunzo, mfumo huu unahitaji washiriki wawe wamepangwa vizuri kabla ya masomo kuanza kutolewa. Hivyo kama utashindwa kujiunga leo, hutaweza kujiunga tena hasa pale mafunzo yatakapoanza. Hivyo kama hukuona ujumbe huu na ntingine zilizopita ndio tayari umeshakosa mambo haya mazuri.

Karibu sana tujifunze ili kuweza kuwa bora zaidi na kufikia mafanikio makubwa.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment