Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, June 21, 2015

UKURASA WA 172; Tatizo La Kuweka Kinyongo...

Ni kwamba unakosa nafasi ya kufuatilia mambo mengine muhimu kwako.
Unaweza kujiaminisha kwamba kinyongo ulichomwekea mtu unastahili kabisa.
Alininyanyasa sana nilipokuwa mdogo...
Alinitesa sana katika mapenzi/ndoa....
Alinisababishia hasara kubwa kwenye biashara yangu...
Alisababisha kifo cha mtu muhimu sana kwangu....
Na sababu nyingine nyingi unazojipa kwamba kuweka kinyongo kwa mtu ni haki yako kabisa.
Lakini hebu niambie, kwa kuwa na kinyongo hiko kumekusaidia nini mpaka sasa? Je alichokufanyia mtu huyo kipindi hiko kimebadilika?
SOMA; SAMEHE…
Kukaa na kinyongo ni kuendelea kujitesa, kujinyima nafasi ya kufanya mambo ya msingi kwako na yatakayokupeleka kwenye mafanikio.
Na kinyongo hiko hakikusaidii wewe wala yule ambaye umemwekea.
TAMKO LA LEO;
Kuanzia leo nafuta vinyongo vyote ambavyo nimewawekea watu. Nimegundua vinyongo hivi haviniongezei chochote zaidi ya kunirudisha nyuma. Yeyote aliyenifanyia jambo baya sina muda wa kuendelea kumfikiria, nina maisha mengine mazuri ya kuishi na kufurahia. Sina nafasi ya vinyongo.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment