Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Friday, June 5, 2015

UKURASA WA 156; Kabla Hujalalamikia Changamoto Unayopitia, Tafadhali Sana Soma Hapa.



Kuna wakati ambapo mambo yanaweza kuwa magumu sana kwako. Huu ni wakati ambapo unakuwa umeweka malengo na mipango yako ila unashindwa kuyafikia. Unapanga kufanya kitu fulani ili baadae upate majibu mazuri lakini hiyo pia haitokei.
Wakati kama huu unaweza kujiona kama wewe una kisirani au huwezi kufikia kile unachotaka. Katika wakati huu unaweza kuona wengine mambo yao yako vizuri ila ni wewe tu ambaye mambo hayakwendi vizuri.
Leo nataka nikuambie kwamba haijalishi unapitia magumu kiasi gani, haupo peke yako. Kuna watu wengi sana wanaopitia magumu kama unayopitia wewe, lakini wanaendelea kuweka juhudi kwa sababu wanajua huo sio mwisho. Kuna watu wengi ambao wanakazana kuboresha maisha yao ila wanakutana na vikwazo vingi. Nao pia hawakati tamaa kwa sababu wanajua hakuna kinachoshindikana.

Naomba nikusihi sana usikate tamaa hata pale mambo yanapokwenda tofauti na ulivyotegemea. Tafuta watu unaowaamini na ongea nao, kuna machache wanaweza kukuambia na ukajiona kumbe sio wewe mwenyewe umepotea kwenye dunia hii. Jua kwamba hata waliofikia mafanikio makubwa na unatamani kuwa kama wao, hawakufika pale kirahisi, walivuka vikwazo vingi ndio wakafika hatua ile. Unahitaji kuvuka vikwazo hivi pia.
TAMKO LA LEO;
Pamoja na changamoto nyingi ninazopitia kwenye kazi, biashara na hata maisha yangu kwa ujumla, najua sipo peke yangu. Kuna watu wengi ambao wanapitia changamoto kama mimi ila hawakati tamaa, wanaendelea kuweka juhudi. Najua hata wale ninaotamani kufikia ngazi walizofikia walipitia nyakati ngumu pia. Nitaendelea kupambana na kamwe sitokata tamaa.
Tukutane kwenye ukurasa wa 157 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment