Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, June 3, 2015

UKURASA WA 154; Jinsi Ya Kuwinda Fedha Zako Mwenyewe Ili Kufikia Uhuru Wa Kifedha.


Kwenye makala ya siku mbili zilizopita tuliona kwamba kila mtu anawinda fedha zako wewe. Kila mtu anayejaribu kukushawishi ununue kitu, kila anayekushawishi utoe fedha yako anaiwinda fedha yako. Kuna watu wengi sana wanaokuzunguka ambao wanawinda fedha yako, hivyo usipokuwa makini utashangaa umefanya kazi miaka mingi ila huoni kikubwa ulichobadili kwenye maisha yako.

Kama hukusoma makala iliyopita isome hapa; Kila Mtu Anawinda Kitu Hiki Muhimu Ulichonacho, Kuwa Makini.


Leo nataka nikushirikishe njia nzuri itakayokuwezesha wewe kuwinda fedha zako mwenyewe. Njia hii itakuwezesha kuona faida ya kipato ambacho unapata kwenye maisha yako kutokana na kazi unazofanya.
Njia rahisi ya wewe kuwinda kipato chako ni kujilipa wewe kwanza kabla hujafanya malipo mengine yoyote. Katika fedha yoyote unayopata, hakikisha kuna kiasi fulani unaweka pembeni kabla hujaanza kufanya matumizi. Kiasi hiki unaweza kuanzia na asilimia kumi ya kipato chako.
Fedha yoyote unayoipata, iwe ni faida kwenye biashara, mshahara wa kazi, umeokota au hata umepewa, usikubali kuitumia yote. Igawe fedha hii kwenye mafungu kumi na chukua fungu moja weka pembeni. Kama ni shilingi elfu kumi, weka elfu moja pembeni, kama ni laki moja weka elfu kumi, kama ni milioni moja weka laki moja. Fedha hii unayoweka pembeni ndio fedha uliyojilipa wewe mwenyewe na hutakiwi kuitumia kwenye matumizi mengine yoyote.
Hii ni fedha yako ambayo utaiwekeza ili iweze kukuzalishia zaidi baadaye. Kama utaweza kufanya hivi bila kuchoka, baada ya muda utajikuta katika nafasi nzuri sana kifedha.
Jambo muhimu la kuzingatia ni kwamba kuwa wa kwanza kuwinda fedha zako. Kabla hujafanya jambo lolote kwa fedha yako, weka chako pembeni kwanza. Yaani usifanye matumizi halafu itakayobaki ndio iwe yako ya kuwekeza. Bali wekeza kwanza na itakayobaki ndio uipeleke kwenye matumizi.
TAMKO LA LEO;
Najua mimi ndio mtu wa kwanza kuwinda fedha zangu kama ninataka kufikia uhuru wa kifedha. Kuanzia sasa, fedha yoyote itakayopita kwenye mikono yangu, nitahakikisha asilimia 10 ya fedha hii inabaki kuwa yangu. Sitakubali tena kuwa mpitishaji tu wa fedha, nataka na mimi niwe sehemu ya fedha hizi. Nitakuwa mwindaji wa kwanza wa fedha zangu, kabla sijawaruhusu wengine kufanya hivyo.
Tukutane kwenye ukurasa wa 135 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment