Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, June 8, 2015

UKURASA WA 159; Njia Bora Ya Kuweza Kufanya Kitu Unachohofia Kufanya.



Hofu ni moja ya vitu ambavyo vinawazuia watu wengi kuweza kupiga hatua kwenye maisha yao. Hofu imewafanya watu wengi kushindwa kuzichangamkia fursa zinazowazunguka na hivyo kushindwa kufikia mafanikio kwenye maisha.
Moja ya hofu kubwa zinazowazuia wengi kupata maendeleo ni hofu ya kupoteza. Mtu akishakuwa na kitu, hufanya kila lililo ndani ya uwezo wake ili kulinda kitu hiko. Hakuna anayependa kupoteza kitu ambacho amekifanyia kazi kwa muda mrefu.
Lakini pia kuhofia kupoteza kitu ulichonacho maana yake utashindwa kuchukua hatua kwenye fursa mbalimbali zitakazojitokeza. Kama tunavyojua kwenye maisha, kitu chochote kizuri huwa kinakuja na hatari zake(risk). Hivyo ili upate faida ni lazima ufanye kitu ambacho kinaweza kuwa hatari kwako. Unakuwa na uwezekano mkubwa wa kupoteza kama ilivyo kwenye kupata.
Unapojikuta kwenye hali ya hofu kama hii, pia kiasi ambacho unaweza kupoteza na pia pima kile ambacho utakipata kama ukichukua hatua. Pia pima ni kitu gani unajifunza kama utachukua hatua na ukapoteza. Pia angalia njia nyingine unazoweza kutumia kupunguza hatari hiyo. Baada ya hapo chukua hatua mara moja.
Watu wengi watakuambia chukua risk, fanya na utajifunza, ila usiingie kichwa kichwa, hakikisha  hata kama utapoteza basi kuna somo utajifunza.

TAMKO LA LEO;
Najua hofu imekuwa inanizuia kufikia malengo yangu kwenye maisha. Hofu ya kupoteza imekuwa inanizuia mimi kuzichangamkia fursa zinazojitokeza. Kuanzia sasa nitakuwa nafanyia kazi fursa inayojitokeza kwa kuhakikisha hata kama ninapoteza kuna somo kubwa ninalojifunza.

Tukutane kwenye ukurasa wa 160 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment