Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, June 1, 2015

UKURASA WA 152; Kila Mtu Anawinda Kitu Hiki Muhimu Ulichonacho, Kuwa Makini.


Tunaishi dunia ambayo kila mtu kuna kitu anatafuta. Na kipimo kimoja ambacho kinapima kile ambacho kila mtu anataka ni fedha. Kama unataka kuwa na maisha yenye hadhi nzuri basi yatapimwa kwa kiwango cha fedha unachotengeneza au ulichonacho. Hivyo kwa kila wakati kila mmoja wetu anapambana kupata fedha. Tunafanya kazi na biashara zinazowasaidia wengine ila mwisho wa siku tunataka na sisi kupata fedha ambazo zitatusaidia kwatika mahitaji mengine muhimu.
Katika mchakato huu wa maisha wa kila mtu kutafuta fedha, imefika hatua sasa kila mtu anawinda fedha uliyonayo wewe. Kila mtu anakazana kukushawishi utoe fedha yako ili aipate yeye. Mtu anayeuza nguzo nzuri na kukushawishi kwamba huwezi kupata nyingine kama hizo anafanya yote hayo ili aipate fedha uliyonayo mfukoni. Mtu anayeandaa tamasha na kukuambia kwamba ni la kukata na shoka, hutakiwi kulikosa, anatumia mbinu zote hizo kuhakikisha wewe unatoa fedha yako na yeye anufaike kwa kiasi chake.
Jua kwamba kila mtu unayekutana naye katika mazingira ya kazi au biashara anatafuta jinsi ya kuipata fedha yako. Sio jambo baya kwa kuwa unapata huduma, ila pia kuna somo kubwa sana unatakiwa kujifunza hapa. Kama kila mtu anaiwinda fedha yako, je wewe ni juhudi gani unazofanya kuilinda isichukuliwe hovyo?
Huwezi tu kutoa fedha kwa sababu mtu amekushawishi ufanye hivyo, japo kuna wengi wanafanya hivi, unakutana na muuza nguo, hukuwa na mpango wa kununua nguo ila unajishangaa umenunua na unafika nyumbani nguo yenyewe hujaipenda. Ni lazima wewe uwe na ulinzi mkubwa kwenye fedha zako, la sivyo utajikuta unampatia kila mtu na wewe mwenyewe unabaki mikono mitupu.
Kuwa mlinzi imara wa fedha zako, hakikisha unatumia kwenye matumizi ambayo ni muhimu sana. Kesho nitakushirikisha njia nyingine muhimu ya kuzilinda fedha zako na pia kuhakikisha na wewe unaziwinda fedha zako mwenyewe. Mshirikishe watu wako wa karibu ujumbe huu kwa kuwatumia email, ni muhimu sana wewe kufanya hivi kwa sababu karibu kila mtu ana matatizo ya fedha, na matatizo yote ya fedha yanaanzia hapa kwenye uwindaji. Mshirikishe mtu na utakuwa umefanya jambo zuri sana.

TAMKO LA LEO;
Najua kila mtu anawinda fedha ambayo ipo kwenye mfuko wangu. Kila mtu anayenishawishi kununua kitu anawinda fedha zangu. Ni jukumu langu kuweka ulinzi kwenye fedha zangu ili na mimi niweze kunufaika nazo.

Tukutane kwenye ukurasa wa 153 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment