Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, June 6, 2015

UKURASA WA 157; Maisha Ya Kuzima Moto, Yajue Na Yaepuke



Watu wanaofanya kwenye idara ya zima moto kazi yao ni moja tu, kusubiri moto utokee na kwenda kuuzima. Kama hakuna moto, hawana kazi kubwa, ila moto unapotokea ndipo hufanya kila juhudi kuuzima.
Sasa kuna watu wengi kati yetu ambao wanaishi maisha ya zima moto. Watu hawa wanaweza kuwa na malengo na mipango mizuri ila wanashindwa kuitekeleza kwa sababu ya mtindo wa maisha waliochagua kuishi ambao ni wa kuzima moto. Watu hawa huhangaika kuzima kila moto ambao unajitokeza kwenye maisha yao.
Watu hawa huishi siku yao kutokana na kitu kilichotokea. Husumbuka na kila kitu kinachotokea hivyo kushindwa kufanyia kazi malengo waliyojiwekea. Na mara nyingi moto wanaozima hauhusiani kabisa na malengo yao hivyo kujikuta wakizidi kupoteza muda.
Kuna uwezekano mkubwa na wewe ni mmoja wa wanaoishi kwa kuzima moto. Ngoja nikupe sifa za wanaozima moto uone kama sio mmoja wao. Kama huwezi kutenga muda wa kufanya kuondokana na kelele nyingine zote wewe ni zima moto. Kama huwezi kukaa mbali na simu yako kwa muda ambao unahitaji kufanya kazi wewe ni zimamoto. Kama unajibu haraka kila ujumbe unaoingia kwenye simu yako, au kuperuzi mitandao ya kijamii ukifikiri kuna kitu kinakupita, wewe ni zimamoto.
Kama wewe umeingia kwenye kundi la zima moto, nina habari mbili kwako, moja nzuri na moja mbaya. Naanza na habari mbaya, hutaweza kufikia mafanikio kwenye maisha kwa kuwa zima moto. Na habari nzuri ni kwamba unaweza kubadili tabia hiyo ya zima moto. Ni wewe kujijengea nidhamu ya kuweza kusimamia mipango yako na kuachana na mambo yasiyokuwa muhimu kwako. Ni vigumu lakini inawezekana. Kama unahitaji msaada wa kuweza kuondokana na tabia ya zima moto tuwasiliane.

TAMKO LA LEO;
Najua kwa maisha ya kuzima moto ninayoenda nayo, sitaweza kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yangu. Naamua sasa kuishi kwa kufuata malengo na mipango yangu na sio kutafuta moto wa kuzima. Moto wangu ni malengo na mipango yangu, vingine vyote ni kelele tu.

Tukutane kwenye ukurasa wa 158 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment