Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, June 4, 2015

UKURASA WA 155; Hii Ndio Sababu Kubwa Inayokufanya Ushindwe Kutatua Matatizo Yako.



Tumewahi kujadili hapa kwamba matatizo uliyonayo umeyatengeneza wewe mwenyewe. Hii inatokea kwa sababu kwa kila tatizo ulilonalo, unapojaribu kulitatua unatengeneza tatizo jingine. Kila suluhisho linakuja na tatizo jipya kabisa. Hivyo unaweza kuchagua ni matatizo ya aina gani unafanya.
Kuna wakati mtu anaweza kuwa kwenye matatizo makubwa sana na akawa hajui afanye nini. Ila anapokuambia wewe kuhusu matatizo yake unaona suluhisho haraka sana na kushangaa kwa nini mtu huyu haoni suluhisho hilo rahisi. Hii yote inatokana na sababu moja kubwa ambayo inawafanya watu washindwe kutatua matatizo yao, japo suluhisho ni rahisi.

SOMA; Kila Mtu Anawinda Kitu Hiki Muhimu Ulichonacho, Kuwa Makini.


Sababu moja kubwa inayokufanya wewe ushindwe kutatua matatizo yako ni kutokukua zaidi ya matatizo yako. Kama tulivyoona hapo juu matatizo uliyonayo umeyatengeneza wewe mwenyewe. Na umeyatengeneza matatizo haya ukiwa na uwezo mzuri sana wa kufikiria. Hivyo kwa kuendelea kufikiria kama ulivyokuwa unafikiria wakati unatengeneza matatizo hayo huwezi kuyatatua kamwe. Unahitaji kuweza kufikiria zaidi ya ulivyokuwa ukifikiria wakati unaingia kwenye matatizo yako.
Unahitaji kuwa mbunifu zaidi ya ulivyokuwa wakati unatengeneza matatizo yako. Kwa kifupi kuwa vile ulivyokuwa wakati unaingia kwenye matatizo hakuwezi kukusaidia hata kidogo kutatua matatizo hayo. Unahitaji kuwa mtu tofauti na ulivyokuwa mwanzo, unahitaji kuweza kufikiri zaidi na kuwa mbunifu zaidi ya wakati unaingia kwenye matatizo hayo.
Unaweza kufikiria zaidi ya ulivyokuwa unafikiri wakati unaingia kwenye matatizo na unaweza kuwa mbunifu zaidi ya ulivyokuwa wakati unaingia kwenye matatizo kama utakuwa matu wa kujifunza kila siku kwa kujisomea na kutafakari. Pia unahitaji kuilazimisha akili yako kufikiri zaidi na kutengeneza majibu ya changamoto unazopitia.

TAMKO LA LEO;
Najua siwezi kutatua matatizo niliyonayo kama nitaendelea kufikiria kama nilivyokuwa nafikiria wakati naingia kwenye matatizo haya. Nahitaji kuwa na mabadiliko ya kifikra na kiutendaji ili kuweza kukabiliana na matatizo ninayokutana nayo. Nahitaji kuwa mbunifu zaidi ya nilivyokuwa wakati naingia kwenye matatizo haya.

Tukutane kwenye ukurasa wa 135 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment