Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, June 11, 2015

UKURASA WA 162; Hakuna Namna Nyingine...



Hakuna namna nyingine, ni lazima ufanikiwe.
Kuna watu ambao wameanzia chini kuliko ulikoanzia wewe lakini wameweza kufanikiwa, kwa nini na wewe usifanikiwe?
Kuna watu ambao wamepata elimu ndogo kuliko uliyopata wewe, lakini wameweza kufanya mambo makubwa kwenye maisha yako, kwa nini wewe ushindwe kufanya?
Kuna watu ambao walikataliwa na kutelekezwa. Lakini hawakujali hilo, waliendelea na kile kilichokuwa ndani yao na sasa wako mbali, kwa nini na wewe usiende mbali zaidi ya ulipofika sasa?
Siandiki haya kukulinganisha wewe na wengine, au kukufanya ujilaumu kwa nini ushindwe na waliokuwa chini zaidi yako.
Ila naandika haya kukumbia kwa hapo ulipofikia sasa hakuna namna nyingine bali ni kufanikiwa tu. Hakuna uchawi utakaokuletea mafanikio haya, hakuna serikali itakayokuletea mafanikio haya, hakuna ndugu atakayekuletea mafanikio haya.
Amka sasa na uanze kupigania kile kilicho chako, amka cha kulalamika, weka juhudi kwenye kazi yako, wenzako wakienda kupiga soga wewe fanya kazi, wenzako wakipitia viti virefu jioni wewe jiandae na kazi, kidogo kidogo na wewe utachomoza na utakuwa habari ya mjini.
Acha kuishia kusema fulani alianzia hapa kafika pale, ingia kwenye kazi na wewe uwe sehemu ya hadithi nzuri kwa wengine.

TAMKO LA LEO;
Leo hii nimeamua kwamba hakuna namna nyingine ila kufikia mafanikio kwenye maisha yangu. Najua uwezo ninao na hivyo naweka juhudi kutengeneza mafanikio makubwa.

Tukutane kwenye ukurasa wa 163 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment