Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, June 20, 2015

UKURASA WA 171; Unapokata Tamaa Maana Yake Umekubali Hivi.

Kukata tamaa maana yake umeamua kuondoka kwenye safari inayokupeleka kwenye mafanikio.
Kukata tamaa maana yake umeamua kwamba nguvu zote ulizoweka, mambo yote uliyojitoa mpaka sasa hayana maana na umeamua kuyapoteza.
Kukata tamaa maana yake ni kusema ulikuwa hujui kile ulichopanga kufanya na hata sasa hujui ni kitu gani unataka kufanya kwenye maisha yako.
Kukata tamaa maana yake unaiambia dunia kwamba wewe huwezi kujitoa mpaka hatua ya mwisho.
Utakutana na mambo magumu sana.
Utakutana na changamoto nyingi sana.
Safari hii sio rahisi, ila pia kukata tamaa hakutakuletea urahisi wowote, zaidi kutakufanya ujisikie vibaya kwa kushindwa kufanikisha chochote.
Kamwe kamwe usikate tamaa, endelea kuweka juhudi, endelea kuboresha pale unapokosea. Hivi ndivyo utakavyoweza kufikia mafanikio makubwa kwenye maisha yako.
TAMKO LA LEO;
Najua kukata tamaa ni kujidhalilisha kwenye maisha yangu. Najua kwamba safari hii sio rahisi, lakini pia kukata tamaa hakutarahisisha chochote. Nitaendelea kupambana mpaka nipate kile ninachotaka.
Tukutane kwenye ukurasa wa 172 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment