Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, December 7, 2014

Tulikuona Wakati Unakuja Mjini…

Tulikuona wakati unakuja mjini, usijione mjanja leo…

Ulikuja umevaa yeboyebo na nguo umebeba kwenye mfuko wa rambo, leo unajiona unajua sana…

Hayo ni maneno ya hovyo sana yanayotolewa na watu walioshindwa. Watu ambao wamepoteza muda wao kwa kufikiri wao ni wakongwe na anakuja mtu na kuwaacha wakishangaa.

Ili kujifariji kwamba na wao wana kitu fulani wanatumia sababu hiyo ya ukongwe.

joti-mpoki-enzi-hizo

Sikiliza mafanikio hayapimwi kwamba ulizaliwa wapi au umekulia wapi. Mafanikio yanapimwa na nini unachoweza kuonesha watu kwamba umefanya na kimeleta mabadiliko kwenye maisha ya wengine.

Kama wewe ndio unaambiwa wakuja usihofu, endelea kukazana.

Kama wewe ndio unawaambia wenzako ni wakuja soma hapa; ONDOKA NYUMBANI. Itakusaidia sana na utajua ni hatua gani ya kuchukua.

Chukua hatua sasa…

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment