Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, December 1, 2014

SIKU YA UKIMWI DUNIANI; Mambo Kumi Unayotakiwa Kujua Kuhusu Ukimwi.

Kila tarehe 01/12 ya kila mwaka dunia inaadhimisha siku ya UKIMWI. Siku hii imepewa heshma yake kutokana na madhara yake makubwa kwa watu wanaoupata.

Wakati tukiwa kwenye siku hii ya UKIMWI jiongeze na mambo haya kumi muhimu.

1. UKIMWI HAUUI.

UKIMWI maana yake ni upungufu wa kinga mwilini. Hivyo kinga yako inapopungua unatoa nafasi ya magonjwa mengine kukushambulia. Hivyo kinachowaua wagonjwa wa ukimwi sio ukimwi wenyewe bali magonjwa nyemelezi.

2. UKIMWI ni tofauti na VIRUSI VYA UKIMWI.

Ukiambukizwa virusi vya ukimwi leo, hauna ukimwi. Unawez akukaa na vizsi hivi kwa muda hata wa miaka kumi na pale kinga ya mwili inaposhindwa kukulinda na magonjwa ndio unakuwa na UKIMWI.

3. Wagonjwa watatu wa kwanza wa UKIMWI Tanzania waligunduliwa katika hospitali ya Ndolange mkoani Kagera mwezi November 1983.

4. UKIMWI husambazwa kwa kupitia maji maji ya mwilini. Yanayoongoza ni damu, na yenye kiasi kidogo ni mate, machozi na majimaji ya ukeni.

UKIMWI TZ

5. Njia kuwa ya kusambaza ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine ni kufanya mapenzi bila ya kujikinga. Njia nyingine ni kuchangia vitu vikali kama sindano na pia mama kwenda kwa mtoto.

6. Mpaka leo hakuna tiba wala kinga ya UKIMWI. Baadhi ya tafiti zimeonesha matokeo mazuri ila hakuna ambayo imedhibitishwa kutumiwa kama kinga au dawa.

7. Afrika chini ya jangwa la sahara ndio sehemu yenye maambukizi makubwa ya UKIMWI, asilimia 80 ya watu wenye ukimwi duniani wako Africa chini ya jangwa la sahara. Wakati idadi ya wanachi walioko Afrika chini ya jangwa la sahara ni asilimia 10 tu ya idadi ya watu wote duniani.

8. Wanawake wana hatari mara nane zaidi ya kuambukizwa ukimwi kuliko wanaume.

9. Mikoa inayoongoza kwa UKIMWI Tanzania ni Njombe ukifuatiwa na Iringa na mikoa yenye maambukizi madogo ni Pemba, Unguja na Lindi.

10. Mapambano ya UKIMWI yanaanza na mimi na wewe. Njia nyingine za maambukizi zimeweza kuzuiwa kwa kiasi kikubwa ila njia moja ndiyo yenye changamoto na njia hiyo ni kupitia kufanya mapenzi.

Tushirikiane kuutokomeza UKIMWI.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment