Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, December 6, 2014

Bado Hujachelewa...

Kuna bwana mmoja alikuwa analalamika ni jinsi gani alikuwa anapenda kujifunza kupiga kinanda ila akakosa muda kwenye maisha yake.
"Kwa nini usianze sasa" rafiki yake alimuuliza.
"Unashangaza wewe" yule bwana alimjibu. "Nina miaka hamsini sasa, nikianza kujifunza leo itanichukua miaka mitano mpaka nijue kupiga kinanda vizuri, wakati huo nitakuwa na miaka hamsini na tano" aliongeza bwana yule.
Rafiki yake alimsikiliza kwa makini kisha akamuuliza, " kama usipoanza kujifunza kinanda leo, miaka mitano ijayo utakuwa na miaka mingapi"?
Katika simulizi hii fupi unaweza kuona ni jinsi gani tunajijengea vikwazo visivyo na msingi sisi wenyewe.
Kama kuna jambo lolote unalotaka kufanya kwenye maisha yako bado hujachelewa kulifanya, ANZA SASA...
Nakutakia kila la kheri,
Kama unahitaji ushauri wa kina juu ya jambo lolote linalokusumbua andika email kwenda ushauri@kisimachamaarifa.co.tz
Karibu sana.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment