Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, December 14, 2014

Nenda Kapige Kura, Au Usipige Na Fanya Hivi…

Leo ni siku ya kupiga kura kuwachagua viongozi wa serikali za mitaa, najua unajua hili, ila imebidi niliandike tena ili tupate pa kuanzia. Kama ulikuwa hujui leo ndio siku ya uchaguzi basi tuna tatizo kubwa zaidi.

Kwa takwimu mbalimbali za chaguzi zilizopita tunaona idadi kubwa ya watu waliojiandikisha hawapigi kura. Na laiti kama watu hao wangepiga kura mabadiliko yangekuwa makubwa sana.

kupiga kura

Sasa sitaki kuandika mengi nikucheleweshe kupiga kura, ninachokuambia leo ni;

Nenda kapige kura, au usiende kupiga na usilalamike chochote.

Maana watanzania tumekuwa mafundi wa kulalamika ila hatua hatuchukui. Kama hatua kubwa za kuwawajibisha watu hatuwezi kuchukua, basi tuchukue hatua ya kupiga kura na kuchagua viongozi ambao ni bora.

Wahi kapige kura yako asubuhi hii, na mhamasishe kila unayekutana naye nae akapige kura.

Hapa ndipo mabadiliko ya nchi yetu yanapoanzia.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment