Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Thursday, July 9, 2015

UKURASA WA 190; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.

Mpaka sasa umeshajifunza mambo mengi sana kuhusu mbinu za kuboresha kazi yako, biashara yako na hata maisha yako kwa ujumla. Lakini mbona bado huchukui hatua yoyote ili kuweza kunufaika na yale ambayo unajifunza?
Mpaka sasa unajua kabisa ya kwamba kwa kufanya kile ambacho kila mtu anafanya utaendelea kupata matokeo ambayo kila mtu anayapata na ambayo sio mazuri sana. Lakini mbona unaendelea kufanya hivyo?
SOMA; Maisha Ni Mchezo Na Sheria Za Kuushinda.
Mpaka sasa unajua kabisa kulalamika au kulaumu wengine hakutakupatia wewe chochote unachotaka, sana sana kutakufanya ujione kama yatima ambaye hana msaada wowote. Lakini bado unaendelea kulalamika na kulaumu, kwa nini?
Kwa sababu huwezi!! Hili ndio jibu ambalo unajiridhisha nalo. Kwamba siwezi kufanya tofauti, kila mtu ameshazoea vile nilivyo. Kwamba siwezi kuweka muda zaidi kwenye kujifunza, kwa sababu nina mambo mengi ya kufanya. Kwamba siwezi kuacha kuangalia tv kila siku, nitapitwa na mambo mengi. Kwamba siwezi kuacha kukaa na jamaa zangu kila siku jioni tukipata moja moto na moja baridi ili nifuatilie zaidi biashara na kazi zangu.
Kama haya ndio majibu yako, kwanza wewe mwenyewe unayaamini kweli? Ni kweli kwamba huwezi kufanya mambo hayo ambayo yatabadili kabisa maisha yako? Vipi kama maisha yako ndio yangekuwa yanategemea hivyo ndio uweze kuishi. Kwa mfano unaambiwa kuchagua kuishi ila usiangalie tv au uangalie tv halafu unakufa, ungechagua nini?
Najua ungechagua kutokuangalia tv, safi sana, una maamuzi mazuri. Na ndio maana mimi siamini kwamba yale yote unayosema huwezi ni kwamba huwezi kweli, bali ni kwamba hutaki tu kufanya.
Kwa hiyo mambo yote unayosema kwamba huwezi, ukweli ni kwamba hutaki tu kufanya. Na kwa maana hii basi nakuomba kuanzia leo usiseme tena SIWEZI, sema SITAKI.
Siku nyingine kabla hujaniambia huwezi hakikisha kwamba ukifanya kitu hiko unakufa, vinginevyo ni sitaki.
TAMKO LA LEO;
Najua hakuna kitu kizuri na cha kubadili maisha yangu ambacho siwezi kufanya. Vingi ninavyoona siwezi kufanya ni kwamba sitaki tu kufanya. Kwa sababu kama maisha yangu yangekuwa yanategemea vitu hivyo ni lazima ningefanya. Hakuna kinachonishinda kufanya, na kuanzia sasa nitaacha kutumia sababu hii kwamba siwezi.
Tukutane kwenye ukurasa wa 191 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, July 8, 2015

UKURASA WA 189; Matatizo Yote Ya Mahusiano Yanaanzia Hapa... Sehemu Ya Pili(2)

Jana nilikushirikisha sababu kubwa ya matatizo kwenye mahusiano yetu sisi na watu wengine. Na kama ukiweza kuondokana na chanzo kile basi utapunguza sehemu kubwa sana ya matatizo kwenye mahusiano yako iwe ya kikazi, kibiashara, kindugu au kimapenzi. Kama hukupata nafasi ya kusoma kile tulichojadili jana basi kisome hapa; Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.
Leo nataka tugusie kitu kingine kikubwa sana kinacholeta matatizo kwenye mahusiano yetu. Najua eneo la mahusiano ndio eneo gumu sana kuelewana na watu kwa sababu moja kubwa, inapokuja swala la mahusiano watu hawatumii akili kufikiri, bali wanatumia hisia kufikiri. Na pale hisia zinapojiongoza zenyewe bila akili basi hapo ni majanga. Ndio maana ni vigumu sana kuweza kumweleza mtu kuhusu mahusiano hasa ya mapenzi akakuelewa.
Sasa sababu nyingine kubwa ambayo inasababisha matatizo kwenye mahusiano ni watu kuvaa visanamu mwanzoni mwa mahusiano. Watu wanapokutana ili kujenga uhusiano, wengi wanadanganya, wanasema vitu ambavyo vitawafanya wakubalike au kupendwa na wale wanaotaka kuwa na mahusiano nao. Hii ni kwenye mahusiano yote, iwe ya kazi, biashara au hata mahusiano mengine ya karibu.
SOMA; Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako Yote.
Mtu anadanganya kwenye usaili wa kazi ili aonekane ni bora na kupewa kazi. Labda hudanganyi vitu vikubwa, ni vitu vidogo vidogo tu kama kuahidi vitu ambavyo unajua kabisa huwezi kufanya kwa muda mrefu.
Au kwenye biashara unamdanganya mteja kwamba unaweza kufanya kitu fulani ili akubali kufanya biashara na wewe.
Kwenye mapenzi sasa, ndio mtu atadanganya vitu vingi sana, atabadili mpaka mfumo wa maisha, kuacha baadhi ya vitu na kadhalika.
Mambo yangekuwa rahisi sana kama kila mtu angeweza kuishi na hiki alichoahidi anaweza kufanya. Lakini kama tulivyoona jana, watu hawabadiliki, tena kwa haraka hivyo.
Kwa hiyo mtu atafanya kile alichosema kwa muda mfupi baada ya hapo anachoka na hivyo kurudia maisha yake ya zamani. Hapa ndio utasikia siku hizi fulani kabadilika. Hapana hajabadilika, amechoka kuvaa kile kisanamu na sasa ameanza kuonesha ukweli wake.
Kuwa makini usivae kisanamu wakati unataka kujenga mahusiano ambayo yatadumu. Kuwa mkweli, kama mtu hawezi kukukubali kwa ukweli wako hata ukimdanganya huo uhusiano hautadumu. Nasisitiza tena hii sio kwa mapenzi tu, bali kwenye mahusiano ya kazi, biashara na hata maisha ya kawaida. Kuwa mkweli na utawavutia wale wa kweli. Vaa kisanamu na utavutia visanamu vingine.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba kudanganya mwanzoni mwa mahusiano ni kujenga kifo cha mahusiano hayo. Hakuna uongo unaoweza kudumu kwa muda mrefu. Nitakuwa mkweli siku zote ili niweze kujenga mahusiano bora na yatakayoniletea mafanikio. Hata kama kuwa kwangu mkweli kutanikosesha baadhi ya mahusiano, najua kutanijengea mahusiano ambayo ni bora.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tuesday, July 7, 2015

UKURASA WA 188; Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.

Kama kuna kazi ngumu hapa duniani basi ni kuishi. Ndio maisha ni mazuri na ndio maisha ni matamu ila ni kazi kubwa sana kuweza kuyaishi.
Ni kazi kubwa kuyaishi kwa sababu huwezi kuishi maisha ya peke yako. Umezungukwa na watu wengi na watu hawa wana tabia tofauti tofauti. Watu wote hawafanani tabia.
Kuna wakati unafikiri kama watu wote wangekuwa kama fulani basi mambo yangekuwa mazuri sana. Saa nyingine unafikiria kama wateja wote wangekuwa kama mteja fulani basi biashara ingekuwa nzuri sana. Au wakati mwingine unafikiria kama bosi wako angekuwa na roho ya tofauti na aliyonayo sasa basi maisha yako ya kazi yangekuwa mazuri sana.
Lakini ukweli ndio huo kwamba watu hatufanani na pamoja na tofauti zote hizo bado unahitaji kushirikiana na watu wote hao.
SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.
Matatizo yote ya kwenye mahusiano, yawe ya kindugu, ya kibiashara, ya kikazi au hata ya kimapenzi yanaanzia pale mtu mmoja anapotaka kumbadilisha mwingine. Yaani ikishafikia hatua hii kwamba mtu mmoja anataka mwingine abadilike, ndio matatizo makubwa sana yanaibuka.
Unajua ni kwa nini? Kwa sababu mwanadamu atafanya kitu chochote kile kinachowezekana ili mradi tu asibadilike. Watu hawapendi kubadilishwa na wanapenda kuendelea kuwa vile walivyo. Tena kama ndio mtu mzima, ndio basi kabisa, atahakikisha anakataa kubadilika hata kama kufanya hivyo kunagharimu maisha yake.
Wakubali watu vile walivyo, au kama huwezi kuwakubali walivyo achana nao. Kama wataona wewe ni wa muhimu sana na hawawezi kukupoteza basi watabadilika wao wenyewe. Na mtu anapoamua yeye mwenyewe kubadilika inakuwa rahisi kwake kubadilika hata kwa kiasi kidogo. Ila kama wewe ndio unamlazimisha mtu abadilike, okoa nguvu zako.
TAMKO LA LEO;
Najua matatizo makubwa kwenye mahusiano ya watu huwa yana anza pale watu wanapojaribu kuwabadilisha wengine. Najua ya kwamba binadamu hawapendi kubadilishwa. Sitapoteza nguvu zangu kutaka kumbadilisha mtu. Nitamkubali mtu kama alivyo na kama siwezi nitaachana naye iwe ni mteja, bosi, ndugu au mwingine wa karibu. Muda wangu ni wa thamani sana siwezi kuupoteza kwa kufanya kazi ambayo haileti matunda.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Monday, July 6, 2015

UKURASA WA 187; Usikubali jua lizame leo kabla hujafanya kitu hiki muhimu.

Siku ya leo kuna watu wengi sana watakaokuudhi. Kuna watu wengi watakukasirisha na wengine watakufanya ujisikie vibaya sana. Kwa hasira inayotokana na watu hawa unaweza kufanya maamuzi ambayo sio mazuri sana kwao na kwako pia.
Ila kumbuka mara nyingi unapokuwa na hasira huwezi kufanya maamuzi ambayo ni sahihi. Na hata kama mtu atakuchukiza kiasi gani, hata kama atakuudhi kiasi gani kwa wewe kuwa na hasira, kwa wewe kuendelea kuwa na kinyongo naye haimuumizi yeye bali inakuumiza wewe mwenyewe.
SOMA; JICHO KWA JICHO; Tutabaki Na Dunia Ya Vipofu.
Sasa leo nataka nikupe kitu kimoja muhimu cha kufanya kabla jua halijazama. Hakikisha jua linapozama umemalizana na kitu hiki ili siku yako ya kesho iwe bora sana.
Kabla jua halijazama leo hakikisha umewasamehe wote waliokukosea leo. hakikisha umeondokana na vinyongo vyote ambavyo unaweza kuwa umejitengenezea kwa siku ya leo. Acha mambo haya yote yazame na jua la leo, ili jua linapochomoza kesho uanze siku yako ukiwa vizuri na uweze kufanya makubwa.
Usikubali jua lizame ukiwa bado na hasira au kinyongo. Vitu hivi havikusaidii chochote zaidi ya kufanya maisha yako kuwa magumu na hata kuharibu afya yako.
TAMKO LA LEO;
Sitakubali siku ya leo na siku nyingine yoyote ipite nikiwa na kinyongo au hasira kwenye moyo wangu. Jua litakapozama nitahakikisha nimeachia yote niliyokumbana nayo siku ya leo. kama kuna mtu ameniudhi, amenikasirisha au amefanya chochote ambacho kimenifanya niwe na kinyongo nitamsamehe. Maisha yangu ni muhimu zaidi ya chuki ninazotaka kutengeneza na watu.
Tukutane kwenye ukurasa wa 188 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Sunday, July 5, 2015

UKURASA WA 186; Kama Utashindwa Kufanya Chochote Utakachojifunza, Basi Fanya Hiki Kimoja Tu, Na Maisha Yako Yatagusa Wengine.

Nimekuwa nakushirikisha mambo mengi sana ambayo unahitaji kuyafanya ili kuboresha maisha yako. Mambo haya yanahitaji wewe ubadilike, uanze kufanya tofauti na ulivyozoea kufanya na sio kitu rahisi sana.
Kuacha kuangalia tv na kujisomea mambo yatakayokuweka mbele zaidiinahitaji kujitoa kweli.
Kuacha kukaa na jamaa zako kila jioni mkipata moja moto na moja baridi ili upate muda mwingi zaidi wa kuweka kwenye kazi au biashara yako sio kitu rahisi.
Kuacha kulalamika pale unapoona kabisa kwamba umeonewa au umeumizwa inahitaji nguvu ya ziada.
Kuacha usingizi na kuamka asubuhi na mapema sana ili uweze kujifunza na kuipangilia siku yako sio kitu rahisi kama unavyoweza kufikiria.
Tuseme labda wewe umeona kwamba mambo haya yote huwezi, kwa sababu tu una uvivu uliopitiliza au kwa kifupi basi tu hutaki kujihangaisha. Leo nataka nikuambie kitu kimoja muhimu sana cha kufanya.
SOMA; Kauli KUMI Za Marcus Aurelius Zitakazokufanya Uyaone Maisha Kwa Utofauti.
Tafadhali sana hata kama una uvivu kiasi gani, jitahidi ufanye kitu hiki kimoja na maisha yako yatagusa wengine kwa kiasi kikubwa sana.
Kitu chenyewe ni kuishi maisha mazuri kwako na kwa wanaokuzunguka. Kuwa mtu mwema, usimwibie mtu, usisengenye mtu, usijihusishe na majungu. Saidia wengine kadiri ya uwezo wako. Yaani kuwa tu mtu mwema na wengine waone wewe ni mfano wa kuigwa. Na hata kama kuna mtu amekosa tumaini kwa kuyaona maisha yako atapata tumaini kwamba dunia bado ina watu wema waliomo.
Hili ni jambo muhimu kwetu sote kufanya hata kama unafanya hayo mengine yote unayojifunza kila siku.
TAMKO LA LEO;
Nitahakikisha naishi maisha ambayo yatakuwa mfano mzuri kwa watu wengine. Nitajiepusha na mambo ambayo sio mazuri kwangu na kwa wale wanaonizunguka. Sitoiba wala kumdhulumu mtu, sitosengenya wala kushiriki majungu na nitasaidia wengine kadiri ya uwezo wangu.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Saturday, July 4, 2015

ONGEA NA KOCHA; Epuka Vipimo Hivi Viwili Ambavyo Jamii Inakupima Navyo.

#ONGEA_NA_KOCHA
Kwa miaka mingi dunia imekuwa inatupima kwa mambo haya mawili makuu...
Wanawake wamekuwa wakipimwa kwa kuonekano wao. Ni mzuri au sio mzuri?
Wanaume wamekuwa wakipimwa kwa umiliki wao. Je ana hela au hana hela, ana mali au hana mali?
Jamii nzima tumekuwa tukifanya hivi japo kwa unafiki tunaweza kukataa.
Vipimo hivi vimekuwa vinawazuia watu wengi kushindwa kufikia mafanikio kwa sababu tu wanatengwa na vipimo hivi.
Kama jamii inasema mwanamke mzuri ndio anaweza kuwa na maisha mazuri, kuna makabila mwanamke mweupe mahari yake ni kubwa kuliko mweusi, yule ambaye anakosa sifa hii atajiona hawezi kuwa na maisha mazuri.
Kama jamii inasema mwanaume mwenye hela ndio wa maana, kwenye jamii zetu wanaosikilizwa ni wenye hela hata kama hawana mawazo mazuri, ambaye anakosa sifa hii atajiona yeye sio wa maana na hivyo kujiondoa kabisa kwenye njia ya mafanikio.
Sasa mimi kama kocha wako nakutangazia rasmi kwamba achana kabisa na vipimo hivi vya hovyo.
Wewe ni zaidi ya vipimo hivi vilivyowekwa na jamii. Haijalishi una uzuri au ubaya, wewe ni bora sana. Haijalishi una fedha au huna fedha wewe ni mtu wa kipekee.
Endelea kuweka juhudi kwenye kile unachofanya na usikubali jamii ikuyumbishe na vipimo vyao visivyo na maana.
Wewe ni wewe, ni wa kipekee, ni bora na una mengi yaliyo mbele yako. Yaendee.
Makirita Amani,
www.amkamtanzania.com

UKURASA WA 185; Bila Kuwajua Watu Hawa Watatu Na Kumalizana Nao, Sahau Kuhusu Mafanikio.

Kuna watu watatu ambao kwa wewe kujua au kutokujua wamekuwa wanakuzuia kufikia mafanikio.
Sio kwamba wao wanakuja na kukuzuia wewe kufikia mafanikio, ila kwa sababu yao wewe mwenyewe umeshindwa kufikia mafanikio kwenye maisha yako.
Aina ya kwanza ya watu hawa ni watu ambao unataka kuwalinda. Kuna watu ambao wewe unataka kuwalinda na hivyo unajizuia kufikia mafanikio ili uendelee kuwalinda. Kuna baadhi ya watu wanaogopa kufikia mafanikio kwa sababu wanataka kuendelea kuwa na watu wanaowazunguka. Kuna wafanyakazi ambao wanaogopa kuonesha ubora wao kwenye kazi zao kwa sababu wanaogopwa kuchukiwa na wenzao au kuonekana ni hatari kwa mabosi zao.
SOMA; Wajue Watu Hawa na Waepuke Kwenye Maisha Yako.
Aina ya pili ni watu ambao unajaribu kuwaadhibu. Kuna watu ambao unaweza kuwa unataka kuwaadhibu na hivyo ukajizuia wewe kufikia mafanikio. Labda wazazi wako hawakukupatia kile ulichofikiri kingekuwa bora kwako. Na hivyo unataka uwaoneshe kwamba walikosea na hivyo wewe huwezi kufikia mafanikio kama ya wengine.... kwa sababu ya kutojali kwao.
Aina ya tatu ni watu ambao unataka kuwafurahisha. Hawa ni watu ambao unataka kuwafurahisha ili waendelee kukuona kama wanavyopenda kukuona na hivyo kujizuia kufikia mafanikio. Kuna watu ambao wanalazimika kuvaa mavazi ya bei ghali, kuendesha magari ya bei ghali na hata kuishi maeneo fulani ili tu waonekane.
Wajue watu hawa watatu kwenye maisha yako na malizana nao, hakikisha unaishi maisha uliyochagua wewe mwenyewe, yatakayokufikisha kwenye mafanikio unayotaka na sio kuwalinda watu, kuwaadhibu au kuwafurahisha.
TAMKO LA LEO;
Nimeamua sasa kwamba sitaki tena kuwalinda watu, kuwaadhibu au kuwafurahisha. Nahitaji kuishi maisha ambayo yatanipa furaha na kunifikisha kwenye mafanikio na sio maisha ambayo yatanirudisha nyuma. Nitaweka juhudi na maarifa ili niweze kuwa bora zaidi ya nilivyo sasa.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Friday, July 3, 2015

UKURASA WA 184; Ni Ruhusa Kwako Kubadili Mawazo.

Kwa mfano umeshakubaliana na mtu mtafanya kitu fulani halafu dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo, sitafanya tena kama nilivyokuambia. Unajisikiaje? Unachukuliaje hali kama hiyo?
Labda ni biashara na umeshakubaliana na mteja ila baadae anakuambia nimebadili mawazo. Au ni kwenye ajira na umeshakubaliana kitu fulani na mwajiri wako, umeshajiandaa kabisa na anakuambia nimebadili mawazo, hutafanya tena hivyo. Au ni kwenye maisha yako ya kawaida, ulipanga muoane na mtu na dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo? Au umeshaona na mtu na kati kati ya safari anakuambia nimebadili mawazo?
Najua kama wewe ndio umeambiwa hivi unaweza kujisikia vibaya sana. Unaweza kuona aliyebadili mawazo hafai na ameharibu maisha yako. Lakini ukweli ni kwamba yeye ametumia haki yake ya msingi, kuruhusu mawazo yake yamchagulie kile ambacho anaona ni bora kwake. Hakuna jinsi unaweza kuzuia hilo.
SOMA; Kabla Hujakubali Kila Unachoambiwa, Kumbuka Jambo Hili Moja Muhimu Sana.
Badala ya wewe kulalamika kwamba kwa nini hakukwambia mapema au kwa nini alikubali mwanzoni, furahi kwamba umejua mapema kabla hata hujapoteza muda mwingi. Shukuru kwamba umejua ni mtu wa aina gani na jifunze wakati mwingine kuangalia vitu muhimu kabla hujaingia kwenye makubaliano na mtu ambayo ni muhimu.
Jipe ruhusa ya kubadili mawazo, wape wengine ruhusa ya kubadili mawazo na usitake kuishi maisha ya kufungwa au kuwafunga wengine kwa sababu tu wanaogopa kubadili mawazo. Maisha yanapaswa kufurahiwa na sio kuishi kwa ajili ya kuwaridhisha wengine.
TAMKO LA LEO;
Najua nina ruhusa ya kubadili mawazo hata kama nilishakubaliana na mtu. Najua pia kwamba watu wana ruhusa ya kubadili mawazo yao hata kama walishaniahidi kitu. Naheshimu uhuru wangu na wa kila mtu na ni kwa uhuru huu ndio naweza kuishi maisha ninayoyafurahia na yenye faida kwa wengine pia.
Tukutane kwenye ukurasa wa 185 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Thursday, July 2, 2015

UKURASA WA 183; Hakuna Anayekuchukia Wewe, Bali Wanahamisha Chuki Zao Kutoka Hapa.

Leo naomba tujadili kidogo kuhusu mtu kumchukia mwingine.
Labda tuseme wewe kuna mtu anakuchukia, na amekuwa akikuonesha wazi wazi kwamba anakuchukia. Na hapa wewe huna tatizo lolote na mtu huyu. Unajaribu kuishi maisha yako bila hata ya kuingilia maslahi yao wala kuwavurugia chochote ambacho ni chao, lakini mtu anachagua tu kukuchukia.
Unajisikiaje katika hali kama hii? Unaumia kwa sababu ulitegemewa mtu ambaye ni wa karibu kwako awe pamoja na wewe badala yake anakuchukia? Unajaribu kumbadili mtu labda akupende?
Leo nataka nikupe sababu kwa nini mtu anaweza kukuchukia na njia bora ya kuondokana na chuki hiyo.
Kwanza kabisa mtu anapokuchukia sio kwamba anakuchukia wewe, ila anajichukia yeye binafsi. Ni hivyo tu. Mtu kuna kitu ambacho kinamsumbua kwenye maisha yake na hataki kukikubali, hivyo anayachukia maisha yake, kwa sababu hataki kukubali hilo pia anatafuta mtu wa kumchukia ili angalau aone tatizo sio lake. Si unajua tabia za wakwepa majukumu?
Hivyo atajipa kila sababu kwa nini anakuchukia wewe, lakini wewe huna tatizo lolote na yeye kukuchukia, hakuna chochote ambacho umemharibia. Labda umeamua tu kubadili maisha yako na kwa kuwa huyo anayekuchukia hawezi kubadilika basi anakuchukia. Kwa mfano ulikuwa na marafiki wa karibu kila siku mnakunywa pamoja, wewe ukakaa chini na kuona kunywa kwenu hakuna faida yoyote, hivyo ukaamua kuacha utaratibu huu wa kukutana baa kila siku na ukaanza kujifunza na kujishughulisha na vitu vya pembeni(fanya hivi kama bado una utaratibu wa kuhudhuria vikao vya baa kila siku). Unafikiri ni nini kitatokea kwa marafiki zako hao? Watakuchukia. Sasa hebu jiulize wanakuchukia kwa sababu wewe umeamua kuacha kukaa vikao hivyo kila siku? Hapana, wanakuchukia kwa sababu wewe unaanza kuwa bora kuliko wao. Kwa mfano ingetokea huna tena kazi na hivyo huna fedha ya kwenda baa kila siku unafikiri wangekuchukia? Hawawezi kukuchukia, watakuonea huruma tu na wataendelea na utaratibu wao.
Hivyo kama kuna mtu yeyote ambaye anakuchukia, wala usijiumize kichwa ufanye nini ili aache kukuchukia, endelea kufanya unachofanya na mwache ajiue mwenyewe na chuki zake. Maisha ni mafupi sana mpaka uanze kupata muda wa kumfurahisha kila mtu.
Usikubali uhusiano wowote wa kindugu au kirafiki uwe kikwazo kwako kuishi maisha unayotaka kuishi wewe, kama huvunji sheria. Hata kama kuna atakayekuchukia hawezi kukuchukia zaidi ya miaka 100 ijayo, kwa sababu wote mtakuwa mmekufa na hakuna atakayekuja kukukumbusha kwamba nilikuchukia sana duniani, kama mtakutana peponi.
SOMA; Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..
Maisha ni yako chaguo ni lako, kama kuna mtu anakuchukia muonee huruma na achana naye, wala hata usimfikirie, wewe endelea kuweka juhudi kwenye kile unachofanya na unachotaka kuwa bora.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba mtu yeyote anayenichukia sio kwa sababu ananichukia kweli, ila ni kwa sababu anajichukia yeye mwenyewe. Mimi sina muda wa kuanza kufikiria kuhusu anayenichukia, ni bora nikatumia muda huo vizuri kujiendeleza kuwa bora zaidi kwenye hiki ninachofanya.
Tukutane kwenye ukurasa wa 184 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, July 1, 2015

UKURASA WA 182; Urahisi Wa Kutengeneza Tabia Mbaya Na Ugumu Wa Kuishi Nazo.

Kuna jambo moja muhimu sana kwenye maisha ambalo unatakiwa kuwa unalijua. Na sio kulijua tu bali kulifanyia kazi kila siku maana kwa jambo hili moja ndio watu wanafanikiwa au wanashindwa.
Jambo hilo ni kwmaba, tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza ila ni ngumu sana kuishi nazo. Na kwa upande wa pili, tabia nzuri ni ngumu sana kutengeneza ila ni rahisi sana kuishi nazo. Hivyo ni wewe kuchagua kuwa tayari kufanya kipi ili uweze kuishije baadae.
Urahisi wa kutengeneza tabia mbaya.
Tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza, kwa mfano ulevi, ni rahisi sana kuwa mlevi, anza kunywa pombe kila siku na kunywa nyingi uwezavyo, hata hivyo unasikia raha, hivyo ni rahisi kutengeneza. Ila sasa maisha ya ulevi ni magumu sana, ni vigumu sana kuweza kufurahia maisha kama tayari wewe ni mlevi, utajikuta maisha yako yametawaliwa na ulevi na unajiona kama huwezi kutoka tena huko.
Tabia zote mbaya, iwe ni uvivu, wizi, uongo, kula hovyo zote ni rahisi sana kutekeleza. Ila kuishi nazo baada ya kuwa zimejijenga ni vigumu sana.
SOMA; Kama Unataka Kumaliza Matatizo Yako Ya Fedha Fanya Kitu Hiki Kimoja.
Ugumu wa kutengeneza tabia nzuri.
Kwa upande wa pili, tabia nzuri ni vigumu sana kuzitengeneza lakini ukishakuwa nazo ni rahisi sana kuishi nazo. Kwa mfano tabia ya kujiwekea akiba, ni vigumu sana mwanzoni, inabidi ujinyime inabidi uonekane huendi na wakati na wakati mwingine utahitaji kuzishinda tamaa zako. Ila unapokuwa na tabia hii ni rahisi na vizuri sana kuishi nayo kwa sababu unajua kuna akiba ambayo inaendelea kukua na hivyo kuvutiwa kuweka zaidi.
Unahitaji nguvu ya ziada ili kuweza kufikia mafanikio, ingekuwa rahisi kila mtu angekuwa nayo. Sio rahisi na ndio maana kuna wakati utaona kama unajitesa, endelea hivyo hivyo na mambo yatakuwa mazuri sana.
TAMKO LA LEO;
Najua nina machanguo mawili, nipate raha ya muda mfupi sasa halafu niteseke kwa muda mrefu au nipate shida ya muda mfupi sasa na kuishi kwa raha muda mrefu. Mimi nimechagua kuteseka kwa muda mfupi sasa ili niishi kwa raha muda mrefu ujao. Nitatengeneza tabia ambazo ni nzuri kwa sasa, ambazo ni ngumu kutengeneza lakini najua baadae nitafurahia kuishi nazo.
Tukutane kwenye ukurasa wa 183 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.