Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, April 26, 2015

UKURASA WA116; Usiwasikilize Watu Hawa.

Kuna watu kazi yao ni kupinga tu. Yaani watu wa aina hii hakuna kitu unaweza kufanya waache kupinga au kukosoa. Na hata utaka[ojaribu kujitetea watayapinga maelezo yako pia.

Ni muhimu sana kuwajua watu hawa na kutowapa nafasi kubw akwenye akili yako. Usiogope kuendelea na mipango yako kwa sababu tu mtu amekwambia huwezi, haiwezekani, unapoteza muda.

SOMA; Huu Ndio Uwekezaji Bora Zaidi Unaoweza Kuufanya.

Elewa kwamba wengi wanaokuambia hivi ndio kitu wanachopenda kufanya. Na ukiwachunguza kwa undani utagundua kwamba hakuna kitu chochote kikubwa wamefanya kwenye maisha yao.

Mara nyingi watu hawa wanakuwa hawajiamini wao wenyewe na hivyo hawaamini kama mtu mwingine anaweza kufanya mambo makubwa. Hawa sio watu unaotakiwa kuwasikiliza hata kidogo. Na angalau wangekuwa wanatoa njia mbadala basi ingejua wanajua kile wanachosema. Badala yake wanakukosoa tu halafu hawakupi njia nyingine nzuri.

SOMA; Mambo 20 Niliyojifunza Kwenye Kitabu The One Thing.

TAMKO LA LEO;

Najua kuna watu ambao kazi yao kubwa ni kukosoa na kupinga. Watu hawa hawajiamini wao wenyewe na hivyi hawaamini mtu mwingine anaweza kufanya mambo makubwa. Sitawaweka kwenye mawazo yangu watu hawa wala yale wanayosema.

Tukutane kwenye ukurasa wa 117 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment