Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, April 29, 2015

UKURASA WA 119; Njia Ya Uhakika Ya Kuondokana Na Hofu.

Hebu jiulize kama isingekuwa hofu leo hii ungekuwa wapi? Fikiria mipango yote ambayo umewahi kuwa nayo kwa muda mrefu lakini ilipofika utekelezaji tu, hofu ikabisha hodi na ikakufanya usidhubutu hata kuanza.

Kumbuka jinsi ambavyo umekuwa unahofia kushindwa, umekuwa unahofia kukataliwa, umekuwa unahofia kwamba utapata hasara kubwa. Umeacha kufanya kile ulichopanga kufanya. Lakini je hofu imetosheka? Jibu ni hapana, inaendele akukufuata popote unapokwenda na kwenye jambo lolote unalotaka kufanya.

SOMA; Ukweli Kuhusu Afya ya Wanaume; Kwa nini Wanaume Wanakufa Wadogo Kuliko Wanawake.

Kama unataka kufikia mafanikio makubwa, huna budi kufanya maamuzi magumu na maamuzi hayo ni kuondokana kabisa na hofu ambazo zinakuzuia wewekuchukua hatua kwenye maisha yako. Sasa unawezaje kuondokana na hofu hizi? Leo nitakushirikisha mbinu moja rahisi sana ya kuweza kufanya hivyo.

Njia rahisi na ya uhakika kabisa ya kuondokana na hofu ni kutengeneza tabia ya kufanya lile jambo ambalo unahofia kufanya. Tuseme labda umekuwa unatamani sana kuandika, ila unaogopa kuandika. Sasa fanya kuandika iwe ndio tabia yako unayofanya kila siku. Anza leo kwa kuandika sentensi moja, kesho mbili, keshokutwa aya na endelea hivyo hivyo. Hakikisha hukosi siku hujafanya hivyo. Na sio lazima kile unachoandika umuoneshe mtu.

SOMA; Hizi Ndio Siri 21 Za Mafanikio

Kama unahofia kuongea mbele ya watu, anza kujenga tabia ya kuongea na kila mtu ambaye unakutana naye, ongea na vikundi vidogo vidogo vya watu na nenda hatua ya juu zaidi mpaka utakapofikia kuongea na kundi kubwa kabisa la watu.

Kama unahofia kuanza biashara, anza kidogo, kwa kitu ambacho unajua huwezi kupata hasara na hata ukiipata haitokuumiza, endelea kuongeza kidogo kidogo kila siku, mpaka siku moja unajikuta unamiliki biashara kubwa sana.

Tabia ni dawa ya uhakika ya kumaliza hofu. Usiendelee kuhofia tena, anza kufanya kile ambacho unahofia kufanya na hofu haitakuw ana budi bali kukimbia na kukuachia wewe uhuru wa kufanya kile ulichochagua kufanya.

SOMA; Kitu Hiki Kimoja Ni Muhimu Kuliko Kiwango Cha Fedha Unachotaka.

TAMKO LA LEO;

Najua dawa ya hofu ni kufanya kile ambacho nahofia kufanya. Kuanzia sasa nitakuwa nafanya kile ambacho nahofia kukifanya, nitaanz akufanya kidogo kidogo na mwishowe nitakuwa nimepiga hatua kubwa sana.

Tukutane kwenye ukurasa wa 120 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment