Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, April 20, 2015

UKURASA WA 110; Ukomo Unaojiwekea Wewe Mwenyewe.

Mimi sio aina ya watu ambao wanaweza kufanikiwa kwenye biashara….

Mimi sio aina ya watu ambao wanapandishwa cheo kazini…

Mimi sio aina ya watu ambao wanaweza kufikia mafanikio makubwa…

Mimi sio aina ya watu ambao wanaweza kufanya mambo makubw akwneye maisha yao.

SOMA; Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

Hizi ni baadhi ya kauli ambazo umekuwa unajiambia wewe mwenyewe. Unaona mtu amefanikiwa sana kwenye biashara unafikiria wewe utawezaje kufanikiwa kama yeye lakini kabla hujafika mbali unajikuta umeshajipa jibu kwamba wewe sio aina ya watu hao. Kwamba wao walipata nafasi ambayo wewe hujapata.

Unaona wenzako wakipata mafanikio makubwa kwenye kazi zao, wakipandishwa vyeo, unajiuliza wewe utawezaje kufikia ngazi kama hizo, kabla hujapata jibu unajikumbusha kwamba wewe sio aina ya watu hao. Kwanza wao wanabahati, wana ukaribu na wengine, lakini sio wewe.

SOMA; Siri Za Kuwa Mjasiriamali Bora Na Kufikia Mafanikio Makubwa.

Yote haya unayojiambia, kwanza ni uongo na pili unajiwekea ukomo wewe mwenyewe.

Hakuna mtu ambaye amezaliwa kuwa mtu fulani, kila kitu tunajifunz ahapa duniani. Kama kuna kitu chochote ambacho hukipendi kwenye maisha yako unawez akukibadili. Kama kuna kitu chochote ambacho ungependa kuwa nacho wkenye maisha yako unawez akukipata.

Hii ni kama utaondoa ukomo huu unaojiwekea kila siku. Na ukaanz akuchukua hatua, kuendea kile ambacho unakitaka.

TAMKO LA LEO;

Najua nimekuwa nikitu ia kauzli nyingi za kujiwekea kikomo na kukatisha tamaa. Najua kuna kipindi ambapo nimejiona mimi siwezi kwa sababu mbali mbali. Nimegundua huu sio ukweli na sasa nitaendela kile ambacho ninakitaka kwenye maisha yangu. Najua hakuna kinachoshindikana kama kweli nikiamua.

SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.

Tukutane kwenye ukurasa wa 111 kesho.

Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.

Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.

Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini.

Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.

TUPO PAMOJA.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment