Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, March 2, 2014

Ni Muhimu Sana Wewe Kuwa Kiongozi.

  Katika safari ya malengo yangu ya kuwa rais wa Tanzania ifikapo mwaka 2040 moja ya maandalizi makubwa ni kujenga sifa za uongozi ndani yangu. Katika kujenga sifa kwangu mimi namkaribisha yeyote anayetaka kujenga sifa za uongozi ndani yake tuwe pamoja kwenye safari hii.

Nani anatakiwa kuwa kiongozi?

Dunia ya sasa inahitaji viongozi zaidi ya kitu kingine chochote. Kila mtu anatakiwa kuwa kiongozi na kuwa na sifa ya uongozi ndani yake.

Watu wengi wakisikia neno KIONGOZI AU UONGOZI mawazo yao yanakwenda moja kwa moja kwenye mambo ya siasa au taasisi mbalimbali. Ni kweli kwamba tunahitaji viongozi kwenye nafasi za kisiasa ama nyinginezo lakini tunahitaji viongozi wengi zaidi ya hapo.

  Uongozi ni mfumo wa maisha, uongozi ni uwezo wa kushawishi watu kuchukua hatua kwa faida yao wenyewe na uongozi ni uwezo wa kubadilisha maono kwenda kwenye uhalisia. Tabia zote hizi zinahitajika kwenye maisha yetu kuanzia kwenye familia, kazi, biashara na maendeleo.

  Ili uweze kulea familia ambapo wanafamilia wanajiamini na kuweza kufanya maisha yao kuwa bora unahitaji kuwa kiongozi mzuri.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye kazi yoyote unayofanya iwe umejiajiri au umeajiriwa ni muhimu sana kutumia sifa za uongozi zilizopo ndani yako.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye biashara ni muhimu sana kuwa kiongozi. Kuweza kuanzisha biashara ndogo na ikakua mpaka kufikia kampuni kubwa sana ni lazima uwe kiongozi mwenye maono na ushawishi mkubwa.

  Ni vigumu sana kufanikiwa kwenye dunia ya sasa kama huna sifa za uongozi ndani yako. Wote wanaofanya vizuri kwenye maisha, biashara, kazi na hata burudani ukiwafuatilia kwa karibu wamakuwa na sifa za uongozi ndani yao.

   Tumekosa viongozi

  Tumefika hapa tulipo kama taifa kwa sababu tumekosa viongozi wenye sifa za uongozi. Tumekosa viongozi kwenye nafasi za kisiasa na tumekosa viongozi kwenye kila nyanja ya maisha kuanzia ngazi ya familia mpaka kwenye biashara.

  Wengi walioshikilia nafasi za kisiasa sio viongozi, wako pale kwa maslahi yao binafsi na hili limetugharimu sana mpaka sasa.

  Tumekosa uongozi kwenye familia ndio maana sasa hivi maadili yanaporomoka kwa kasi kubwa sana. Tumekosa uongozi mzuri kwenye kazi na biashara ndio ndio maana watu wanaishia kuigana na kushindana mwishowe kupotezana

  Tunahitaji viongozi wengi wenye sifa za uongozi ili tuweze kuendelea kama taifa.

  Katika shughuli yoyote unayofanya unahusisha watu na ili uweze kufanya kazi vizuri na watu mbalimbali ambao wana mitazamo mbalimbali utafanikiwa endapo tu una sifa za uongozi. Tofauti na hapo kazi inaweza kuwa ngumu sana kwako.

  Wewe unahitaji kuwa kiongozi kwenye sehemu yako ya kazi, unahitaji kuwa kiongozi kwenye biashara yako, unahitaji kuwa kiongozi kwenye familia yako na una jukumu la kutengeneza viongozi wengi zaidi kwa maendeleo ya taifa letu.

  Kama upo tayari kuwa kiongozi jiunge nami kwenye safari hii na tujifunze na kuendeleza sifa za uongozi zilizopo ndani yetu. Weka jina lako na email yako hapo juu kwenye blog ili upate kila makala ya uongozi inapotoka moja kwa moja kwenye email yako.

  Katika safari hii tutajifunza uongozi, sifa za viongozi, uongozi na maendeleo, uongozi na siasa na jinsi ya kufanya maamuzi mbalimbali kama kiongozi.

  Tuache kulalamika sasa na tuwe sehemu ya suluhisho kwa kuanza kuchukua hatua.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment