Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Wednesday, July 17, 2013

HAKUNA JIBU MOJA SAHIHI

  Shuleni tumefundishwa kuchagua jibu moja sahihi, unapewa swali na majibu mengi ila jibu moja tu ndio sahihi. Kwenye maisha ni tofauti kabisa, hakuna jibu mja sahihi, kuna majibu mengi sahihi na mengi ambayo sio sahihi. Hakuna njia moja ya kufanikiwa kwenye maisha, zipo njia nyingi sana, baadhi zitakupeleka pazuri ningine zitakupeleka pabaya.

  Usisumbuke kujaribu kuiga kila njia ambayo baadhi ya watu wamepita wakafanikiwa, wapo wengi na zipo nyingi. Na katika njia hizo hizo walizopita wakafanikiwa kuna wengine wamezipita wakashindwa. Tafuta njia inayokufaa wewe na itumie hiyo vizuri kufikia mafanikio yako. Huwezi kupita kila njia, lazima utafute njia moja inayokufaa wewe ndio uipite.

multiple choices

  Majibu ni mengi kwenye njia ya mafanikio na sio yote yanayokufaa wewe hata kama yamewatoa wengine. Usipoteze muda kufanya kitu ambacho hakikupatii majibu unayotarajia.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment