Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Monday, September 15, 2014

Njia 10 Rahisi Za Kuondoa Msongo Wa Mawazo.

Msongo wa mawazo ni kitu kibaya sana kwa afya yako na hata kwa kazi au biashara yako. Unapokuwa na msongo wa mawazo huwezi kufanya maamuzi sahihi na hivyo kujikuta ukipata matatizo zaidi.
Japokuwa hakuna anayependa kuwa na msongo wa mawazo, maisha yetu ya kila siku yanatutengenezea msongo wa mawazo. Msongo huu unaweza kutokana na watu wanaotuzunguka au hata kazi tunazofanya.
stress2

Fanya mambo haya kumi ambayo ni rahisi sana na utaweza kuondoa msongo wa mawazo.

1. Pata muda wa kutosha wa kupumzika. Ukiweza kulala inakuwa bora zaidi.
2. Fanya matembezi ya taratibu ukiwa mwenyewe kwa muda usiopungua nusu saa. Tembea sehemu ambayo unaweza kuona vitu vya asili kama majani au miti.
3. Chukua karatasi na uandike vitu kumi kwenye maisha yako ambayo unafurahi kuwa navyo, cha kwanza furahi kwamba bado unaishi.
4. Sikiliza mziki ambao unaupenda sana. Kila mtu ana aina yake ya mziki anaipenda.
5. Kaa kimya kwa dakika tano, usifikirie chochote kwa dakika hizo tano tu. Kuhakikisha hufikirii chochote hesabu pumzi zako.
6. Nyoosha misuli yako. Kama umekaa kwa muda mrefu nyanyuka na ufanye mazoezi kidogo yatakachangamsha misuli yako.
7. Fanya kazi ya kujitolea, tenga siku moja au muda wako na ufanye kazi za jamii za kujitolea. Kwa kutoa unajisikia vizuri zaidi.
8. Panga kukutana na marafiki zako uliopotezana nao muda mrefu. Kwa kukutana nao na kukumbushana mambo mliyokuwa mnafanya utajisikia vizuri.
9. Nenda sehemu ambayo hujawahi kwenda. Utaona mambo mapya na kujifunza mambo mapya yatakayokufanya uwe na mawazo mapya.
10. Angalia vichekesho, utacheka na kubadili hali yako ya msongo.
Fanya mambo haya kuondoa msongo wa mawazo. Sio lazima ufanye yote kwa wakati mmoja. Chagua machache unayoweza kuyafanya na yakabadili hali yako ya msongo wa mawazo.
Kila la kheri.

Tafadhali Washirikishe Wengine Makala Hii Nzuri!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

0 comments:

Post a Comment