Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Saturday, July 18, 2015

Nakukumbusha Kwamba Tumeshahama hapa.

Habari za leo mpenzi msomaji wa blog hii.
Napenda kukumbusha kwamba blog hii sasa imehama na makala zotye zinapatikana kwenye www.kisimachamaarifa.co.tz
Kwa wale ambao walikuwa wanapokea makala kwa email, unapoenda kwenye KISIMA CHA MAARIFA kuna sehemu ya kuweka email yako ili uendelee kupata makala kila zinapotoka.
Nakutakia kila la kheri.
TUPO PAMOJA.

Friday, July 17, 2015

UKURASA WA 198; Tuko Upande Mmoja.

Katika shule moja kulikuwa na kundi la wanafunzi watukutu ambao walikuwa wakionea wanafunzi wenzao. Wanafunzi hao walikuwa wakikuta mwanafunzi mwingine wanamlazimisha achague wa kupigana naye na akikataa wanampiga wote.
Siku moja kundi hili walikutana na mwanafunzi mmoja aliyeonekana kuwa mnyonge sana. Wakamwambia achague wa kupigana naye. Yule mwanafunzi akachora mstari na kusema yule ambaye anajiona ndio mbabe kuliko wote avuke huu mstari. Yule ambaye ndio alikuwa mbabe alivuka mstari ule na alipofika upande wa pili yule mwanafunzi mnyonge alimwambia sasa tupo upande mmoja, tuungane kupambana na hao wengine.
Maisha ndivyo yalivyo, sisi wote tuko upande mmoja. Na watu wote wanaokuzunguka mpo nao upande mmoja. Sema watu hatuelewi hili na ndio maana tumekuwa tunashindana lakini hatufiki mbali.
Kama wanandoa wangejua kwamba wapo upande mmoja, wa kutaka maisha yao wote kuwa bora basi matatizo mengi sana ya ndoa yasingekuwepo na ndoa zingedumu.
Kama mwajiri na mwajiriwa wangejua wapo upande mmoja, kunufaisha kazi yao na maisha yao kwa ujumla, basi kungekuwa na ufanisi mkubwa sana kwenye eneo la kazi.
Kama mfanyabiashara na mteja wake wangejua kwamba wapo upande mmoja basi biashara zingeendeshwa kwa mafanikio makubwa kwa wote wawili.
Lakini mara nyingi tunafikiri kwamba tuko pande tofauti na hivyo kuishia kushindana, mashindano ambayo hayamfaidishi hata mmoja wetu.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba wale wote ambao wamenizunguka tupo upande mmoja. Mwenza wangu, wateja wangu, mwajiri/mwajiriwa wangu wote tupo upande mmoja. Kila mara nitajitahidi kuelewa upande tuliopo ili iweze kutusaidia kuboresha maisha yetu sote.
Tukutane kwenye ukurasa wa 199 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tangazo muhimu kuhusiana na blog zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS.

Habari za leo mpenzi msomaji wa blog mbalimbali zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS. Naamini unaendelea vizuri na harakati zako za kuboresha maisha yako. Na pia naamini TUPO PAMOJA ukiendelea kujifunza na kuhamasika kupitia makala mbalimbali zinazopatikana kwenye blog zako zinazoendeshwa na AMKA CONSULTANTS.
Kama unavyojua lengo kubwa la AMKA CONSULTANTS ni kukuwezesha wewe kuishi maisha bora sawa sawa na uwezo wako. Hapo ulipo una uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo makubwa zaidi ya unavyofanya sasa. Ila mfumo wa elimu uliopitia na malezi uliyokulia vimekufanya ushindwe kufikia uwezo wako mkubwa.
Kama umekuwa unafuatilia blog zetu mbali mbali na ukawa unafanyia kazi yale ambayo umekuwa unajifunza, utakubaliana nami kwamba maisha yako umeona yanabadilika, hata kama ni kwa kiasi kidogo. Kama hiki ndio kinachotokea kwenye maisha yako basi nakusihi endelea kufanyia kazi na utazidi kuona mabadiliko makubwa zaidi.
AMKA CONSULTANTS ilianza na blog ya AMKA MTANZANIA na baadae zilianzishwa blog nyingine kutokana na mahitaji tofauti ya wasomaji wetu. Blog hizo ni KISIMA CHA MAARIFA, ambayo unalipia kuwa mwanachama, MAKIRITA AMANI na JIONGEZE UFAHAMU.
Kupitia blog hizi umekuwa unajifunza mambo mengi na mazuri sana. Kwa sababu makala zinazowekwa kwenye blog hizi zinatofautiana na zinalenga maeneo tofauti tofauti ya maisha yako ikiwemo kazi, biashara na hata maisha kwa ujumla.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha wasomaji wote kwamba kutakuwa na mabadiliko kwenye blog hizi zinazoendeshwa na AMKA CONSULTSNTS. Makala ambazo zilikuwa zinawekwa kwenye JIONGEZE UFAHAMU sasa zitahamishiwa kwenye AMKA MTANZANIA na makala zilizokuwa zinawekwa kwenye MAKIRITA AMANI sasa zitahamishiwa kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Na blog hizi mbili, MAKIRITA AMANI na JIONGEZE UFAHAMU zitafutwa.
Kwa nini mabadiliko haya?
Kama umekuwa msomaji mzuri wa blog hizi utakuwa uliona tatizo ambalo lilijitokeza kama mwezi mmoja uliopita. Wasomaji ambao walikuwa wanapokea makala za blog moja wapo kwa email ghafla waliacha kupata makala. Wakati huo makala zilikuwa zinatumwa kama kawaida. Kutokana na tatizo hili ilibidi kutafuta suluhisho la haraka ili wasomaji waendelee kupata makala zetu nzuri. Tulipata suluhisho la muda lakini halitadumu kwa muda mrefu, siku zio nyingi tutaingia tena kwenye tatizo kama lile. Na hii inatokana na sababu ya pili ya kuondoka kwenye blog hizi ambayo ni kuwa zimekuwa zinaendeshwa bure.
Blog inapokuwa imehifadhiwa bure na kutumia jina la bure, kuna baadhi ya vitu huwezi kuvibadili. Sasa hili linakwenda tofauti na kile ambacho nataka wewe msomaji ukipate. Kuna wakati nataka kufanya kitu ambacho ni cha tofauti lakini nashindwa kwa sababu blog imehifadhiwa bure na hivyo huwezi kubadili baadhi ya vitu.
Sababu nyingine ni kwamba nina sehemu kubwa ya kuhifadhi blog hizi ambayo ninailipia kila mwaka ambayo kwa sasa imehifadhi KISIMA CHA MAARIFA, sasa ni vyema kutumia sehemu hii ambayo tunailipia gharama kubwa kuweka mafunzo ambayo yataendelea kuboresha maisha yako.
Na sababu ya mwisho tunayoweza kujadili hapa ambayo imepelekea kufanya mabadiliko haya ni wewe msomaji uweze kupata makala zote nzuri kwenye blog chache. Ni kweli kuna umuhimu wa kutenganisha mambo lakini ni vyema wewe kama msomaji ukijua unapata makala zako zote nzuri kwenye sehemu chache ambazo unaweza kuzitembelea kila siku na kutumia muda wao vizuri.
KISIMA CHA MAARIFA ni kulipia, je sisi tuliokuwa tunapata makala bure ndio mwisho?
Ni kweli kabisa ili uweze kusoma makala kwenye KISIMA CHA MAARIFA inabidi uwe umejiunga na ulipie. Ila kwa sasa kwa kipengele hiki cha KURASA 365 ZA MWAKA 2015 wasomaji wote wataendelea kuzipata hata kama hawajajiunga na kulipia. Ila nakusihi sana kama bado hujajiunga na KISIMA CHA MAARIFA ufanye hivyo mara moja kwani unakosa mengi na utaendelea kukosa mengi. Bonyeza maandishi haya KUJIUNGA NA KISIMA CHA MAARIFA. Kuendelea kupata makala za KURASA 365 hakikisha unatembelea KISIMA CHA MAARIFA kila siku, na pia jiunge kwa kuweka email yako unapokuw akwneye KISIMA na utatarifiwa kila makala inapokwenda hewani.
Asante sana kwa kuendelea kujifunza na kufanyia kazi yale ambayo yanawekwa kwenye mitandao hii. Tunaendelea kukuahidi kwamba tutakuletea makala bora kabisa zitakazo boresha na kubadili maisha yako.
TUPO PAMOJA.
Makirita Amani,
makirita@kisimachamaarifa.co.tz

Thursday, July 16, 2015

UKURASA WA 197; Una Sababu Moja Tu, Nyingine Zote Ni Kuchagua.

Umekuwa ukisikia mara nyingi kwamba kosa sio kutenda kosa, bali kosa ni kurudia kosa. Hii ikiwa na maana kwamba unapofanya jambo kwa mara ya kwanza na ukapata majibu ambayo hukutegemea kupata, tunaweza kukusamehe. Ila tunatarajia kwamba uwe umejifunza kwamba njia uliyotumia mwanzo haileti majibu unaotaka.
Sasa kama wewe utarudia tena kufanya vile vile na ukapata majibu yale yale ambayo hukuyataka ndio tunasema kwamba wewe unafanya makosa. Nafikiri tumeelewana vizuri hapo kwenye kosa, na unajua ni makosa gani ambayo umechagua kuwa unayafanya tena na tena.
Sasa leo nataka nikuambie kitu kingine kizuri ambacho kinaweza kuendana na hiko. Una sababu moja tu, nyingine zote ni kuchagua mwenyewe. Kwa maana nyingine unaweza kuwa na kisingizio mara moja tu, baada ya hapo umeamua mwenyewe na huna sababu au kisingizio chochote.
Kwa mfano; kwa nini kila siku unasema utaanza biashara ila huanzi? Sababu ya kweli, sina mtaji. Swali hilo tena miaka mitano baadae, kwa nini mpaka sasa hujaanza biashara... hapa ukisema tena huna mtaji sio sababu tena, maana yake unajua kabisa kwamba huna mtaji na hufanyi jitihada zozote kutafuta mtaji huo.
Usipende kutafuta sababu(visingizio), ila kama haikwepeki, basi sababu iwe mara moja tu. Kama utaendelea kutuambia sababu ile kila siku sio sababu tena bali umeamua kuishi maisha hayo. Hivyo tafadhali sana, usitupigie tena kelele, tumeshasikia sababu yako na umeshatuambia kwamba umekubali kuishi nayo.
TAMKO LA LEO;
Najua nina nafasi moja tu ya kuwa na sababu au kisingizio. Ila baada ya hapo siwezi tena kutumia kisingizio hiko kwa sababu nitakuwa nimeamua mwenyewe. Kuanzia leo nitakwepa kutoa sababu na kama sababu haikwepeki nitatoa mara moja tu.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, July 15, 2015

UKURASA WA 196; Kama Huwezi Kujibu Swali Hili Hujui Maisha Yako Yanakoelekea.

Siku zote huwa nasema kwamba kuna ‘emergency’ chache sana kwenye maisha. Ile hali kwamba jambo limetokea na watu wanashangaa limetokeaje ni kuamua tu kutumia unafiki wetu wenyewe.
Ni sawa na shimo ambalo lipo njiani kwa muda mrefu lakini watu wanaliangalia tu, siku moja linasababisha vifo watu wanasema ni ajali. Hapana sio ajali, ni watu wamechagua kufa kwa njia hiyo. Kwa sababu shimo lilikuwa linaonekana siku zote, lakini hakuna aliyejali.
Hivyo hivyo kwenye maisha yako, kuna vitu vingi sana ambavyo unavipuuzia kwa sasa lakini kuna siku vitakukaba sana. Na wakati huo ndio utaanza kuhangaika, utaanza kusumbua wengine kwamba kwa nini hawachukulii hali yako kwa tahadhari. Bila ya wewe kujua na kukubali kwamba hakuna tahadhari kubwa ila ni kitu ulichotengeneza wewe mwenyewe.
Kila siku inayoanza jiulize swali hili muhimu sana, je mambo haya ninayofanya leo hayatengenezi tahadhari siku ya kesho? Au siku zijazo? Mambo ninayoyapuuza leo hayajitengenezi na kuwa makubwa halafu siku moja yakanizidi?
Ni kawaida ya binadamu kufanya vitu kwa mazoea ila mambo yanapokuwa magumu tunasahau kwamba tumeyatengeneza wenyewe. Na kama wewe ni mtu wa kulaumu utaanza kulaumu na uzuri ni kwamba hutakosa mtu wa kumlaumu.
Hakuna kitu kinachokea kwa ajali kwenye maisha yako, kila kitu kinasababishwa na wewe mwenyewe ndiye unayesababisha. Kuwa makini na yale yote unayofanya, yanaweza kukusababishia matatizo makubwa siku za mbeleni.
TAMKO LA LEO;
Najua chochote ninachofanya leo kina madhara kwenye maisha yangu siku za baadae. Madhara haya yanaweza kuwa chanya au kuwa hasi. Nitahakikisha maamuzi ninayofanya hayanipelekei kwenye madhara hasi ili niepuke kuwa na dharura zisizo za msingi kwenye maisha yangu.
Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tuesday, July 14, 2015

UKURASA WA 195; Dunia Inapenda Washindi, Usiumizwe Na Hilo.

Wakati unaweka juhudi za ziada zaidi ya wengine hakuna atakayekutukuza, na wengine wengi watakukatisha tamaa.
Wakati wewe unafanya kazi wakati wengine wamepumzika, wanastareheka hakuna atakayekuwa anakumulika, na wanaojua watakuwa wanakubeza na kukuona hujui unachofanya.
Kama utaendelea kung’ang’ana na kuweka juhudi licha ya watu kukususa na wengine kukukatisha tamaa, unajua ni nini kitatokea?
Mambo yako yatakuwa mazuri, utaanza kupata majibu tofauti na wengine wanayopata, kila mtu ataanza kuona mafanikio yako. Na wakati huu unajua ni kitu gani kitatokea?
Kila mtu ataanza kukutukuza, kukusifu, huyu hakukata tamaa. Na wanaokujua wataanza kusema tulijua tu atafika mbali, wakati hakuna hata siku moja wamekutia moyo.
Je utawachukia watu hawa kwa sababu ni wanafiki, wanakusifia wakati tu umefikia mafanikio? Hapana usifanye hivyo, sio kosa lao, ndivyo dunia ilivyowatengeneza. Dunia inapenda washindi, dunia haina muda na wanaoteseka, wanaokazana na ukishindwa ndio kabisa utakuwa mfano wa kuwatisha wengine.
Ufanye nini sasa? Endelea kuweka juhudi, endelea kushinda. Hata pale wanapokusifia usione ndio umefika mwisho, wacha wao waendelee kutoa sifa, na wewe endelea kuweka juhudi.
TAMKO LA LEO;
Najua dunia inapenda washindi. Hainisumbui kama sasa hivi hakuna anayeniona pamoja na juhudi kubwa ninazoweka. Na hata nitakapofikia mafanikio na waliokuwa wa kwanza kunicheka wakawa ndio wa kwanza kusema walijua nitafanikiwa pia halitakuwa tatizo kwangu. Mimi nitaendelea kuweka juhudi bila ya kujali watu wanasema nini.
Tukutane kwenye ukurasa wa 196 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Monday, July 13, 2015

UKURASA WA 194; Utaanza kuona fursa nzuri pale utakapofanya hivi.

Hivi ulishawahi kununua nguo ambayo uliona ni nzuri na ya kipekee ila kila ulipopita mtaani ukaanza kuona karibu kila mtu anayo?
Au labda unafikiria kununua kitu fulani mfano gari au vifaa, mara ghafla ukiwasha tv unaona kitu kile, ukipita mtaani unaona kitu kile?
Au umewahi kufikiria kufanya biashara fulani mara ghafla ukaanza kuona kila unapopita unaona watu wanafanya biashara ile?
Je unafikiri vitu hivyo nimeanza kutoke kwa sababu wewe unafikiria kufanya? Jibu ni hapana, vitu hivyo vilikuwepo kila siku, ila kwa sababu hujawahi kuvifikiria na kuvizingatia basi umekuwa huvioni. Ila unapoanza kuvifikiria au kuvizingatia sana macho yako yanafunguka na unaanza kuona vizuri zaidi.
SOMA; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.
Kuna fursa nyingi sana ambazo zinakuzunguka hapo ulipo. Ila kwa sasa huzioni kwa sababu hujazingatia kuzifikiria. Anza kufikiria kitu fulani na utaanza kuona kwamba kuna njia nyingi sana za kuweza kukipata au kukifanya kitu hiko?
Unataka kuona fursa zaidi? Fungua akili yako, fungua mawazo yako na macho yako yataanza kuona.
TAMKO LA LEO;
Najua nimekuwa sioni fursa nyingi kwa sababu macho yangu hayajafunguliwa kuona. Nitayafungua sasa macho yangu kwa kuzingatia vitu ninavyotaka, kuviweka kwenye akili yangu na macho yangu yatanionesha njia za kufanya au kupata vitu hivyo.
Tukutane kwenye ukurasa wa 195 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Sunday, July 12, 2015

UKURASA WA 193; Ushabiki Unavyokuzuia Kufikia Mafanikio.

Ushabiki umekuwa kikwazo kwa watu wengi sana kuweza kufikia mafanikio makubwa. Watu wamekuwa wakijikuta wanalazimika kuacha mambo yao ya msingi kwa sababu hataki kupitwa na kitu ambacho anashabikia.
Kuna watu ambao ni mashabiki wa mpira kiasi kamba hawezi kuacha kuangalia timu yake inacheza hata kama kutakuwa na kitu gani anachofanya. Kuna wengine ni mashabiki wa muziki, mashabiki wa tamthilia, mashabiki wa matamasha mbalimbali na pia mashabiki wa siasa.
Sina tatizo na wewe kuwa shabiki, ila kama kweli lengo lako ni kuwa na maisha bora na yenye mafanikio basi unatakiwa kufikiria mara mbili kuhusu ushabiki wako.
Fikiria kile unachoshabikia na jiulize, je kinakuongezea maarifa? Je kinakuongezea kipato? Je kinafanya maisha yako na ya wengine kuwa bora zaidi/ kama jibu ni hapana basi ushabiki huo usiwe kipaumbele kwenye maisha yako.
SOMA; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.
Mimi nilikuwa mshabiki wa tamthilia mpaka siku moja mtu akaniambia(kupitia kitabu nilichokuwa nasoma), unapoangalia tv, kuna mambo mawili yanatokea. Yule unayemwona kwenye kioo cha tv analipwa kwa wewe kumwangalia na wewe unalipa kumwangalia mtu huyo. Je unataka kuwa upande upi? Kulipa uangalie maisha ya wengine au kulipwa kwa watu kuangalia maisha yako? Kuanzia hapa nilikata shauri la kutoangalia tamthilia tena, sijaziangalia tangu mwaka 2012 na hakuna nilichokosa zaidi ya maisha yangu kuwa bora zaidi.
Achana na ushabiki ambao hautaboresha maisha yako na anza leo kuwa shabiki wako mwenyewe. Mimi ni shabiki namba moja wa Makirita Amani, huwa sikosi chochote alichopanga kufanya na nitaahirisha vingine vyote ili kuhakikisha namshabikia. Je shabiki wako namba moja ni nani?
Una muda mfupi sana kuanza kuugawa kwa kushabikia vitu ambavyo havina msaada mkubwa kwenye maisha yako, hasa ambavyo unaweza kuvipata baadae. Kwa mfano kama unashabikia timu ya mpira, badala ya kukesha ukiangalia mpira na kesho yake ukashindwa kufanya kazi zako vizuri kwa nini usilale mapema na kesho yake utayajua tu matokeo? Hakuna tofauti yoyote kuona magoli mawili yakifungwa na kuja kuyaona kesho yake. Tena siku hizi mipira inarekodiwa kwa hiyo unaweza kuangalia kwa muda wako.
Narudia tena, usikubali ushabiki uharibu ratiba zako, una mengi yakufanya, yape kipaumbele.
TAMKO LA LEO;
Najua ushabiki wangu umekuwa unanifanya nishindwe kufikia mafanikio makubwa. Nimekuwa nashabikia mambo mengi sana. Nimekuwa naahirisha mipango yangu kwa sababu tu nisipitwe na ushabiki. Leo naamua kwamba mtu wa kwanza kumshabikia ni mimi mwenyewe. Sitakatisha ratiba zangu kwa sababu kuna kitu nakishabikia. Nitaendelea na mipango yangu na ninajua nitafahamishwa kila kinachoendelea.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Saturday, July 11, 2015

UKURASA WA 192; Tatizo La Kuweka Kipimo Cha Furaha, Na Kwa Nini Hukifikii.

Kuna watu ambao huwa wanaweka furaha kwenye kipimo. Mtu anafikiri nikishapa kitu fulani basi nitakuwa na furaha sana.
Kwa hiyo huwa inaanza hivi;
Uko mtoto mdogo unatamani sana kwenda shule unasema nikianza darasa la kwanza nitafurahi sana. Unaanza na unagundua hakuna kitu cha tofauti sana.
Unaendelea na shule kwa miaka saba, unapokaribia mwisho unasubiri kwa hamu sana ukisema nikimaliza darasa la saba tu, nitakuwa na raha sana. Unamaliza na unaona kumbe kilikuwa kitu cha kawaida sana.
Unaanza sekondari unasoma na kufikiria nikimaliza tu, nitakuwa na raha, unamaliza na maisha ni yale yale.
SOMA; Ndege Wa Angani Hawalimi Ila Wanakula, Kuna Mambo Haya Matano(5) Pia Wanakuzidi Ujanja.
Hivyo hivyo mpaka unaingia chuoni, unafikiria nikimaliza na nikapata kazi, maisha yangu yatakuwa ya furaha sana. Unamaliza na labda unapata kazi na unakuta ni kawaida tu na huenda ukakutana na changamoto nyingi zaidi.
Hivyo pia inakuwa kwenye kila kitu unachofanya kwenye maisha yako, unafikiri ukipata kitu fulani utakuwa na furaha, ila unakifanya na unagundua kuna kingine zaidi cha kufanya.
Ni vigumu sana kupima furaha kwa vipimo hivi hasa pale unaposogeza kipimo kila unapokifikia.
Wakati sahihi kwako kuwa na furaha ni sasa hivi, hapo ulipo na unaposoma hii. Na utakapotoka hapo kila wakati kuwa na furaha. Kama unafikiria utaipataje furaha chukua kalamu na karatasi na andika vitu kumi unavyoshukuru kuwa navyo hapo ulipo. Huenda ni kazi au biashara inayokupatia fedha za kuendesha maisha, huenda ni familia inayokupenda, huenda ni marafiki mnaopendana na kadhalika.
Huwezi kupima furaha na ukaipata, furaha ipo ndani yako, ni wewe kuifikia na kuiishi.
TAMKO LA LEO;
Kuanzia sasa naacha kupima furaha kwa sababu nimegundua kwamba kuweka kipimo kwenye furaha ni sababu namba moja ya kushindwa kuifurahia. Hapa nilipo nina furaha kwa sababu nina vitu hivi vifuatavyo(soma orodha yako ya vitu kumi).
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Friday, July 10, 2015

UKURASA WA 191; unalipwa kwa sababu unaonekana au kwa sababu unatoa thamani?

Swali muhimu sana hilo kujiuliza kama hujawahi kufanya hivyo. Ngoja nikuulize tena vizuri ili twende sawa,
Je unalipwa mshahara kwa sababu unaonekana kazi au kwa sababu una thamani unayotoa kwenye kazi yako?
Je mteja wa biashara yako ananunua kutoka kwako kwa sababu amekuona na wewe unafanya biashara au kwa sababu kuna thamani anaifuata?
Jipe muda wa kujibu swali hili, maana ndio msingi wako wote wa mafanikio umelala hapo.
Kulipwa kwa kuonekana.
Hapa ni pale unapotegemea malipo kwa sababu tu umeonekana kazini, au kwa sababu tu na wewe unauza. Hivyo kinachotokea ni wewe kujionesha kwamba na wewe upo. Kama ni kazini basi unahakikisha unaonekana una kazi nyingi na upo bize kumbe hakuna thamani kubwa unayotengeneza. Ukiwa mtu wa aina hii inakubidi uonekane una juhudi sana kumbe ukweli sio hivyo.
Kama ni biashara unakazana kutangaza ili uonekane na wewe upo.
Tatizo la kutegemea kipato kwa njia hii ni kwamba huwezi kupata kipato kizuri na huwezi kujiamini.
SOMA; Ukiendelea Na Maisha Haya Watu Watakunyanyasa Sana…
Kulipwa kwa kuongeza thamani.
Hiki ndio wanachofanya watu wote wenye mafanikio. Hawaendi kazini ili waonekane na wao wamekuja, ila wanakwenda pale kuleta mabadiliko. Kuongeza thamani kwenye kile wanachofanya na hivyo kuwanufaisha wengi zaidi.
Kama ni wafanyabiashara wanakazana kutatua matatizo yanayowasumbua wengi. Na kwa kuwa suluhisho lao ni bora watu wanakuwa wanawatafuta wenyewe.
Na kwa upande wa kipato, watu hawa wao wenyewe ndio wanaamua walipwe kiasi gani, wakitaka kuongezwa kipato wanaongeza thamani wanayotoa.
Je umeshajua uko wapi? Kazana kuongeza thamani na sio kukazana kuonekana. Unapokazana kuonekana maana yake unapiga kelele. Unapokazana kuongeza thamani umuhimu wako pia unaongezeka. Na kila mtu atataka kufanya kazi na wewe. Na utaanza kupanga ulipwe kiasi gani.
TAMKO LA LEO;
Najua njia bora ya kutengeneza kipato sio kwa kuonekana bali kwa kuongeza thamani. Kuanzia sasa nitakuwa nakazana kuongeza thamani na sio kuwapigia watu kelele ili wajue kama nipo. Najua nitakapotoa thamani kubwa na kipato changu pia kitaongezeka.
Tukutane kwenye ukurasa wa 192 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Thursday, July 9, 2015

UKURASA WA 190; Huwezi Au Hutaki? Kabla Hujaniambia Huwezi, Hakikisha Huponi.

Mpaka sasa umeshajifunza mambo mengi sana kuhusu mbinu za kuboresha kazi yako, biashara yako na hata maisha yako kwa ujumla. Lakini mbona bado huchukui hatua yoyote ili kuweza kunufaika na yale ambayo unajifunza?
Mpaka sasa unajua kabisa ya kwamba kwa kufanya kile ambacho kila mtu anafanya utaendelea kupata matokeo ambayo kila mtu anayapata na ambayo sio mazuri sana. Lakini mbona unaendelea kufanya hivyo?
SOMA; Maisha Ni Mchezo Na Sheria Za Kuushinda.
Mpaka sasa unajua kabisa kulalamika au kulaumu wengine hakutakupatia wewe chochote unachotaka, sana sana kutakufanya ujione kama yatima ambaye hana msaada wowote. Lakini bado unaendelea kulalamika na kulaumu, kwa nini?
Kwa sababu huwezi!! Hili ndio jibu ambalo unajiridhisha nalo. Kwamba siwezi kufanya tofauti, kila mtu ameshazoea vile nilivyo. Kwamba siwezi kuweka muda zaidi kwenye kujifunza, kwa sababu nina mambo mengi ya kufanya. Kwamba siwezi kuacha kuangalia tv kila siku, nitapitwa na mambo mengi. Kwamba siwezi kuacha kukaa na jamaa zangu kila siku jioni tukipata moja moto na moja baridi ili nifuatilie zaidi biashara na kazi zangu.
Kama haya ndio majibu yako, kwanza wewe mwenyewe unayaamini kweli? Ni kweli kwamba huwezi kufanya mambo hayo ambayo yatabadili kabisa maisha yako? Vipi kama maisha yako ndio yangekuwa yanategemea hivyo ndio uweze kuishi. Kwa mfano unaambiwa kuchagua kuishi ila usiangalie tv au uangalie tv halafu unakufa, ungechagua nini?
Najua ungechagua kutokuangalia tv, safi sana, una maamuzi mazuri. Na ndio maana mimi siamini kwamba yale yote unayosema huwezi ni kwamba huwezi kweli, bali ni kwamba hutaki tu kufanya.
Kwa hiyo mambo yote unayosema kwamba huwezi, ukweli ni kwamba hutaki tu kufanya. Na kwa maana hii basi nakuomba kuanzia leo usiseme tena SIWEZI, sema SITAKI.
Siku nyingine kabla hujaniambia huwezi hakikisha kwamba ukifanya kitu hiko unakufa, vinginevyo ni sitaki.
TAMKO LA LEO;
Najua hakuna kitu kizuri na cha kubadili maisha yangu ambacho siwezi kufanya. Vingi ninavyoona siwezi kufanya ni kwamba sitaki tu kufanya. Kwa sababu kama maisha yangu yangekuwa yanategemea vitu hivyo ni lazima ningefanya. Hakuna kinachonishinda kufanya, na kuanzia sasa nitaacha kutumia sababu hii kwamba siwezi.
Tukutane kwenye ukurasa wa 191 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, July 8, 2015

UKURASA WA 189; Matatizo Yote Ya Mahusiano Yanaanzia Hapa... Sehemu Ya Pili(2)

Jana nilikushirikisha sababu kubwa ya matatizo kwenye mahusiano yetu sisi na watu wengine. Na kama ukiweza kuondokana na chanzo kile basi utapunguza sehemu kubwa sana ya matatizo kwenye mahusiano yako iwe ya kikazi, kibiashara, kindugu au kimapenzi. Kama hukupata nafasi ya kusoma kile tulichojadili jana basi kisome hapa; Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.
Leo nataka tugusie kitu kingine kikubwa sana kinacholeta matatizo kwenye mahusiano yetu. Najua eneo la mahusiano ndio eneo gumu sana kuelewana na watu kwa sababu moja kubwa, inapokuja swala la mahusiano watu hawatumii akili kufikiri, bali wanatumia hisia kufikiri. Na pale hisia zinapojiongoza zenyewe bila akili basi hapo ni majanga. Ndio maana ni vigumu sana kuweza kumweleza mtu kuhusu mahusiano hasa ya mapenzi akakuelewa.
Sasa sababu nyingine kubwa ambayo inasababisha matatizo kwenye mahusiano ni watu kuvaa visanamu mwanzoni mwa mahusiano. Watu wanapokutana ili kujenga uhusiano, wengi wanadanganya, wanasema vitu ambavyo vitawafanya wakubalike au kupendwa na wale wanaotaka kuwa na mahusiano nao. Hii ni kwenye mahusiano yote, iwe ya kazi, biashara au hata mahusiano mengine ya karibu.
SOMA; Katika Kula Ujana Usifanye Mambo Haya Matano, Utajutia Maisha Yako Yote.
Mtu anadanganya kwenye usaili wa kazi ili aonekane ni bora na kupewa kazi. Labda hudanganyi vitu vikubwa, ni vitu vidogo vidogo tu kama kuahidi vitu ambavyo unajua kabisa huwezi kufanya kwa muda mrefu.
Au kwenye biashara unamdanganya mteja kwamba unaweza kufanya kitu fulani ili akubali kufanya biashara na wewe.
Kwenye mapenzi sasa, ndio mtu atadanganya vitu vingi sana, atabadili mpaka mfumo wa maisha, kuacha baadhi ya vitu na kadhalika.
Mambo yangekuwa rahisi sana kama kila mtu angeweza kuishi na hiki alichoahidi anaweza kufanya. Lakini kama tulivyoona jana, watu hawabadiliki, tena kwa haraka hivyo.
Kwa hiyo mtu atafanya kile alichosema kwa muda mfupi baada ya hapo anachoka na hivyo kurudia maisha yake ya zamani. Hapa ndio utasikia siku hizi fulani kabadilika. Hapana hajabadilika, amechoka kuvaa kile kisanamu na sasa ameanza kuonesha ukweli wake.
Kuwa makini usivae kisanamu wakati unataka kujenga mahusiano ambayo yatadumu. Kuwa mkweli, kama mtu hawezi kukukubali kwa ukweli wako hata ukimdanganya huo uhusiano hautadumu. Nasisitiza tena hii sio kwa mapenzi tu, bali kwenye mahusiano ya kazi, biashara na hata maisha ya kawaida. Kuwa mkweli na utawavutia wale wa kweli. Vaa kisanamu na utavutia visanamu vingine.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba kudanganya mwanzoni mwa mahusiano ni kujenga kifo cha mahusiano hayo. Hakuna uongo unaoweza kudumu kwa muda mrefu. Nitakuwa mkweli siku zote ili niweze kujenga mahusiano bora na yatakayoniletea mafanikio. Hata kama kuwa kwangu mkweli kutanikosesha baadhi ya mahusiano, najua kutanijengea mahusiano ambayo ni bora.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Tuesday, July 7, 2015

UKURASA WA 188; Matatizo Yote Ya Mahusiano Huanzia Hapa.

Kama kuna kazi ngumu hapa duniani basi ni kuishi. Ndio maisha ni mazuri na ndio maisha ni matamu ila ni kazi kubwa sana kuweza kuyaishi.
Ni kazi kubwa kuyaishi kwa sababu huwezi kuishi maisha ya peke yako. Umezungukwa na watu wengi na watu hawa wana tabia tofauti tofauti. Watu wote hawafanani tabia.
Kuna wakati unafikiri kama watu wote wangekuwa kama fulani basi mambo yangekuwa mazuri sana. Saa nyingine unafikiria kama wateja wote wangekuwa kama mteja fulani basi biashara ingekuwa nzuri sana. Au wakati mwingine unafikiria kama bosi wako angekuwa na roho ya tofauti na aliyonayo sasa basi maisha yako ya kazi yangekuwa mazuri sana.
Lakini ukweli ndio huo kwamba watu hatufanani na pamoja na tofauti zote hizo bado unahitaji kushirikiana na watu wote hao.
SOMA; Tabia Saba Za Watu Wasiokuwa Na Mafanikio.
Matatizo yote ya kwenye mahusiano, yawe ya kindugu, ya kibiashara, ya kikazi au hata ya kimapenzi yanaanzia pale mtu mmoja anapotaka kumbadilisha mwingine. Yaani ikishafikia hatua hii kwamba mtu mmoja anataka mwingine abadilike, ndio matatizo makubwa sana yanaibuka.
Unajua ni kwa nini? Kwa sababu mwanadamu atafanya kitu chochote kile kinachowezekana ili mradi tu asibadilike. Watu hawapendi kubadilishwa na wanapenda kuendelea kuwa vile walivyo. Tena kama ndio mtu mzima, ndio basi kabisa, atahakikisha anakataa kubadilika hata kama kufanya hivyo kunagharimu maisha yake.
Wakubali watu vile walivyo, au kama huwezi kuwakubali walivyo achana nao. Kama wataona wewe ni wa muhimu sana na hawawezi kukupoteza basi watabadilika wao wenyewe. Na mtu anapoamua yeye mwenyewe kubadilika inakuwa rahisi kwake kubadilika hata kwa kiasi kidogo. Ila kama wewe ndio unamlazimisha mtu abadilike, okoa nguvu zako.
TAMKO LA LEO;
Najua matatizo makubwa kwenye mahusiano ya watu huwa yana anza pale watu wanapojaribu kuwabadilisha wengine. Najua ya kwamba binadamu hawapendi kubadilishwa. Sitapoteza nguvu zangu kutaka kumbadilisha mtu. Nitamkubali mtu kama alivyo na kama siwezi nitaachana naye iwe ni mteja, bosi, ndugu au mwingine wa karibu. Muda wangu ni wa thamani sana siwezi kuupoteza kwa kufanya kazi ambayo haileti matunda.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Monday, July 6, 2015

UKURASA WA 187; Usikubali jua lizame leo kabla hujafanya kitu hiki muhimu.

Siku ya leo kuna watu wengi sana watakaokuudhi. Kuna watu wengi watakukasirisha na wengine watakufanya ujisikie vibaya sana. Kwa hasira inayotokana na watu hawa unaweza kufanya maamuzi ambayo sio mazuri sana kwao na kwako pia.
Ila kumbuka mara nyingi unapokuwa na hasira huwezi kufanya maamuzi ambayo ni sahihi. Na hata kama mtu atakuchukiza kiasi gani, hata kama atakuudhi kiasi gani kwa wewe kuwa na hasira, kwa wewe kuendelea kuwa na kinyongo naye haimuumizi yeye bali inakuumiza wewe mwenyewe.
SOMA; JICHO KWA JICHO; Tutabaki Na Dunia Ya Vipofu.
Sasa leo nataka nikupe kitu kimoja muhimu cha kufanya kabla jua halijazama. Hakikisha jua linapozama umemalizana na kitu hiki ili siku yako ya kesho iwe bora sana.
Kabla jua halijazama leo hakikisha umewasamehe wote waliokukosea leo. hakikisha umeondokana na vinyongo vyote ambavyo unaweza kuwa umejitengenezea kwa siku ya leo. Acha mambo haya yote yazame na jua la leo, ili jua linapochomoza kesho uanze siku yako ukiwa vizuri na uweze kufanya makubwa.
Usikubali jua lizame ukiwa bado na hasira au kinyongo. Vitu hivi havikusaidii chochote zaidi ya kufanya maisha yako kuwa magumu na hata kuharibu afya yako.
TAMKO LA LEO;
Sitakubali siku ya leo na siku nyingine yoyote ipite nikiwa na kinyongo au hasira kwenye moyo wangu. Jua litakapozama nitahakikisha nimeachia yote niliyokumbana nayo siku ya leo. kama kuna mtu ameniudhi, amenikasirisha au amefanya chochote ambacho kimenifanya niwe na kinyongo nitamsamehe. Maisha yangu ni muhimu zaidi ya chuki ninazotaka kutengeneza na watu.
Tukutane kwenye ukurasa wa 188 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Sunday, July 5, 2015

UKURASA WA 186; Kama Utashindwa Kufanya Chochote Utakachojifunza, Basi Fanya Hiki Kimoja Tu, Na Maisha Yako Yatagusa Wengine.

Nimekuwa nakushirikisha mambo mengi sana ambayo unahitaji kuyafanya ili kuboresha maisha yako. Mambo haya yanahitaji wewe ubadilike, uanze kufanya tofauti na ulivyozoea kufanya na sio kitu rahisi sana.
Kuacha kuangalia tv na kujisomea mambo yatakayokuweka mbele zaidiinahitaji kujitoa kweli.
Kuacha kukaa na jamaa zako kila jioni mkipata moja moto na moja baridi ili upate muda mwingi zaidi wa kuweka kwenye kazi au biashara yako sio kitu rahisi.
Kuacha kulalamika pale unapoona kabisa kwamba umeonewa au umeumizwa inahitaji nguvu ya ziada.
Kuacha usingizi na kuamka asubuhi na mapema sana ili uweze kujifunza na kuipangilia siku yako sio kitu rahisi kama unavyoweza kufikiria.
Tuseme labda wewe umeona kwamba mambo haya yote huwezi, kwa sababu tu una uvivu uliopitiliza au kwa kifupi basi tu hutaki kujihangaisha. Leo nataka nikuambie kitu kimoja muhimu sana cha kufanya.
SOMA; Kauli KUMI Za Marcus Aurelius Zitakazokufanya Uyaone Maisha Kwa Utofauti.
Tafadhali sana hata kama una uvivu kiasi gani, jitahidi ufanye kitu hiki kimoja na maisha yako yatagusa wengine kwa kiasi kikubwa sana.
Kitu chenyewe ni kuishi maisha mazuri kwako na kwa wanaokuzunguka. Kuwa mtu mwema, usimwibie mtu, usisengenye mtu, usijihusishe na majungu. Saidia wengine kadiri ya uwezo wako. Yaani kuwa tu mtu mwema na wengine waone wewe ni mfano wa kuigwa. Na hata kama kuna mtu amekosa tumaini kwa kuyaona maisha yako atapata tumaini kwamba dunia bado ina watu wema waliomo.
Hili ni jambo muhimu kwetu sote kufanya hata kama unafanya hayo mengine yote unayojifunza kila siku.
TAMKO LA LEO;
Nitahakikisha naishi maisha ambayo yatakuwa mfano mzuri kwa watu wengine. Nitajiepusha na mambo ambayo sio mazuri kwangu na kwa wale wanaonizunguka. Sitoiba wala kumdhulumu mtu, sitosengenya wala kushiriki majungu na nitasaidia wengine kadiri ya uwezo wangu.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Saturday, July 4, 2015

ONGEA NA KOCHA; Epuka Vipimo Hivi Viwili Ambavyo Jamii Inakupima Navyo.

#ONGEA_NA_KOCHA
Kwa miaka mingi dunia imekuwa inatupima kwa mambo haya mawili makuu...
Wanawake wamekuwa wakipimwa kwa kuonekano wao. Ni mzuri au sio mzuri?
Wanaume wamekuwa wakipimwa kwa umiliki wao. Je ana hela au hana hela, ana mali au hana mali?
Jamii nzima tumekuwa tukifanya hivi japo kwa unafiki tunaweza kukataa.
Vipimo hivi vimekuwa vinawazuia watu wengi kushindwa kufikia mafanikio kwa sababu tu wanatengwa na vipimo hivi.
Kama jamii inasema mwanamke mzuri ndio anaweza kuwa na maisha mazuri, kuna makabila mwanamke mweupe mahari yake ni kubwa kuliko mweusi, yule ambaye anakosa sifa hii atajiona hawezi kuwa na maisha mazuri.
Kama jamii inasema mwanaume mwenye hela ndio wa maana, kwenye jamii zetu wanaosikilizwa ni wenye hela hata kama hawana mawazo mazuri, ambaye anakosa sifa hii atajiona yeye sio wa maana na hivyo kujiondoa kabisa kwenye njia ya mafanikio.
Sasa mimi kama kocha wako nakutangazia rasmi kwamba achana kabisa na vipimo hivi vya hovyo.
Wewe ni zaidi ya vipimo hivi vilivyowekwa na jamii. Haijalishi una uzuri au ubaya, wewe ni bora sana. Haijalishi una fedha au huna fedha wewe ni mtu wa kipekee.
Endelea kuweka juhudi kwenye kile unachofanya na usikubali jamii ikuyumbishe na vipimo vyao visivyo na maana.
Wewe ni wewe, ni wa kipekee, ni bora na una mengi yaliyo mbele yako. Yaendee.
Makirita Amani,
www.amkamtanzania.com

UKURASA WA 185; Bila Kuwajua Watu Hawa Watatu Na Kumalizana Nao, Sahau Kuhusu Mafanikio.

Kuna watu watatu ambao kwa wewe kujua au kutokujua wamekuwa wanakuzuia kufikia mafanikio.
Sio kwamba wao wanakuja na kukuzuia wewe kufikia mafanikio, ila kwa sababu yao wewe mwenyewe umeshindwa kufikia mafanikio kwenye maisha yako.
Aina ya kwanza ya watu hawa ni watu ambao unataka kuwalinda. Kuna watu ambao wewe unataka kuwalinda na hivyo unajizuia kufikia mafanikio ili uendelee kuwalinda. Kuna baadhi ya watu wanaogopa kufikia mafanikio kwa sababu wanataka kuendelea kuwa na watu wanaowazunguka. Kuna wafanyakazi ambao wanaogopa kuonesha ubora wao kwenye kazi zao kwa sababu wanaogopwa kuchukiwa na wenzao au kuonekana ni hatari kwa mabosi zao.
SOMA; Wajue Watu Hawa na Waepuke Kwenye Maisha Yako.
Aina ya pili ni watu ambao unajaribu kuwaadhibu. Kuna watu ambao unaweza kuwa unataka kuwaadhibu na hivyo ukajizuia wewe kufikia mafanikio. Labda wazazi wako hawakukupatia kile ulichofikiri kingekuwa bora kwako. Na hivyo unataka uwaoneshe kwamba walikosea na hivyo wewe huwezi kufikia mafanikio kama ya wengine.... kwa sababu ya kutojali kwao.
Aina ya tatu ni watu ambao unataka kuwafurahisha. Hawa ni watu ambao unataka kuwafurahisha ili waendelee kukuona kama wanavyopenda kukuona na hivyo kujizuia kufikia mafanikio. Kuna watu ambao wanalazimika kuvaa mavazi ya bei ghali, kuendesha magari ya bei ghali na hata kuishi maeneo fulani ili tu waonekane.
Wajue watu hawa watatu kwenye maisha yako na malizana nao, hakikisha unaishi maisha uliyochagua wewe mwenyewe, yatakayokufikisha kwenye mafanikio unayotaka na sio kuwalinda watu, kuwaadhibu au kuwafurahisha.
TAMKO LA LEO;
Nimeamua sasa kwamba sitaki tena kuwalinda watu, kuwaadhibu au kuwafurahisha. Nahitaji kuishi maisha ambayo yatanipa furaha na kunifikisha kwenye mafanikio na sio maisha ambayo yatanirudisha nyuma. Nitaweka juhudi na maarifa ili niweze kuwa bora zaidi ya nilivyo sasa.
Tukutane kwenye ukurasa wa kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Friday, July 3, 2015

UKURASA WA 184; Ni Ruhusa Kwako Kubadili Mawazo.

Kwa mfano umeshakubaliana na mtu mtafanya kitu fulani halafu dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo, sitafanya tena kama nilivyokuambia. Unajisikiaje? Unachukuliaje hali kama hiyo?
Labda ni biashara na umeshakubaliana na mteja ila baadae anakuambia nimebadili mawazo. Au ni kwenye ajira na umeshakubaliana kitu fulani na mwajiri wako, umeshajiandaa kabisa na anakuambia nimebadili mawazo, hutafanya tena hivyo. Au ni kwenye maisha yako ya kawaida, ulipanga muoane na mtu na dakika za mwisho anakuambia nimebadili mawazo? Au umeshaona na mtu na kati kati ya safari anakuambia nimebadili mawazo?
Najua kama wewe ndio umeambiwa hivi unaweza kujisikia vibaya sana. Unaweza kuona aliyebadili mawazo hafai na ameharibu maisha yako. Lakini ukweli ni kwamba yeye ametumia haki yake ya msingi, kuruhusu mawazo yake yamchagulie kile ambacho anaona ni bora kwake. Hakuna jinsi unaweza kuzuia hilo.
SOMA; Kabla Hujakubali Kila Unachoambiwa, Kumbuka Jambo Hili Moja Muhimu Sana.
Badala ya wewe kulalamika kwamba kwa nini hakukwambia mapema au kwa nini alikubali mwanzoni, furahi kwamba umejua mapema kabla hata hujapoteza muda mwingi. Shukuru kwamba umejua ni mtu wa aina gani na jifunze wakati mwingine kuangalia vitu muhimu kabla hujaingia kwenye makubaliano na mtu ambayo ni muhimu.
Jipe ruhusa ya kubadili mawazo, wape wengine ruhusa ya kubadili mawazo na usitake kuishi maisha ya kufungwa au kuwafunga wengine kwa sababu tu wanaogopa kubadili mawazo. Maisha yanapaswa kufurahiwa na sio kuishi kwa ajili ya kuwaridhisha wengine.
TAMKO LA LEO;
Najua nina ruhusa ya kubadili mawazo hata kama nilishakubaliana na mtu. Najua pia kwamba watu wana ruhusa ya kubadili mawazo yao hata kama walishaniahidi kitu. Naheshimu uhuru wangu na wa kila mtu na ni kwa uhuru huu ndio naweza kuishi maisha ninayoyafurahia na yenye faida kwa wengine pia.
Tukutane kwenye ukurasa wa 185 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Thursday, July 2, 2015

UKURASA WA 183; Hakuna Anayekuchukia Wewe, Bali Wanahamisha Chuki Zao Kutoka Hapa.

Leo naomba tujadili kidogo kuhusu mtu kumchukia mwingine.
Labda tuseme wewe kuna mtu anakuchukia, na amekuwa akikuonesha wazi wazi kwamba anakuchukia. Na hapa wewe huna tatizo lolote na mtu huyu. Unajaribu kuishi maisha yako bila hata ya kuingilia maslahi yao wala kuwavurugia chochote ambacho ni chao, lakini mtu anachagua tu kukuchukia.
Unajisikiaje katika hali kama hii? Unaumia kwa sababu ulitegemewa mtu ambaye ni wa karibu kwako awe pamoja na wewe badala yake anakuchukia? Unajaribu kumbadili mtu labda akupende?
Leo nataka nikupe sababu kwa nini mtu anaweza kukuchukia na njia bora ya kuondokana na chuki hiyo.
Kwanza kabisa mtu anapokuchukia sio kwamba anakuchukia wewe, ila anajichukia yeye binafsi. Ni hivyo tu. Mtu kuna kitu ambacho kinamsumbua kwenye maisha yake na hataki kukikubali, hivyo anayachukia maisha yake, kwa sababu hataki kukubali hilo pia anatafuta mtu wa kumchukia ili angalau aone tatizo sio lake. Si unajua tabia za wakwepa majukumu?
Hivyo atajipa kila sababu kwa nini anakuchukia wewe, lakini wewe huna tatizo lolote na yeye kukuchukia, hakuna chochote ambacho umemharibia. Labda umeamua tu kubadili maisha yako na kwa kuwa huyo anayekuchukia hawezi kubadilika basi anakuchukia. Kwa mfano ulikuwa na marafiki wa karibu kila siku mnakunywa pamoja, wewe ukakaa chini na kuona kunywa kwenu hakuna faida yoyote, hivyo ukaamua kuacha utaratibu huu wa kukutana baa kila siku na ukaanza kujifunza na kujishughulisha na vitu vya pembeni(fanya hivi kama bado una utaratibu wa kuhudhuria vikao vya baa kila siku). Unafikiri ni nini kitatokea kwa marafiki zako hao? Watakuchukia. Sasa hebu jiulize wanakuchukia kwa sababu wewe umeamua kuacha kukaa vikao hivyo kila siku? Hapana, wanakuchukia kwa sababu wewe unaanza kuwa bora kuliko wao. Kwa mfano ingetokea huna tena kazi na hivyo huna fedha ya kwenda baa kila siku unafikiri wangekuchukia? Hawawezi kukuchukia, watakuonea huruma tu na wataendelea na utaratibu wao.
Hivyo kama kuna mtu yeyote ambaye anakuchukia, wala usijiumize kichwa ufanye nini ili aache kukuchukia, endelea kufanya unachofanya na mwache ajiue mwenyewe na chuki zake. Maisha ni mafupi sana mpaka uanze kupata muda wa kumfurahisha kila mtu.
Usikubali uhusiano wowote wa kindugu au kirafiki uwe kikwazo kwako kuishi maisha unayotaka kuishi wewe, kama huvunji sheria. Hata kama kuna atakayekuchukia hawezi kukuchukia zaidi ya miaka 100 ijayo, kwa sababu wote mtakuwa mmekufa na hakuna atakayekuja kukukumbusha kwamba nilikuchukia sana duniani, kama mtakutana peponi.
SOMA; Hiki Ndio Kitakachotokea Miaka 100 Ijayo..
Maisha ni yako chaguo ni lako, kama kuna mtu anakuchukia muonee huruma na achana naye, wala hata usimfikirie, wewe endelea kuweka juhudi kwenye kile unachofanya na unachotaka kuwa bora.
TAMKO LA LEO;
Najua kwamba mtu yeyote anayenichukia sio kwa sababu ananichukia kweli, ila ni kwa sababu anajichukia yeye mwenyewe. Mimi sina muda wa kuanza kufikiria kuhusu anayenichukia, ni bora nikatumia muda huo vizuri kujiendeleza kuwa bora zaidi kwenye hiki ninachofanya.
Tukutane kwenye ukurasa wa 184 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.

Wednesday, July 1, 2015

UKURASA WA 182; Urahisi Wa Kutengeneza Tabia Mbaya Na Ugumu Wa Kuishi Nazo.

Kuna jambo moja muhimu sana kwenye maisha ambalo unatakiwa kuwa unalijua. Na sio kulijua tu bali kulifanyia kazi kila siku maana kwa jambo hili moja ndio watu wanafanikiwa au wanashindwa.
Jambo hilo ni kwmaba, tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza ila ni ngumu sana kuishi nazo. Na kwa upande wa pili, tabia nzuri ni ngumu sana kutengeneza ila ni rahisi sana kuishi nazo. Hivyo ni wewe kuchagua kuwa tayari kufanya kipi ili uweze kuishije baadae.
Urahisi wa kutengeneza tabia mbaya.
Tabia mbaya ni rahisi sana kutengeneza, kwa mfano ulevi, ni rahisi sana kuwa mlevi, anza kunywa pombe kila siku na kunywa nyingi uwezavyo, hata hivyo unasikia raha, hivyo ni rahisi kutengeneza. Ila sasa maisha ya ulevi ni magumu sana, ni vigumu sana kuweza kufurahia maisha kama tayari wewe ni mlevi, utajikuta maisha yako yametawaliwa na ulevi na unajiona kama huwezi kutoka tena huko.
Tabia zote mbaya, iwe ni uvivu, wizi, uongo, kula hovyo zote ni rahisi sana kutekeleza. Ila kuishi nazo baada ya kuwa zimejijenga ni vigumu sana.
SOMA; Kama Unataka Kumaliza Matatizo Yako Ya Fedha Fanya Kitu Hiki Kimoja.
Ugumu wa kutengeneza tabia nzuri.
Kwa upande wa pili, tabia nzuri ni vigumu sana kuzitengeneza lakini ukishakuwa nazo ni rahisi sana kuishi nazo. Kwa mfano tabia ya kujiwekea akiba, ni vigumu sana mwanzoni, inabidi ujinyime inabidi uonekane huendi na wakati na wakati mwingine utahitaji kuzishinda tamaa zako. Ila unapokuwa na tabia hii ni rahisi na vizuri sana kuishi nayo kwa sababu unajua kuna akiba ambayo inaendelea kukua na hivyo kuvutiwa kuweka zaidi.
Unahitaji nguvu ya ziada ili kuweza kufikia mafanikio, ingekuwa rahisi kila mtu angekuwa nayo. Sio rahisi na ndio maana kuna wakati utaona kama unajitesa, endelea hivyo hivyo na mambo yatakuwa mazuri sana.
TAMKO LA LEO;
Najua nina machanguo mawili, nipate raha ya muda mfupi sasa halafu niteseke kwa muda mrefu au nipate shida ya muda mfupi sasa na kuishi kwa raha muda mrefu. Mimi nimechagua kuteseka kwa muda mfupi sasa ili niishi kwa raha muda mrefu ujao. Nitatengeneza tabia ambazo ni nzuri kwa sasa, ambazo ni ngumu kutengeneza lakini najua baadae nitafurahia kuishi nazo.
Tukutane kwenye ukurasa wa 183 kesho, Like page yangu ya Coach Makirita Amani uendelee kupata mambo mazuri ya kuboresha kazi yako, biashara yako na maisha yako kwa ujumla.
Kuhakikisha hukosi mfululizo huu wa makala za KURASA 365 bonyeza hapa na uweke email.
Kusoma makala zilizopita za KURASA 365 ZA MWAKA 2015 bonyeza hayo maandishi.
Pia washirikishe wengine makala hii kwa kubonyeza vitufe vya facebook au twitter hapo chini. Pia watumie makala hii nzuri kwa njia ya email.
Kwa lolote andika email kwenda makirita@kisimachamaarifa.co.tz
Kujifunza zaidi ili kuweza kufikia mafanikio makubwa jiunge na KISIMA CHA MAARIFA bonyeza hayo maandishi kupata utaratibu.
TUPO PAMOJA.