Jiunge Hapa Kupata Makala Mpya Inapotoka!

We'll not spam mate! We promise.

Sunday, March 30, 2014

Huhitaji Cheo Ili Kuwa Kiongozi.

Ni wakati gani unafikiri unahitaji kuanza kuonesha tabia za uongozi? Unapoambiwa umepewa nafasi ya kuwa meneja? Au unapoteuliwa kuwa mwakilishi wa watu au msimamizi wa sekta fulani? Yote hayo yanaweza kukupa nguvu ya uongozi ila hayawezi kukufanya kiongozi kama hukuwa kiongozi kabla. Na vibaya zaidi ni kwamba nguvu hii ya uongozi huisha mara moja pale nafasi hiyo inapoondoka.

Huhitaji cheo ili kuwa kiongozi, unahitaji kutumia uwezo wako na vipaji vyako katika maisha yako ili kuwa kiongozi. Unahitaji kutimiza wajibu wako na kufanya zaidi ya unavyotegemewa kwenye kazi, biashara na hata kwenye maisha yako. Kwa kufanya hivi ndio utajitengeneza kama kiongozi ambapo wengine watafurahia kukufuata.

Ili kuwa kiongozi huhitaji cheo, unahitaji kufanya maamuzi ya kuwa kiongozi kisha kuanza kuongoza. Kila mtu anayo nafasi ya kuwa kiongozi ila wachache ndio wanaochagua kuwa viongozi. Kama kila mtu angefagia mtaa wake dunia nzima ingekuwa safi sana. Ila kwa kuwa wengi hawafanyi wanayopaswa kufanya tunaishia kuwa na matatizo mengi duniani.

Nguvu nne za uongozi ambazo hazihitaji cheo.

Kama unajiuliza unawezaje kuwa kiongozi bila ya kuwa na cheo soma nguvu hizi nne za uongozi ambazo tayari unazo bila hata ya kuwa na cheo. Kwa kufanya mambo haya manne ambayo hayahitaji cheo kutakutengeneza kuwa kiongozi mzuri kwenye maisha yako.

1. Una uwezo wa kwenda kwenye shughuli zako, iwe kazi au biashara na kufanya kazi kwa moyo mmoja na ubunifu wa kipekee kitu ambacho kitakufanya utoe majibu mazuri sana. Una uwezo wa kuamua kuwa bora siku ya leo zaidi ya ulivyokuwa bora siku ya jana na huhitaji kuwa na cheo ili kufanya hivyo. Kwa kutimiza wajibu wako na kuongeza ubora kila siku unakuwa kiongozi ambaye wengine watapenda kukufuata.

2. Leo hii unao uwezo wa kushawishi na kuchochea watu wanaokuzunguka ili wafanye mambo ambayo yatawasaidia kuboresha kazi zao na maisha yao kwa ujumla. Huhitaji kuwa na cheo ndio uweze kumshawishi mtu kwamba akifanya juhudi kwenye kazi zake ataboresha maisha yake. Unahitaji kumuonesha picha kubwa na kumchochea aweze kuifikia, kama na wewe unaelekea kuifikia au umeshaifikia.

3. Unao uwezo wa kuleta mageuzi chanya kwenye mazingira hasi. Hata mazingira ya kazi au maisha yawe magumu kiasi gani unao uwezo wa kubadili mtazamo wako na wa wanaokuzunguka kuhusu mazingira hayo. Huhitaji cheo kuweza kuangalia faida unayoweza kupata kwenye mazingira fulani zaidi ya kuangalia hasara tu. Pia huhitaji cheo kubadili mazingira mambovu ambayo yanakukandamiza wewe au wale wanaokuzunguka.

4. Una uwezo wa kuwa mwema kwa wale wanaokuzunguka kwenye shughuli zako na maisha yako kwa ujumla. Huhitaji cheo ndio uweze kuwaheshimu, kuwajali na kuwapenda watu wanaokuzunguka kwenye maisha yako. Kwa kufanya hivyo utawafanya watu hawa kufurahia kuwa karibu na wewe na kuona maisha yao yana thamani kubwa. Mtu anayeona thamani kubwa ya maisha yake anaweza kufanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yake na shughuli zake.

Mambo haya manne hayahitaji cheo ndio uweze kuyafanya. Hebu anza kuyafanya mara moja kwenye maisha yako na utaona mabadiliko makubwa. Kumbuka wewe ni kiongozi hata kama huna cheo.

Huhitaji Cheo Ili Kuwa Kiongozi.

Ni wakati gani unafikiri unahitaji kuanza kuonesha tabia za uongozi? Unapoambiwa umepewa nafasi ya kuwa meneja? Au unapoteuliwa kuwa mwakilishi wa watu au msimamizi wa sekta fulani? Yote hayo yanaweza kukupa nguvu ya uongozi ila hayawezi kukufanya kiongozi kama hukuwa kiongozi kabla. Na vibaya zaidi ni kwamba nguvu hii ya uongozi huisha mara moja pale nafasi hiyo inapoondoka.

Huhitaji cheo ili kuwa kiongozi, unahitaji kutumia uwezo wako na vipaji vyako katika maisha yako ili kuwa kiongozi. Unahitaji kutimiza wajibu wako na kufanya zaidi ya unavyotegemewa kwenye kazi, biashara na hata kwenye maisha yako. Kwa kufanya hivi ndio utajitengeneza kama kiongozi ambapo wengine watafurahia kukufuata.

Ili kuwa kiongozi huhitaji cheo, unahitaji kufanya maamuzi ya kuwa kiongozi kisha kuanza kuongoza. Kila mtu anayo nafasi ya kuwa kiongozi ila wachache ndio wanaochagua kuwa viongozi. Kama kila mtu angefagia mtaa wake dunia nzima ingekuwa safi sana. Ila kwa kuwa wengi hawafanyi wanayopaswa kufanya tunaishia kuwa na matatizo mengi duniani.

Nguvu nne za uongozi ambazo hazihitaji cheo.

Kama unajiuliza unawezaje kuwa kiongozi bila ya kuwa na cheo soma nguvu hizi nne za uongozi ambazo tayari unazo bila hata ya kuwa na cheo. Kwa kufanya mambo haya manne ambayo hayahitaji cheo kutakutengeneza kuwa kiongozi mzuri kwenye maisha yako.

1. Una uwezo wa kwenda kwenye shughuli zako, iwe kazi au biashara na kufanya kazi kwa moyo mmoja na ubunifu wa kipekee kitu ambacho kitakufanya utoe majibu mazuri sana. Una uwezo wa kuamua kuwa bora siku ya leo zaidi ya ulivyokuwa bora siku ya jana na huhitaji kuwa na cheo ili kufanya hivyo. Kwa kutimiza wajibu wako na kuongeza ubora kila siku unakuwa kiongozi ambaye wengine watapenda kukufuata.

2. Leo hii unao uwezo wa kushawishi na kuchochea watu wanaokuzunguka ili wafanye mambo ambayo yatawasaidia kuboresha kazi zao na maisha yao kwa ujumla. Huhitaji kuwa na cheo ndio uweze kumshawishi mtu kwamba akifanya juhudi kwenye kazi zake ataboresha maisha yake. Unahitaji kumuonesha picha kubwa na kumchochea aweze kuifikia, kama na wewe unaelekea kuifikia au umeshaifikia.

3. Unao uwezo wa kuleta mageuzi chanya kwenye mazingira hasi. Hata mazingira ya kazi au maisha yawe magumu kiasi gani unao uwezo wa kubadili mtazamo wako na wa wanaokuzunguka kuhusu mazingira hayo. Huhitaji cheo kuweza kuangalia faida unayoweza kupata kwenye mazingira fulani zaidi ya kuangalia hasara tu. Pia huhitaji cheo kubadili mazingira mambovu ambayo yanakukandamiza wewe au wale wanaokuzunguka.

4. Una uwezo wa kuwa mwema kwa wale wanaokuzunguka kwenye shughuli zako na maisha yako kwa ujumla. Huhitaji cheo ndio uweze kuwaheshimu, kuwajali na kuwapenda watu wanaokuzunguka kwenye maisha yako. Kwa kufanya hivyo utawafanya watu hawa kufurahia kuwa karibu na wewe na kuona maisha yao yana thamani kubwa. Mtu anayeona thamani kubwa ya maisha yake anaweza kufanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yake na shughuli zake.

Mambo haya manne hayahitaji cheo ndio uweze kuyafanya. Hebu anza kuyafanya mara moja kwenye maisha yako na utaona mabadiliko makubwa. Kumbuka wewe ni kiongozi hata kama huna cheo.

Sunday, March 23, 2014

Je Wewe ni Kiongozi au Mfuasi?

Duniani tuna makundi mawili ya watu, kuna kundi la kwanza ambapo watu hawa ni viongozi na kundi la pili ambapo watu hao ni wafuasi. Mara nyingi wanaofanikiwa sana na kufikia malengo waliyojiwekea ni wale waliopo kwenye kundi la viongozi.

Viongozi huanzisha na wafuasi hufuata au kuiga, hii ndio inawafanya viongozi wanafanikiwa sana kwenye mipango yao. Hakuna mtu anayepanga huyu awe kuingozi na huyu awe mfuasi. Ni mfumo wako wa maisha na tabia zako zitakuweka kwenye kundi la viongozi au kundi la wafuasi.

Je unajua wewe upo kwenye kundi gani? Unaweza kujiita kiongozi kwa kuwa umepewa nafasi ya kuwasimamia watu, ila kama huna sifa za uongozi basi wewe sio kiongozi bali ni msimamizi tu. Hapa tutaangalia tofauti tano za kitabia kati ya viongozi na wafuasi. Kwa kuzijua tofauti hizi za kitabia itakufanya ujue upo kundi gani na pia uweze kuchukua hatua.

1. Uanzilishi.

Viongozi huanzisha mambo kutokana na malengo na mipango yao kwenye maisha na kazi wanazofanya. Hujua ni nini watafanya kwenye kila hatua na mwishowe hufanikiwa.

Wafuasi hufanya mambo yaliyoanzishwa na watu wengine. Hata siku moja hawana udhubutu wa kuanzisha kitu chao wenyewe na kukisimamia mpaka kitoe majibu wanayotarajia. Wafuasi huishia kuiga mambo yanayofanywa na watu wengine na inakuwa rahisi kwao kushindwa.

2. Mawasiliano.

Viongozi huanzisha mawasiliano na watu wengine. Mara nyingi huwa wa kwanza kuwatafuta watu wanaowahitaji ili kukamilisha jambo fulani. Pia huwa wa kwanza kuwapigia wengine simu katika kuwasiliana.

Wafuasi huwa ni wasikilizaji kwenye mawasiliano. Ni wazuri kupokea taarifa walizopewa na kwenda kuzifanyia kazi. Kama wasipotafutwa hawajisumbui kutafuta mtu, hukaa na kusubiri. Wafusi husubiri simu iite wapewe taarifa au maagizo.

3. Matumizi ya muda.

Viongozi hutumia sehemu kubwa ya muda wao kupanga mipango mbalimbali. Pia hutumia muda huo kufikiri matatizo yanayoweza kutokea na kufikiri njia za kukabiliana nayo. Kwa njia hii viongozi wanaongeza uwezo wao wa kutatua matatizo.

Wafuasi hutumia muda wao mwingi kuishi maisha yao ya kawaida na hawana muda mwingi wa kuweka mipango mikubwa. Wafuasi ni wazuri kustushwa pale tatizo linapotokea na huwa wa kwanza kusumbuliwa na tatizo hilo. Kibaya zaidi wanakuwa hawana uwezo wa kutatua tatizo hilo zaidi ya kupata msongo wa mawazo.

4. Uwekezaji wa muda.

Viongozi huwekeza muda wao kwa watu wengine. Hutumia muda wao mwingi kujenga na kufundisha watu kuwa viongozi. Pia hutumia muda kuwapa wengine uwezo wa kuweka mipango na kutatua matatizo.

Wafuasi hawawekezi muda wao bali wanautumia na watu wengine. Wafuasi wanapokuwa na muda wa ziada huutumia kufanya mambo ambayo hayana msaada wowote kwao kimaisha au kikazi. Ni watumiaji wa muda hovyo.

5. Upangaji wa ratiba.

Viongozi wanapanga ratiba zao kulingana na vipaumbele vyao. Hupanga ratiba kutokana na malengo na mipango yao na huweka mbele vipaumbele vyao.

Wafuasi hupanga ratiba zao kulingana na maombi na maagizo. Ratiba za wafuasi zimejaa vitu ambavyo ni maombi ya watu wengine au ni maagizo ya watu wengine. Hawawezi kuweka vipaumbele vyao wenyewe kwenye ratiba zao.

Hizo ndio tofauti tano kati ya viongozi na wafuasi kitabia. Hakuna mtu anayekupangia tabia hizi bali unaziendeleza mwenyewe.

Kama kwa tabia hizo hapo chini unajiona uko upande wa wafuasi usife moyo. Kama tulivyosema, viongozi pia hutengenezwa, hivyo unaweza kujitengeneza kuwa kiongozi mzuri na ukafanikiwa kwenye mipango yako ya maisha. Jiunge na mtandao huu kwa kuweka email yako hapo juu kwenye blog ili kupata mafundisho haya ya uongozi moja kwa moja.

Nakutakia kila la kheri kwenye harakati zako za maisha, kumbuka viongozi ndio wanaofanikiwa kwenye nyanja yoyote.

Je Wewe ni Kiongozi au Mfuasi?

Duniani tuna makundi mawili ya watu, kuna kundi la kwanza ambapo watu hawa ni viongozi na kundi la pili ambapo watu hao ni wafuasi. Mara nyingi wanaofanikiwa sana na kufikia malengo waliyojiwekea ni wale waliopo kwenye kundi la viongozi.

Viongozi huanzisha na wafuasi hufuata au kuiga, hii ndio inawafanya viongozi wanafanikiwa sana kwenye mipango yao. Hakuna mtu anayepanga huyu awe kuingozi na huyu awe mfuasi. Ni mfumo wako wa maisha na tabia zako zitakuweka kwenye kundi la viongozi au kundi la wafuasi.

Je unajua wewe upo kwenye kundi gani? Unaweza kujiita kiongozi kwa kuwa umepewa nafasi ya kuwasimamia watu, ila kama huna sifa za uongozi basi wewe sio kiongozi bali ni msimamizi tu. Hapa tutaangalia tofauti tano za kitabia kati ya viongozi na wafuasi. Kwa kuzijua tofauti hizi za kitabia itakufanya ujue upo kundi gani na pia uweze kuchukua hatua.

1. Uanzilishi.

Viongozi huanzisha mambo kutokana na malengo na mipango yao kwenye maisha na kazi wanazofanya. Hujua ni nini watafanya kwenye kila hatua na mwishowe hufanikiwa.

Wafuasi hufanya mambo yaliyoanzishwa na watu wengine. Hata siku moja hawana udhubutu wa kuanzisha kitu chao wenyewe na kukisimamia mpaka kitoe majibu wanayotarajia. Wafuasi huishia kuiga mambo yanayofanywa na watu wengine na inakuwa rahisi kwao kushindwa.

2. Mawasiliano.

Viongozi huanzisha mawasiliano na watu wengine. Mara nyingi huwa wa kwanza kuwatafuta watu wanaowahitaji ili kukamilisha jambo fulani. Pia huwa wa kwanza kuwapigia wengine simu katika kuwasiliana.

Wafuasi huwa ni wasikilizaji kwenye mawasiliano. Ni wazuri kupokea taarifa walizopewa na kwenda kuzifanyia kazi. Kama wasipotafutwa hawajisumbui kutafuta mtu, hukaa na kusubiri. Wafusi husubiri simu iite wapewe taarifa au maagizo.

3. Matumizi ya muda.

Viongozi hutumia sehemu kubwa ya muda wao kupanga mipango mbalimbali. Pia hutumia muda huo kufikiri matatizo yanayoweza kutokea na kufikiri njia za kukabiliana nayo. Kwa njia hii viongozi wanaongeza uwezo wao wa kutatua matatizo.

Wafuasi hutumia muda wao mwingi kuishi maisha yao ya kawaida na hawana muda mwingi wa kuweka mipango mikubwa. Wafuasi ni wazuri kustushwa pale tatizo linapotokea na huwa wa kwanza kusumbuliwa na tatizo hilo. Kibaya zaidi wanakuwa hawana uwezo wa kutatua tatizo hilo zaidi ya kupata msongo wa mawazo.

4. Uwekezaji wa muda.

Viongozi huwekeza muda wao kwa watu wengine. Hutumia muda wao mwingi kujenga na kufundisha watu kuwa viongozi. Pia hutumia muda kuwapa wengine uwezo wa kuweka mipango na kutatua matatizo.

Wafuasi hawawekezi muda wao bali wanautumia na watu wengine. Wafuasi wanapokuwa na muda wa ziada huutumia kufanya mambo ambayo hayana msaada wowote kwao kimaisha au kikazi. Ni watumiaji wa muda hovyo.

5. Upangaji wa ratiba.

Viongozi wanapanga ratiba zao kulingana na vipaumbele vyao. Hupanga ratiba kutokana na malengo na mipango yao na huweka mbele vipaumbele vyao.

Wafuasi hupanga ratiba zao kulingana na maombi na maagizo. Ratiba za wafuasi zimejaa vitu ambavyo ni maombi ya watu wengine au ni maagizo ya watu wengine. Hawawezi kuweka vipaumbele vyao wenyewe kwenye ratiba zao.

Hizo ndio tofauti tano kati ya viongozi na wafuasi kitabia. Hakuna mtu anayekupangia tabia hizi bali unaziendeleza mwenyewe.

Kama kwa tabia hizo hapo chini unajiona uko upande wa wafuasi usife moyo. Kama tulivyosema, viongozi pia hutengenezwa, hivyo unaweza kujitengeneza kuwa kiongozi mzuri na ukafanikiwa kwenye mipango yako ya maisha. Jiunge na mtandao huu kwa kuweka email yako hapo juu kwenye blog ili kupata mafundisho haya ya uongozi moja kwa moja.

Nakutakia kila la kheri kwenye harakati zako za maisha, kumbuka viongozi ndio wanaofanikiwa kwenye nyanja yoyote.

Sunday, March 16, 2014

Sifa Moja Muhimu Ambayo Kila Kiongozi Mkubwa Anayo.

Kwenye makala zilizopita tuliona ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa kiongozi kwenye maisha yake na shughuli anazofanya. Pia tuliona kwamba kila mmoja wetu anaweza kuwa kiongozi kama ataamua, iwe kwa kuendeleza sifa za uongozi zilizopo ndani yake au kwa kujifunza sifa za uongozi.

Leo tutaangalia sifa moja muhimu ambayo kila kiongozi mkubwa anayo na imechangia sana kwenye mafanikio yao kiuongozi. Ninaposema viongozi wakubwa simaanishi viongozi walioshika nafasi kubwa bali viongozi ambao wamefanya mambo makubwa ambayo yameleta mabadiliko kwa watu wengi na dunia kwa ujumla. Viongozi kama Nyerere, Mandela na hata viongozi wakubwa kwenye nyanja za biashara na kazi wameweza kufikia mafanikio makubwa kutokana na sifa hii moja.

Kwa kuwa na wewe unataka kuwa kiongozi wa maisha yako, kiongozi kwenye familia yako, kiongozi kwenye kazi au biashara zako na hata kiongozi wa kuwakilisha watu ni vyema ukaijua sifa hii na kuanza kujifunza au kuiendeleza ili uweze kufikia malengo yako. Sifa hii moja sio kwamba ndio inakutosha kuwa kiongozi ila kwa kuwa na sifa hii unaweza kuziendeleza sifa nyingine za uongozi. Kwa kukosa sifa hii ni vigumu kuweza kuzitumia sifa nyingine za uongozi ulizonazo.

Sifa muhimu ya uongozi ninayozungumzia hapa ni ujasiri. Ujasiri ni sifa ambayo imewawezesha viongozi wakubwa kufanya mambo makubwa kwenye uongozi wao. Kukosa ujasiri ndio kumefanya watu wengi washindwe kwenye uongozi.

Kuweza kusimamia kile unachoamini ni sahihi hata kama watu wengi wanakupinga kunahitaji ujasiri wa hali ya juu. Kama ilivyotokea kwa Mandela, alikuwa na ujasiri wa kuweza kusimama na kupinga ubaguzi hata baada ya kufungwa jela miaka 27. Wafanyabiashara wakubwa na waliofanikiwa sana mwanzoni walipingwa, kukatishwa tamaa na hata kuchekwa kwamba mawazo yao ya biashara hayawezi kufanikiwa. Ila kutokana na ujasiri waliweza kuendelea na misimamo yao na baadae ikawa historia kubwa ya mabadiliko.

Inahitaji ujasiri wa hali ya juu kuenda tofauti na watu wengine ili kufuata ndoto zako. Inahitaji ujasiri mkubwa kuweza kufanya kazi na watu ambao wana misimamo tofauti na wewe na mkaweza kuelewana. Inahitaji ujasiri mkubwa kufanya na kusimamia maamuzi magumu ambayo wengi hawayafurahii ila yana manufaa kwao baadae. Yote haya yameweza kutengeneza viongozi wakubwa sana na walioshindwa ujasiri wa kufanya mambo haya wameishia kuwa kawaida tu.

Kutokukata tamaa wakati umeshindwa, kuweza kusimama baada ya kupata hasara kubwa na kutokuwasikiliza wanaokukatisha tamaa ni muhimu sana kwenye mafanikio ya kibiashara na kikazi. Watu wenye ujasiri wanaweza kuvuka changamoto hizo na kuwa viongozi wa mfano kwenye kazi na biashara zao.

Unaweza kujifunza ujasiri?

Huenda mpaka kufika hapa umeshaona kwamba ujasiri kwako ni kitu kigumu sana hivyo njia yako ya kuwa kiongozi imeshakutana na kizuizi kikubwa. Habari njema kwako ni kwamba unaweza kujifunza ujasiri. Unawezaje kujifunza ujasiri?

Ili uwe na ujasiri kitu cha kwanza kabisa ni lazima ujue ni nini unasimamia. Kama huna kitu unachosimamia utakubaliana na kila kitu na kama unakubaliana na kila kitu wewe sio jasiri na huwezi kupata mafanikio makubwa kwenye jambo lolote unalofanya, hilo halina ubishi. Jua ni kitu gani unasimamia, jua ni kwa nini unasimamia na jua ni nini unategemea kutoka kwenye huo msimamo wako. Hii ni kwenye maisha, familia, kazi, biashara na hata uongozi wa wananchi.

Baada ya kujua unachosimamia izidi hofu. Hofu na woga ndio vitu vinavyoondoa ujasiri kwa watu wengi. Ukiweza kuishinda hofu utaweza kukamilisha mambo mengi sana kwenye maisha yako na kuacha alama. Kama utakubaliana na hofu na kuacha kufanya mipango yako hakuna kitu kikubwa utakachofanya. Watu wenye ujasiri na waliofanikiwa sio kwamba hawana hofu ila wamechagua kuzishinda hofu zao. Chagua na wewe kushinda hofu zako na kufanya yale unayojua ni sahihi na yatawasaidia watu wengine.

Kuna faida kubwa ya kuwa na ujasiri kwenye maisha yako. Watu wenye ujasiri huwavutia watu wengine kuwa karibu nao na hivyo kuangaliwa kama kiongozi. Watu wenye ujasiri hufanya mambo makubwa na kuwafaidisha wengine hivyo wengine kutaka kufanya kama wao. Hivi ndivyo ujasiri unajenga viongozi wakubwa. Na kwa kuwa wewe unataka kuwa kiongozi mkubwa anza kwa kujenga ujasiri wako.

Kwanzia wiki ijayo tutazijadili sifa 21 za kiongozi kutoka kwenye kitabu  The 21 Indispensable Qualities of a Leader. Tutajadili sifa tatu tatu mpaka zitakapoisha. Kuhakikisha hukosi makala hizi nzuri za uongozi weka email yako hapo juu kwenye blog sehemu iliyoandikwa jiunge hapa kupata makala mpya inapotoka

Pia usiache kupitia blog hii kila jumapili ili kujifunza mengi kuhusiana na uongozi. Washirikishe marafiki zako nao ili wajifunze masomo haya ya uongozi. Pia weka maoni yako hapo chini kuhusiana na mambo ya uongozi.

Sifa Moja Muhimu Ambayo Kila Kiongozi Mkubwa Anayo.

Kwenye makala zilizopita tuliona ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuwa kiongozi kwenye maisha yake na shughuli anazofanya. Pia tuliona kwamba kila mmoja wetu anaweza kuwa kiongozi kama ataamua, iwe kwa kuendeleza sifa za uongozi zilizopo ndani yake au kwa kujifunza sifa za uongozi.

Leo tutaangalia sifa moja muhimu ambayo kila kiongozi mkubwa anayo na imechangia sana kwenye mafanikio yao kiuongozi. Ninaposema viongozi wakubwa simaanishi viongozi walioshika nafasi kubwa bali viongozi ambao wamefanya mambo makubwa ambayo yameleta mabadiliko kwa watu wengi na dunia kwa ujumla. Viongozi kama Nyerere, Mandela na hata viongozi wakubwa kwenye nyanja za biashara na kazi wameweza kufikia mafanikio makubwa kutokana na sifa hii moja.

Kwa kuwa na wewe unataka kuwa kiongozi wa maisha yako, kiongozi kwenye familia yako, kiongozi kwenye kazi au biashara zako na hata kiongozi wa kuwakilisha watu ni vyema ukaijua sifa hii na kuanza kujifunza au kuiendeleza ili uweze kufikia malengo yako. Sifa hii moja sio kwamba ndio inakutosha kuwa kiongozi ila kwa kuwa na sifa hii unaweza kuziendeleza sifa nyingine za uongozi. Kwa kukosa sifa hii ni vigumu kuweza kuzitumia sifa nyingine za uongozi ulizonazo.

Sifa muhimu ya uongozi ninayozungumzia hapa ni ujasiri. Ujasiri ni sifa ambayo imewawezesha viongozi wakubwa kufanya mambo makubwa kwenye uongozi wao. Kukosa ujasiri ndio kumefanya watu wengi washindwe kwenye uongozi.

Kuweza kusimamia kile unachoamini ni sahihi hata kama watu wengi wanakupinga kunahitaji ujasiri wa hali ya juu. Kama ilivyotokea kwa Mandela, alikuwa na ujasiri wa kuweza kusimama na kupinga ubaguzi hata baada ya kufungwa jela miaka 27. Wafanyabiashara wakubwa na waliofanikiwa sana mwanzoni walipingwa, kukatishwa tamaa na hata kuchekwa kwamba mawazo yao ya biashara hayawezi kufanikiwa. Ila kutokana na ujasiri waliweza kuendelea na misimamo yao na baadae ikawa historia kubwa ya mabadiliko.

Inahitaji ujasiri wa hali ya juu kuenda tofauti na watu wengine ili kufuata ndoto zako. Inahitaji ujasiri mkubwa kuweza kufanya kazi na watu ambao wana misimamo tofauti na wewe na mkaweza kuelewana. Inahitaji ujasiri mkubwa kufanya na kusimamia maamuzi magumu ambayo wengi hawayafurahii ila yana manufaa kwao baadae. Yote haya yameweza kutengeneza viongozi wakubwa sana na walioshindwa ujasiri wa kufanya mambo haya wameishia kuwa kawaida tu.

Kutokukata tamaa wakati umeshindwa, kuweza kusimama baada ya kupata hasara kubwa na kutokuwasikiliza wanaokukatisha tamaa ni muhimu sana kwenye mafanikio ya kibiashara na kikazi. Watu wenye ujasiri wanaweza kuvuka changamoto hizo na kuwa viongozi wa mfano kwenye kazi na biashara zao.

Unaweza kujifunza ujasiri?

Huenda mpaka kufika hapa umeshaona kwamba ujasiri kwako ni kitu kigumu sana hivyo njia yako ya kuwa kiongozi imeshakutana na kizuizi kikubwa. Habari njema kwako ni kwamba unaweza kujifunza ujasiri. Unawezaje kujifunza ujasiri?

Ili uwe na ujasiri kitu cha kwanza kabisa ni lazima ujue ni nini unasimamia. Kama huna kitu unachosimamia utakubaliana na kila kitu na kama unakubaliana na kila kitu wewe sio jasiri na huwezi kupata mafanikio makubwa kwenye jambo lolote unalofanya, hilo halina ubishi. Jua ni kitu gani unasimamia, jua ni kwa nini unasimamia na jua ni nini unategemea kutoka kwenye huo msimamo wako. Hii ni kwenye maisha, familia, kazi, biashara na hata uongozi wa wananchi.

Baada ya kujua unachosimamia izidi hofu. Hofu na woga ndio vitu vinavyoondoa ujasiri kwa watu wengi. Ukiweza kuishinda hofu utaweza kukamilisha mambo mengi sana kwenye maisha yako na kuacha alama. Kama utakubaliana na hofu na kuacha kufanya mipango yako hakuna kitu kikubwa utakachofanya. Watu wenye ujasiri na waliofanikiwa sio kwamba hawana hofu ila wamechagua kuzishinda hofu zao. Chagua na wewe kushinda hofu zako na kufanya yale unayojua ni sahihi na yatawasaidia watu wengine.

Kuna faida kubwa ya kuwa na ujasiri kwenye maisha yako. Watu wenye ujasiri huwavutia watu wengine kuwa karibu nao na hivyo kuangaliwa kama kiongozi. Watu wenye ujasiri hufanya mambo makubwa na kuwafaidisha wengine hivyo wengine kutaka kufanya kama wao. Hivi ndivyo ujasiri unajenga viongozi wakubwa. Na kwa kuwa wewe unataka kuwa kiongozi mkubwa anza kwa kujenga ujasiri wako.

Kwanzia wiki ijayo tutazijadili sifa 21 za kiongozi kutoka kwenye kitabu  The 21 Indispensable Qualities of a Leader. Tutajadili sifa tatu tatu mpaka zitakapoisha. Kuhakikisha hukosi makala hizi nzuri za uongozi weka email yako hapo juu kwenye blog sehemu iliyoandikwa jiunge hapa kupata makala mpya inapotoka

Pia usiache kupitia blog hii kila jumapili ili kujifunza mengi kuhusiana na uongozi. Washirikishe marafiki zako nao ili wajifunze masomo haya ya uongozi. Pia weka maoni yako hapo chini kuhusiana na mambo ya uongozi.

Sunday, March 9, 2014

Kiongozi Anazaliwa au Anatengenezwa? Jibu Hili Hapa.

Kumekuwa na mjadala au mabishano kwa muda mrefu ikiwa kiongozi anazaliwa au anatengenezwa. Wapo wengi ambao wanaamini watu wenye sifa za uongozi wanazaliwa nazo na haziwezi kutengenezwa. Wapo wengine wanaoamini viongozi wanatengenezwa kutokana na jamii wanayoishi na elimu wanayopata.

Nani yupo sahihi hapa? Je wewe una maoni gani juu ya tabia za uongozi? Je mtu anazaliwa nazo au anazipata kutoka kwenye malezi na elimu?

Majibu yote mawili ya kiongozi kuzaliwa au kutengenezwa yapo sahihi kabisa. Ni kweli kwamba kuna watu wanazaliwa wakiwa na sifa za uongozi na kuna wengine wanajifunza uongozi kutokana na malezi na elimu wanayopata.

Kwa nini tuna upungufu mkubwa wa viongozi?

Pamoja na kwamba viongozi wanaweza kuzaliwa na wengine kutengenezwa bado tuna upungufu mkubwa sana wa viongozi kwenye jamii zetu. Hii inasababishwa na kwamba jamii haitengenezi viongozi. Hivyo viongozi pekee wanaopatikana ni wale waliozaliwa na sifa za uongozi na huwa ni wachache sana.

Mfumo wa maisha wa jamii nyingi hautengenezi viongozi. Watoto wanakuzwa bila ya kujengewa misingi ambayo inawasaidia kuweza kufanya maamuzi kama viongozi. Jamii nyingi zinalea watoto kwa kuwaepusha wasikutane na changamoto ambazo zinawafanya wafikiri zaidi. Kwa njia hii jamii sio tu kwamba haitengenezi viongozi bali inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya watoto waliozaliwa nazo. Kwenye jamii kuna watu wengi sana ambao hawana sifa za uongozi, kwa kuwa watoto wanaiga tabia za wanaowazunguka ni rahisi sana kwao kufanana na wanajamii ambao hawana sifa za uongozi.

Kitu kingine kikubwa kinachoua uongozi ni mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu hasa kwa nchi yetu Tanzania haujakaa kutengeneza viongozi. Kwanzia darasa la kwanza mpaka elimu ya chuo mtoto anafundishwa kukazania vitu vichache ili kufaulu masomo. Hapewi nafasi ya kufikiri tofauti na kuibua na kupambana na changamoto. Pia mfumo wa elimu unajenga watu kuwa na ubinafsi na kufikiria maisha yao tu badala ya kufikiri na ya wale wanaomzunguka. Kwa njia hii mfumo wa elimu unashindwa kutengeneza viongozi na inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya wenye nazo.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi, iwe umezaliwa na sifa za uongozi ama hukuzaliwa nazo. Unaweza kufufua sifa za uongozi zilizokufa ndani yako au kujifunza sifa mpya za uongozi.

Kama nilivyosema kwenye makala iliyopita ni muhimu sana wewe kuwa kiongozi(kuisoma bonyeza hapa). Ni muhimu wewe kuwa kiongozi kwa sababu wote wanaofanikiwa kwenye chochote wanachofanya wanasifa za uongozi. Ili uweze kufanikiwa kwenye biashara, kazi, sanaa, michezo na hata uongozi wa kisiasa ni lazima uwe na sifa za uongozi. Hata kwenye malezi ya familia, wazazi wenye sifa za uongozi wanalea familia zao vizuri na kuwa na watoto wanaoweza kuendesha maisha yao vizuri.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi mzuri na ukafanikiwa sana kwenye shughuli zako. Unaweza kujifunza sifa na tabia za uongozi na ukaanza kuzitumia kwa mafanikio yako. Kuna vitabu na maandiko mengi sana yanayozungumzia uongozi. Unaweza kutafuta na kuanza kusoma, ila kama unaona huna muda wa kutosha unaweza kuwa unajifunza kupitia blog hii. Kila wiki kutakuwa na makala moja inayohusiana na uongozi hivyo unaweza kuwa unakuja kujifunza hapa. Pia ili kuhakikisha hukosi makala yoyote inayohusiana na uongozi au mengineyo weka jina na email yako hapo juu kwenye blog na utapata makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu tutengeneze viongozi wa kuliinua taifa letu kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo kwa ujumla. Hili ni jukumu letu sote.

Kiongozi Anazaliwa au Anatengenezwa? Jibu Hili Hapa.

Kumekuwa na mjadala au mabishano kwa muda mrefu ikiwa kiongozi anazaliwa au anatengenezwa. Wapo wengi ambao wanaamini watu wenye sifa za uongozi wanazaliwa nazo na haziwezi kutengenezwa. Wapo wengine wanaoamini viongozi wanatengenezwa kutokana na jamii wanayoishi na elimu wanayopata.

Nani yupo sahihi hapa? Je wewe una maoni gani juu ya tabia za uongozi? Je mtu anazaliwa nazo au anazipata kutoka kwenye malezi na elimu?

Majibu yote mawili ya kiongozi kuzaliwa au kutengenezwa yapo sahihi kabisa. Ni kweli kwamba kuna watu wanazaliwa wakiwa na sifa za uongozi na kuna wengine wanajifunza uongozi kutokana na malezi na elimu wanayopata.

Kwa nini tuna upungufu mkubwa wa viongozi?

Pamoja na kwamba viongozi wanaweza kuzaliwa na wengine kutengenezwa bado tuna upungufu mkubwa sana wa viongozi kwenye jamii zetu. Hii inasababishwa na kwamba jamii haitengenezi viongozi. Hivyo viongozi pekee wanaopatikana ni wale waliozaliwa na sifa za uongozi na huwa ni wachache sana.

Mfumo wa maisha wa jamii nyingi hautengenezi viongozi. Watoto wanakuzwa bila ya kujengewa misingi ambayo inawasaidia kuweza kufanya maamuzi kama viongozi. Jamii nyingi zinalea watoto kwa kuwaepusha wasikutane na changamoto ambazo zinawafanya wafikiri zaidi. Kwa njia hii jamii sio tu kwamba haitengenezi viongozi bali inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya watoto waliozaliwa nazo. Kwenye jamii kuna watu wengi sana ambao hawana sifa za uongozi, kwa kuwa watoto wanaiga tabia za wanaowazunguka ni rahisi sana kwao kufanana na wanajamii ambao hawana sifa za uongozi.

Kitu kingine kikubwa kinachoua uongozi ni mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu hasa kwa nchi yetu Tanzania haujakaa kutengeneza viongozi. Kwanzia darasa la kwanza mpaka elimu ya chuo mtoto anafundishwa kukazania vitu vichache ili kufaulu masomo. Hapewi nafasi ya kufikiri tofauti na kuibua na kupambana na changamoto. Pia mfumo wa elimu unajenga watu kuwa na ubinafsi na kufikiria maisha yao tu badala ya kufikiri na ya wale wanaomzunguka. Kwa njia hii mfumo wa elimu unashindwa kutengeneza viongozi na inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya wenye nazo.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi, iwe umezaliwa na sifa za uongozi ama hukuzaliwa nazo. Unaweza kufufua sifa za uongozi zilizokufa ndani yako au kujifunza sifa mpya za uongozi.

Kama nilivyosema kwenye makala iliyopita ni muhimu sana wewe kuwa kiongozi(kuisoma bonyeza hapa). Ni muhimu wewe kuwa kiongozi kwa sababu wote wanaofanikiwa kwenye chochote wanachofanya wanasifa za uongozi. Ili uweze kufanikiwa kwenye biashara, kazi, sanaa, michezo na hata uongozi wa kisiasa ni lazima uwe na sifa za uongozi. Hata kwenye malezi ya familia, wazazi wenye sifa za uongozi wanalea familia zao vizuri na kuwa na watoto wanaoweza kuendesha maisha yao vizuri.

Hata wewe unaweza kuwa kiongozi mzuri na ukafanikiwa sana kwenye shughuli zako. Unaweza kujifunza sifa na tabia za uongozi na ukaanza kuzitumia kwa mafanikio yako. Kuna vitabu na maandiko mengi sana yanayozungumzia uongozi. Unaweza kutafuta na kuanza kusoma, ila kama unaona huna muda wa kutosha unaweza kuwa unajifunza kupitia blog hii. Kila wiki kutakuwa na makala moja inayohusiana na uongozi hivyo unaweza kuwa unakuja kujifunza hapa. Pia ili kuhakikisha hukosi makala yoyote inayohusiana na uongozi au mengineyo weka jina na email yako hapo juu kwenye blog na utapata makala hizi moja kwa moja kwenye email yako.

Karibu tutengeneze viongozi wa kuliinua taifa letu kijamii, kisiasa, kiuchumi na kimaendeleo kwa ujumla. Hili ni jukumu letu sote.

Sunday, March 2, 2014

Ni Muhimu Sana Wewe Kuwa Kiongozi.

  Katika safari ya malengo yangu ya kuwa rais wa Tanzania ifikapo mwaka 2040 moja ya maandalizi makubwa ni kujenga sifa za uongozi ndani yangu. Katika kujenga sifa kwangu mimi namkaribisha yeyote anayetaka kujenga sifa za uongozi ndani yake tuwe pamoja kwenye safari hii.

Nani anatakiwa kuwa kiongozi?

Dunia ya sasa inahitaji viongozi zaidi ya kitu kingine chochote. Kila mtu anatakiwa kuwa kiongozi na kuwa na sifa ya uongozi ndani yake.

Watu wengi wakisikia neno KIONGOZI AU UONGOZI mawazo yao yanakwenda moja kwa moja kwenye mambo ya siasa au taasisi mbalimbali. Ni kweli kwamba tunahitaji viongozi kwenye nafasi za kisiasa ama nyinginezo lakini tunahitaji viongozi wengi zaidi ya hapo.

  Uongozi ni mfumo wa maisha, uongozi ni uwezo wa kushawishi watu kuchukua hatua kwa faida yao wenyewe na uongozi ni uwezo wa kubadilisha maono kwenda kwenye uhalisia. Tabia zote hizi zinahitajika kwenye maisha yetu kuanzia kwenye familia, kazi, biashara na maendeleo.

  Ili uweze kulea familia ambapo wanafamilia wanajiamini na kuweza kufanya maisha yao kuwa bora unahitaji kuwa kiongozi mzuri.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye kazi yoyote unayofanya iwe umejiajiri au umeajiriwa ni muhimu sana kutumia sifa za uongozi zilizopo ndani yako.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye biashara ni muhimu sana kuwa kiongozi. Kuweza kuanzisha biashara ndogo na ikakua mpaka kufikia kampuni kubwa sana ni lazima uwe kiongozi mwenye maono na ushawishi mkubwa.

  Ni vigumu sana kufanikiwa kwenye dunia ya sasa kama huna sifa za uongozi ndani yako. Wote wanaofanya vizuri kwenye maisha, biashara, kazi na hata burudani ukiwafuatilia kwa karibu wamakuwa na sifa za uongozi ndani yao.

   Tumekosa viongozi

  Tumefika hapa tulipo kama taifa kwa sababu tumekosa viongozi wenye sifa za uongozi. Tumekosa viongozi kwenye nafasi za kisiasa na tumekosa viongozi kwenye kila nyanja ya maisha kuanzia ngazi ya familia mpaka kwenye biashara.

  Wengi walioshikilia nafasi za kisiasa sio viongozi, wako pale kwa maslahi yao binafsi na hili limetugharimu sana mpaka sasa.

  Tumekosa uongozi kwenye familia ndio maana sasa hivi maadili yanaporomoka kwa kasi kubwa sana. Tumekosa uongozi mzuri kwenye kazi na biashara ndio ndio maana watu wanaishia kuigana na kushindana mwishowe kupotezana

  Tunahitaji viongozi wengi wenye sifa za uongozi ili tuweze kuendelea kama taifa.

  Katika shughuli yoyote unayofanya unahusisha watu na ili uweze kufanya kazi vizuri na watu mbalimbali ambao wana mitazamo mbalimbali utafanikiwa endapo tu una sifa za uongozi. Tofauti na hapo kazi inaweza kuwa ngumu sana kwako.

  Wewe unahitaji kuwa kiongozi kwenye sehemu yako ya kazi, unahitaji kuwa kiongozi kwenye biashara yako, unahitaji kuwa kiongozi kwenye familia yako na una jukumu la kutengeneza viongozi wengi zaidi kwa maendeleo ya taifa letu.

  Kama upo tayari kuwa kiongozi jiunge nami kwenye safari hii na tujifunze na kuendeleza sifa za uongozi zilizopo ndani yetu. Weka jina lako na email yako hapo juu kwenye blog ili upate kila makala ya uongozi inapotoka moja kwa moja kwenye email yako.

  Katika safari hii tutajifunza uongozi, sifa za viongozi, uongozi na maendeleo, uongozi na siasa na jinsi ya kufanya maamuzi mbalimbali kama kiongozi.

  Tuache kulalamika sasa na tuwe sehemu ya suluhisho kwa kuanza kuchukua hatua.

Ni Muhimu Sana Wewe Kuwa Kiongozi.

  Katika safari ya malengo yangu ya kuwa rais wa Tanzania ifikapo mwaka 2040 moja ya maandalizi makubwa ni kujenga sifa za uongozi ndani yangu. Katika kujenga sifa kwangu mimi namkaribisha yeyote anayetaka kujenga sifa za uongozi ndani yake tuwe pamoja kwenye safari hii.

Nani anatakiwa kuwa kiongozi?

Dunia ya sasa inahitaji viongozi zaidi ya kitu kingine chochote. Kila mtu anatakiwa kuwa kiongozi na kuwa na sifa ya uongozi ndani yake.

Watu wengi wakisikia neno KIONGOZI AU UONGOZI mawazo yao yanakwenda moja kwa moja kwenye mambo ya siasa au taasisi mbalimbali. Ni kweli kwamba tunahitaji viongozi kwenye nafasi za kisiasa ama nyinginezo lakini tunahitaji viongozi wengi zaidi ya hapo.

  Uongozi ni mfumo wa maisha, uongozi ni uwezo wa kushawishi watu kuchukua hatua kwa faida yao wenyewe na uongozi ni uwezo wa kubadilisha maono kwenda kwenye uhalisia. Tabia zote hizi zinahitajika kwenye maisha yetu kuanzia kwenye familia, kazi, biashara na maendeleo.

  Ili uweze kulea familia ambapo wanafamilia wanajiamini na kuweza kufanya maisha yao kuwa bora unahitaji kuwa kiongozi mzuri.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye kazi yoyote unayofanya iwe umejiajiri au umeajiriwa ni muhimu sana kutumia sifa za uongozi zilizopo ndani yako.

  Ili uweze kufanikiwa kwenye biashara ni muhimu sana kuwa kiongozi. Kuweza kuanzisha biashara ndogo na ikakua mpaka kufikia kampuni kubwa sana ni lazima uwe kiongozi mwenye maono na ushawishi mkubwa.

  Ni vigumu sana kufanikiwa kwenye dunia ya sasa kama huna sifa za uongozi ndani yako. Wote wanaofanya vizuri kwenye maisha, biashara, kazi na hata burudani ukiwafuatilia kwa karibu wamakuwa na sifa za uongozi ndani yao.

   Tumekosa viongozi

  Tumefika hapa tulipo kama taifa kwa sababu tumekosa viongozi wenye sifa za uongozi. Tumekosa viongozi kwenye nafasi za kisiasa na tumekosa viongozi kwenye kila nyanja ya maisha kuanzia ngazi ya familia mpaka kwenye biashara.

  Wengi walioshikilia nafasi za kisiasa sio viongozi, wako pale kwa maslahi yao binafsi na hili limetugharimu sana mpaka sasa.

  Tumekosa uongozi kwenye familia ndio maana sasa hivi maadili yanaporomoka kwa kasi kubwa sana. Tumekosa uongozi mzuri kwenye kazi na biashara ndio ndio maana watu wanaishia kuigana na kushindana mwishowe kupotezana

  Tunahitaji viongozi wengi wenye sifa za uongozi ili tuweze kuendelea kama taifa.

  Katika shughuli yoyote unayofanya unahusisha watu na ili uweze kufanya kazi vizuri na watu mbalimbali ambao wana mitazamo mbalimbali utafanikiwa endapo tu una sifa za uongozi. Tofauti na hapo kazi inaweza kuwa ngumu sana kwako.

  Wewe unahitaji kuwa kiongozi kwenye sehemu yako ya kazi, unahitaji kuwa kiongozi kwenye biashara yako, unahitaji kuwa kiongozi kwenye familia yako na una jukumu la kutengeneza viongozi wengi zaidi kwa maendeleo ya taifa letu.

  Kama upo tayari kuwa kiongozi jiunge nami kwenye safari hii na tujifunze na kuendeleza sifa za uongozi zilizopo ndani yetu. Weka jina lako na email yako hapo juu kwenye blog ili upate kila makala ya uongozi inapotoka moja kwa moja kwenye email yako.

  Katika safari hii tutajifunza uongozi, sifa za viongozi, uongozi na maendeleo, uongozi na siasa na jinsi ya kufanya maamuzi mbalimbali kama kiongozi.

  Tuache kulalamika sasa na tuwe sehemu ya suluhisho kwa kuanza kuchukua hatua.